Na John Gagarini,
Kibaha
KIJANA mwenye umri
kati ya miaka (25) na (30) anayedahaniwa kuwa ni kibaka ambaye jina lake
halikuweza kufahamika ameuwawa kwa kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kwa
tuhuma za kuiba pikipiki.
Wananchi hao walifikia
hatua hiyo baada ya kubaini kuwa mtuhumiwa huyo akiwa na mwenzake waliiba
pikipiki hiyo huko Gairo mkoani Morogoro na kutaka kuiuza Chalinze wilayani
Bagamoyo mkoani Pwani.
Akithibitisha kutokea
kwa tukio hilo kaimu kamanda wa Polisi mkoani humo Athuman Mwambalaswa alisema
kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 25 mwaka huu majira ya saa 1 asubuhi eneo la
Pera Chalinze wilaya ya Bagamoyo.
Kamanda Mwambalaswa
alisema kuwa watuhumiwa hao wawili walikuwa na pikipiki ainaya ya Toyo yenye
namba za usajili T 336 BZC ambayo inadhaniwa kuwa waliiba huko Gairo na
walifika Chalinze kwa lengo la kutaka kuiuza.
“Vijana hao ambao ni
wa kabila la Kimasai walifika hapo huku wakitafuta wateja wa pikipiki hiyo na
wananchi hao walipowauliza uthibitisho wa pikipiki hiyo yaani kadi walishindwa
kuonyesha na ndipo walipoanza kuwapiga na mmoja alifanikiwa kukimbia huku
mwingine akipigwa kisha kuchomwa moto,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Alisema kuwa mwili wa
marehemu ulikutwa mashambani ukiwa umechomwa moto na kuharibika vibaya sehemu
mbalimbali za mwili.
Aidha aliwataka
wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na
kuwataka kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria ikiwa ni pamoja na polisi ili
hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment