Friday, January 12, 2024

KATA PICHA YA NDEGE YAISHUKURU SERIKALI KUWAPATIA MILIONI 340 UJENZI MADARASA PICHA YA NDEGE SEKONDARI



KATA ya Picha ya Ndege imefanikiwa kuongeza madarasa 17 kwenye Shule ya Sekondari Picha ya Ndege ambayo awali ilikuwa na madarasa sita lakini kwa sasa ni madarasa 23 ambapo zimetumika kiasi cha shilingi milioni 340 kwa madarasa hayo yaliyoongezeka.

Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata hiyo Karim Mtambo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi juu ya kuboreka kwa sekta ya elimu kulikofanywa na Serikali ya awamu ya sita.

Mtambo alisema kuwa ongezeko la madarasa hayo kumeondoa changamoto iliyokuwepo ya upungufu wa madarasa ambapo madarasa hayo pia yana viti vyake hivyo wanafunzi watasoma kwa raha bila ya usumbufu.

"Wakati tunaingia kwenye uongozi kulikuwa na boma la maabara mbili za Baiolojia na Kemia Serikali ilitoa milioni 60 kwa awamu ya kwanza na awamu ya ya pili ilitoa milioni 80 ambazo zimekamilisha maabara hizo ambapo bado ya Fizikia,"alisema Mtambo.

Alisema kuwa kuna baadhi ya changamoto zilizopo kwa sasa ni ukosefu wa jengo la Utawala kwaniwalimu imebidi watumie darasa moja kama ofisi kwa ajili ya shughuli zao ambapo walipeleka ombi Halmashauri ili kujengewa jengo la Utawala.

"Changamoto nyingine ni vyoo vya walimu ambapo imebidi watumie matundu ya vyoo vya wanafunzi moja kwa walimu wanawake na walimu wanaume na tumeongea na wazazi watoe tofali tano ili kuwajengea choo walimu kwani jambo ambalo siyo sawa,"alisema Mtambo.

Aidha alisema kulikuwa na changamoto ya maji ambapo walipewa milioni 10 na Halmashauri na kuvuta maji lakini bomba wanalotumia majo yanatoka kwa mgao lakini mradi wa Pangani ukikamilika maji yatapatikana muda wote.

No comments:

Post a Comment