Sunday, February 25, 2024

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE YATOA MAFUNZO ITIFAKI, UZALENDO NA USALAMA MAHALI PA KAZI KWA CWT KIBITINYERERE







TAASISI ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani imetoa mafunzo ya Itifaki, Uzalendo na Usalama Mahali pa kazi kwa viongozi wa walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti na kuzindua Club ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Wilaya ya Kibiti.

Mafunzo hayo yalitolewa Februari 24, 2024 Wilayani Kibiti kwa viongozi walimu hao kutoka Chama Cha Walimu (CWT) Wilaya ya Kibiti wapokea mafunzo ya ya Itifaki, Uzalendo na Usalama yalifunguliwa na Bi Nelea Nyanguye  ofisa Usalama mahali pa kazi wa Chama Cha Walimu (CWT) Taifa.

Katibu wa Taasisi hiyo ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere Mkoa wa Pwani Ndugu Omary Punzi alifundisha mada ya Itifaki na Uzalendo na kuwaelekeza misingi ya Kiitifaki na kuwa Mzalendo wa Taifa la Tanzania.

Sadick Mchama alifundisha Usalama Mahali pa kazi ambapo mgeni rasmi Ndugu Salumu Mzanganya ofisa Tarafa Kibiti ambaye  alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Mheshimiwa Kanali Joseph Kolombo, alitoa nasaha kwa wahitimu kuwa baada ya Mafunzo hayo kuwa wanatakiwa wawe wazalendo na kuisidia Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla kisha alizindua Club ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Wilaya ya Kibiti.

Kwa Upande wa Mwenyekiti wa CWT  Wilaya ya Kibiti Ndugu Hamdani Juma na Katibu Wake Bi Crencencia Ditrick walipongeza na kushukuru kuletewa mafunzo ambapo jumla ya washiriki 130 waliopatiwa vyeti vya mafunzo na  hayo.

No comments:

Post a Comment