KATIBU wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani Ndugu Omary Punzi ametuma salamu za Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Taifa Mhe.Paul Petro Kimiti na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Taasisi Mhe.Mizengo Peter Pinda (Waziri Mkuu Mstaafu) kwa kutoa misaada mbalimbali kwa wafungwa.
Punzi amesema kuwa misaada hiyo ambayo imewalenga wafungwa imetolewa leo kwenye Gereza la Utete Wilaya ya Rufiji ikiwa inalenga kusherehekea miaka 60 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya Tarehe 12.1.1964 .
ametaja misaada iliyotolewa kuwa ni sabuni za unga na vipande, mafuta ya kupakaa, miswaki na dawa za meno pamoja na juisi katika .
Ndugu Omary Punzi aliwaomba wadau nchini wajitokeze kwa wingi kuwasaidia wafungwa Magereza kwa kutoa misaada mbalimbali kwani bado wanamahitaji mengi.
Kwa Upande wake Mkuu wa Magereza Utete Christopher Mwenda ambaye alipokea misaada hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Magereza Mkoa ameishukuru Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani kwa jinsi wanavyoendelea kuwatia moyo wafungwa siyo mara ya kwanza Taasisi hiyo kutoa misaada kwani mwaka jana walipokea katoni za sabuni boksi 50 za taulo za kike kwa ajili ya wafungwa wanawake
Aliomba wadau wajitokeze kwa wingi kuwasaidia wafungwa wanahitaji mahitaji mengi na Serikali haiwezi kufanya peke yake katika mahitaji.
Naye Monica Mbilla Mkuu wa idara ya Malezi ya Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani amesema msaada mkubwa atakao wasaidia ni kuhakikisha wanapewa elimu na Msaada wa kisheria .
No comments:
Post a Comment