TIMU ya soka ya Zegereni Fc imetwaa ubingwa wa Likunja Cup baada ya kuifunga Visiga Veterans kwa mabao 2-0
Mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Zegereni ulihudhuriwa na mashabiki wengi licha ya mvua kubwa kunyesha.
Washindi walipata seti ya jezi na mpira mmoja huku mshindi wa pili akijinyakulia jezi seti moja ambapo zawadi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka.
Nyamka amesema kuwa michezo ni ajira hivyo mashindano hayo ni moja ya utekelezaji wa ilani ya CCM hivyo kuwataka wadau wa michezo kuandaa michezo mingi.
Amesema kuwa mbali ya michezo kuwa ajira pia ni afya hivyo wananchi washiriki michezo na wahakikishe wanadumisha ulinzi na kuwaondoa vijana kwenye matumizi ya dawa za kulevya.
Naye mwandaaji wa mashindano hayo Rashid Likunja ambaye ni mwenyekiti wa serikali ua mtaa wa Zegereni amesema kuwa jumla ya timu 12 zilishiriki mashindano hayo.
Likunja amesema mashindano hayo kwa mwaka huu ni mwaka wa 10 kuyaandaa ambapo mwakani zawadi zitaongezwa ili kuleta msisimko.
No comments:
Post a Comment