Thursday, January 11, 2024

WATANZANIA WATAKIWA WAPANDE MITI KULINGANA NA UMRI WAO

WATANZANIA wametakiwa kuadhimisha siku za kumbukumbu zao za kuzaliwa kwa kupanda miti kutokana na umri wao ili kukabili mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yalisemwa na Brigadia Jenerali Mstaatu Martin Kemwaga mwasisi wa kampeni ya Miti kwa Umri alipozungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kuwa malengo yake ni kuifanya nchi kuwa ya kijani.

Kemwaga alisema kuwa kampeni hiyo ambayo alianza miaka mitano iliyopita ambapo ilizinduliwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete eneo la Msata Wilayani Bagamnoyo mkoani Pwani kwenye Hoteli ya Makmar ambayo yeye ni Mtendaji Mkuu.

"Namshukuru Rais Mstaafu Dk Kikwete kwa kutuzindulia kampeni yetu ambayo mimi na familia yangu, marafiki na vikundi mbalimbali huwa tunapanda miti kutokana na umri wetu na ningependa kila Mtanzania apande miti kutokana na umri wake,"alisema Kemwaga.

Alisema kuwa Watanzania waadhimishe siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti badala ya kutumia
gharama kubwa za kukumbuku za kukumbuka siku siku zao za kuzaliwa ambapo idadi ya Watanzania.

"Watu watumie maeneo ya taasisi za Umma kama vile kwenye Mashule, Hospitali, Zahanati, Polisi na vyuo na maeneo mbalimbali ya wazi ambapo miti ikipandwa kutasaidia hali ya hewa kuwa nzuri na kuondokoana na arhari za mabadiliko tabianchi,"alisema Kemwaga.

Aidha alisema kuwa Utamaduni huo warithishwe watoto ili wawe wanafanya hivyo ambapo ndani ya muda mnfupi nchi itakuwa na miti mingi na kukabili changamoto mbalimbali za hali ya hewa inayojitokeza
kutokana na ukosefu wa miti.

Aidha alisema kuwa katika eneo ambalo wamepanda miti wanaifuatilia ili kuhakikisha inakuwa na kama
mtu kapanda atakuwa anafuatilia mti alioupanda tofauti na baadhi ya taasisi zimekuwa zikipanda miti lakini hawaifuatili na kufa.

No comments:

Post a Comment