HALMASHAURI ya Mji Kibaha imeitaka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Kibaha kufanya utaratibu wa kupeleka maji kwenye Hospitali ya Wilaya ya Lulanzi ambapo ni miezi mitatu imepita tangu kutolewa hela kiasi cha milioni 60.
Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Mwenyekiti wa Halmashauri Mussa Ndomba amesema kuwa fedha hizo zipo lakini wameshindwa kuzichukua.
Mussa amesema kuwa adha ya maji kwenye Hospitali ni kubwa sana kwa matumizi mbalimbali kwa wagonjwa wakiwemo mama wajawazito hali ni mbaya sana.
Akijibu hoja hiyo Meneja wa DAWASA Kibaha Alfa Ambokile amesema kuwa mradi huo tayari amesha andikia makao makuu juu ya fedha hizo kuchukuliwa.
No comments:
Post a Comment