Tuesday, February 6, 2024

JINSI SERIKALI ILIVYOBORESHA SHULE YA SEKONDARI MWANALUGALI YAPELEKA MAMILIONI

MTAA wa Mwanalugali B Wilaya ya Kibaha umepokea kiasi cha shilingi milioni 452.6 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili madarasa saba na bwalo la chakula kwenye Shule ya Sekondari ya Mwanalugali.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Mwenyekiti wa Mtaa huo ilipo shule hiyo Deodatus Rwekaza amesema kuwa wanaishukuru serikali kwa kutoa fedha hizo ili wanafunzi wasome kwenye mazingira mazuri.

Rwekaza amesema kuwa fedha kiasi cha shilingi milioni 240 kwa ajili ya bweni moja ilitolewa na limekamilika linatumika, bweni la pili ilitolewa fedha kiasi cha shilingi milioni 120 zimetolewa na ujenzi umefikia hatua ya kupaua.

"Fedha nyingine ni kiasi cha shilingi milioni 88 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa saba ambapo sita yamekamilika moja likiwa bado tunaishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wetu Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha sekta ya elimu,"amesema Rwekaza.

Amesema kuwa fedha kiasi cha shilingi milioni 100 zometolewa kwa ajili ya ujenzi wa bwalo la wanafunzi ambalo ujenzi wake umefikia hatua ya linta.

"Shule hii pia imechimbiwa kisima kirefu kutoka kwa wafadhili kutoka taasisi ya Ishik Education and Medical Foundation ya nchi ya Uturuki tunawashukuru sana kwa msaada huo ili kukabiliana na changamoto ya maji,"amesema Rwekaza.

No comments:

Post a Comment