Friday, October 24, 2014

POLISI WAKAMATA LUNDO LA SILAHA, FEDHA NA VITU MBALIMBALI

Na John Gagarini, Kibaha
WATU watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamekamatwa wakiwa na silaha aina ya Short Gun yenye namba 07019302 ikiwa na risasi nane.
Hayo yamesemwa na kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alipoongea na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Mohamed Kalipa (20) dereva wa Bajaji mkazi wa Mbagala Rangi Tatu, Salum Shekivui (20) mkazi wa Buza na Seuli Lucas (18) makazi wa Mbagala Rangi Tatu Jijini Dar es Salaam.
Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa Oktoba 20 mwaka huu majira ya saa 2:30 huko Mlandizi wilaya ya Kibaha.
“Mbali ya silaha pia walikutwa na fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 6,611,800, vocha mbalimbali za simu zenye thamani ya shilingi milioni 2,185,500 na simu za mkononi sita za aina mbalimbali ambazo thamani yake bado hazijafahamika,” alisema Kamanda Matei.
Aaidha alisema kuwa watuhumiwa hao wanadaiwa kuwa walifanya tukio la unyanganyi wa kutumia silaha huko Kijiji cha Mbwewe wilaya ya Bagamoyo kwenye duka la Twaha Mbuta siku ya Oktoba 19 saa 1:30 usiku na kupora kiasi cha shilingi milioni 30,000,000.
“Baada ya kukamatwa walimtaja mtuhumiwa mwenzao ambaye  walikuwa wakishirikiana naye Samwel Joseph mkazi wa Kongowe Kibaha ambapo baada ya upekuzi walimkuta na risasi sita za Short Gun ambazo alikuwa akizimiliki bila ya kibali hata hivyo mtuhumiwa huyo alitoroka,” alisema Kamanda Matei.
Katika tukio lingine watu wawili walikamatwa kwa tuhuma za wizi wa ngombe 61 wenye thamani ya shilingi milioni 27,450 ,000 mali ya Keke Furaha (37) kwa kutumia silaha aina ya sime.
Alibainisha kuwa tukio hilo limetokea Oktoba Mosi mwaka huu majira ya saa 5 asubuhi huko Lulenge kata ya Ubena wilayani Bagamoyo ambapo watuhumiwa ni Sadala Lupoto (25) mkazi wa Kimamba Kilosa na Luseky Sogoyo (25) na juhudi za kuwatafuta ngombe wengine 39 zinaendelea.  
Katika tukio lingine watu wawili wanashikiliwa kwa tuhuma za kukutwa na silaha aina ya gobore bila ya kibali  huku wengine 11 walikamatwa kwenye matukio ya kukutwa na bangi gunia mbili na kete 250 pamoja na lizla zipatazo 100.
            
Mwisho.









Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei akionyesha moja ya silaha zilizokamatwa kwa watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi. 

Silaha mbalimbali ambazo jeshi la polisi mkoani Pwani limezikamata mara baada ya kufanya misako maeneo mbalimbali ya mkoa huo. 

 Redio na deki vilivyoibiwa na kukamatwa kwa watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi. 

  Bunduki, tv, simu na vifaa vingine ambavyo vilikamatwa na polisi baada ya kuibiwa kwa watu mbalimbali mkoani humo.

Silaha pamoja na kiasi kikubwa cha fedha ambazo ziliibiwa kwa mfanyabiashara Twaha Mbuta wa huko Mbwewe. 

Sehemu ya fedha, vocha na risasi zilizokamatwa na polisi baada ya kufanya masako wa kusaka majambambazi.

 Redio zilizoibiwa kwa watu mbalimbali mkoani Pwani baada ya polisi kufanya misako mkoani humo
Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Ulrich Matei akiongea na waandishi wa habari mjini Kibaha hawapo pichani

No comments:

Post a Comment