Thursday, October 2, 2014

MABANDA UMIZA YAONGEZA VITENDO VYA UBAKAJI

Na John Gagarini, Kibaha
BAADHI ya wadau wa watoto wilayani Kibaha mkoani Pwani wameiomba serikali kuyafutia usajili mabanda ya video ambayo yamekuwa chanzo kikuu cha watoto wadogo kufanyiwa vitendo vya ubakaji.
Mabanda hayo yamekuwa yakitumiwa na baadhi ya watu wazima ambao wanawafanyia watoto hao vitendo hivyo baada ya kuwarubuni kuwaingiza kwenye mabanda hayo kisha kuwapakata na kuwaingilia watoto hao ikiwa ni pamoja na kinyume cha maumbile.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mratibu wa shirika lisilo la kiserikali la (KICODET) Dk Rose Mkonyi wakati wa mafunzo ya kupinga vitendo vya ukatili kwa watoto kwa wadau mbalimbali kwenye kata ya Kibaha wilayani humo  alisema moja ya vyanzo vya ongezeko la vitendo vya ubakaji watoto ni mabanda hayo.
“Vitendo vya ubakaji watoto ambapo ni moja ya ukatili vimekithiri na kuongezeka wilayani Kibaha na moja ya sababu ni mabanda hayo ambayo yanaonyesha video chafu za ngono bila ya kujali umri,” alisema Dk Mkonyi.
Dk Mkonyi alisema kuwa mabanda hayo yamejaa kwenye mitaa na vijiji hayajali umri licha ya sheria kutaka watoto wenye umri chini ya miaka 18 kutoingia lakini wamiliki wamekuwa wakiwaruhusu watoto hao ambao ni wanafunzi kuingia pia kufunguliwa muda wa kazi ambapo wanafunzi hao wamekuwa wakiishia humo na kuacha kwenda shule.
Kwa upande wake mwezeshaji wa mafunzo hayo Faustina Kayombo ambaye ni ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha alisema kuwa tatizo kubwa ni usiri unaofanywa na umaskini imekuwa ni chanzo kikuu cha kuendela kwa vitendo hivyo.
Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mwenyekiti wa mafunzo hayo Alkhas Katopola alisema kuwa mafunzo hayo yamtawafanya waweze kujua namna ya kukabilina na vitendo hivyo ndani ya jamii ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwenye vyombo vya sheria.
Katopolo alisema kuwa baadhi ya matukio hayo yamekuwa yakiendelea kutokana na wanafamilia kuficha kuogopa mahusiano mabaya au kurubunia kwa kupewa fedha ili wasitoe taarifa za vitendo hivyo.
Mradi huo ni wa miaka miwili ambapo mafunzo hayo yamefadhiliwa na Plan International, UNICEF, Save the Children na Jumuiya ya Ulaya na serikali kwa kushirikiana na shirika hilo la KICODET.
Mwisho.

   



No comments:

Post a Comment