Na John Gagarini,
Bagamoyo
JIMBO la Jilin nchini
China limekubali kuwekeza hapa nchini kwenye eneo la Uwekezaji la (EPZ) la
Kamal lililopo Kijiji cha Kerege kwa Kiwete wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Uwekezaji huo
utafanyika baada ya ujio wa baadhi ya viongozi wa Jimbo hilo kutembelea maeneo
mbalimbali ya uwekezaji wilayani humo na kuonekana kuvutiwa na sehemu hiyo.
Akizungumza jana mara
baada ya kutembelea maeneo kadhaa akiongozana na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu
Mahiza na sekretarieti ya mkoa wa Pwani na kuvutiwa na eneo hilo la uwekezaji
la EPZ, Naibu Gavana wa Jimbo hilo Zhoncheng Sui alisema ameridhika na eneo
hilo.
Sui alisema kuwa
kutokana na urafiki wa kihistoria uliyopo kati ya Tanzania na China toka enzi
za viongozi wa mataifa hayo Mwalimu Julius Nyerere na Mao Tse Sung kumekuwa na
ushirikiano ambao ni wa damu hivyo lazima udumishwe kwa ushirikiano wa
kimaendeleo.
“Tumeona mambo mengi
ambayo tunaweza kushirikiana ambapo moja ni pale kwenye eneo la uwekezaji
ambapo tutakuja kuwekeza hapo kwani kuna miuondombinu mizuri ya barabara, maji
na umeme pia waiteni na wenzetu waliopo hapa Tanzania ili nao waje wajionee na
kuangalia namna wanavyoweka kuwekeza kwenye mkoa huu wa Pwani,” alisema Sui.
Awali akimkaribisha
naibu gavana wa Jimbo hilo la Jilin mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza
alisema kuwa mkoa wa Pwani una mambo mengi ambayo wawekezaji wanaweza kuwekeza
ikiwa ni pamoja na kwenye kilimo, uvuvi, utalii na mifugo.
“Fursa zipo nyingi
ndani ya mkoa wetu na hata miundombinu ya barabara, anga, bandari, uememe na
reli viko vizuri kwa ajili ya kufanikisha uwekezaji ambao una hitaji uwepo wa
mawasiliano mazuri,” alisema Mahiza.
Ujumbe huo ulikuwa na
ziara ya siku moja wilayani Bagamoyo kutembelea
maeneo ya uwekezaji kwenye ujenzi wa soko la kimataifa la samaki, eneo
itakapojengwa bandari na eneo la uwekezaji la Kamal.
Mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza kulia akiteta jambo na kiongozi wa ujumbe kutoka Jimbo la Jilin nchini China Zhongcheng Sui wali[potembelea wilaya Bagamoyo kuangalia maeneo ya uwekezaji |
Mkuu wa mkoa katikati na ugeni kutoka nchini China wakiangalia bomba ambalo limetoboka na maji kumwagika, kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi |
No comments:
Post a Comment