Na John Gagarini, Kibaha
KWAYA
na Waimbaji wa nyimbo za Injili nchini wameshauriwa kujisajili Baraza la Sanaa
ili watambulike kisheria kwa lengo la kuepuka kudhulumiwa haki za kazi zao.
Hayo
yalisemwa mjini Kibaha mwishoni mwa wiki na Naibu Waziri wa Sheria na Katiba
Angella Kairuki wakati alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuchangia fedha za
kununulia vifaa vya mawasiliano na kurekodi albamu ya video ya kwaya ya kanisa
la Sabato la Maili Moja Kibaha mkoani Pwani.
Waziri Kairuki alisema kuwa baadhi ya
kwenye makanisa ya na waimbaji mbalimbali hawajaona umuhimu wa kujisajili ili
ziweze kutambulika na kunufaika kama zilivyo kazi nyingine za sanaa.
“Kwaya na waimbaji wa nyimbo za injili
nazo zinawajibu wa kujisajili katika baraza hilo ili ziweze kupata haki zao pamoja
fursa mbalimbali pia kukabiliana na baadhi ya watu wanaotumia kazi zao
kujinufaisha binafsi huku walengwa wakiwa hawaambulii kitu hivyo sio vyema
kukaa bila kujisajili rasmi,” alisema Waziri Kairuki.
Alisema ameona ni vyema akawahimiza kwani
jambo hilo lina manufaa kwa waimbaji na
kwaya za makanisa ili waweze kupiga hatua kama ilivyo kwa baadhi ya wasanii
wengine wa nyimbo za injili ambao tayari wamepiga hatua.
Alibainisha kuwa muziki unachangia
amani,upendo na mshikamano hivyo wajitahidi pia kuimba nyimbo za kuiombea nchi
yetu kwa masuala hayo muhimu pamoja na kumtukuza mungu.
“Nawaomba wanakwaya wa nyimbo na
waimbaji wa nyimbo za injili kutengeneza albamu za video zenye maadili kwa
michezo na mazingira yake pasipo kwenda kinyume na maadili ya kidini na kugeuza
injili kuwa biashara, kwani zipo baadhi ya kanda za wasanii wengine ambazo
hazionyeshi maadili mazuri,” alisema Waziri Kairuki.
Waziri Kairuki alisema serikali ipo
pamoja na wasanii wa aina zote na inatambua kazi za sanaa ,tasnia ya wasanii na
ndio maana katika katiba inayopendekezwa walihakikisha wanatambua kazi za
wasanii, katika
hafla hiyo kulipatikana zaidi ya sh m 22 ambapo ahadi zilizotolewa ni zaidi ya
Mil 19.
Mwisho
No comments:
Post a Comment