Mchezo huo wa fainali ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilayani Kibaha Muharakani walijinyakulia kiasi cha shilingi 500,000 na washindi watatu Tp Pwani wakijinyakulia seti ya jezi.
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Mussa Ndomba ambaye alimwakilisha mdhamini wa ligi hiyo Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema michezo ni afya na ajira.
Ndomba amesema kuwa Halmashauri itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya michezo ili vijana waweze kucheza na kujipatia ajira.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani COREFA Mohamed Lacha amesema kuwa malengo ni kutaka soka lichezwe ndani ya mkoa huo.
Lacha amesema ili soka likue ni kuwa na michezo mingi ili kuibua vipaji vingi na kuviendeleza ili kuwa na timu nzuri.
Naye meneja wa mashindano hayo Walter Mwemezi amesema jumla ya timu 16 zilichuana kwenye mashindano hayo.
Mwemezi amesema kuwa matarajio yao kwa mwakani ni kushirikisha timu nyingi ili mashindano hayo yawe na msisimko zaidi.
Kwa upande wake mwakilishi wa Koka Said Mbecha amesema kuwa Mbunge ameahidi kuendelea kusaidia michezo ili vijana wengi wapate fursa mbalimbali zilizopo kwenye michezo.
No comments:
Post a Comment