Tuesday, November 5, 2024

TAKUKURU PWANI KUTOA ELIMU KUPAMBANA NA RUSHWA



TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani itaendelea kutoa elimu ya kupambana na rushwa kwa makundi mbalimbali wakati huu wa mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.
Aidha makundi hayo ni pamoja na viongozi wa vyama vya siasa, wapiga kura, wagombea, wasimamizi, azaki, taasisi za dini, mashirika yasiyo ya kiserikali na waandishi wa habari.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Takukuru Mkoani humo Christopher Myava alisema walishatoa elimu juu ya kupambana na vitendo vya rushwa tangu mchakato wa uchaguzi ndani ya vyama vya siasa.

Myava alisema kuwa makundi hayo ni muhimu kipindi hichi cha uchaguzi lengo likiwa ni kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa hawatokani na rushwa.

"Tunataka wananchi wachague viongozi bora ambao wataendana na dira ya serikali ya maendeleo kwani serikali inatumia gharama kubwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo hivyo viongozi watakaochaguliwa wawe na sifa na uwezo wa kuongoza,"alisema Myava.

Alisema kuwa wanatoa elimu kwa makundi hayo ili kama yataona kuna viashiria vya rushwa waweze kutoa taarifa ili hatua ziweze kuchukuliwa kwani viongozi bora hawatokani na kutoa rushwa bali ni kwa uwezo wao wa kuongoza.

"Tutaendelea kutoa elimu hadi itakapofikia hatua ya kutangaza matokeo ili tuhakikishe wanapatikana viongozi wenye sifa, waadilifu ili wasimamie rasilimali na fedha zinazotolewa ili wananchi wapate maendeleo,"alisema Myava.

Aliongeza kuwa kiongozi atakayechaguliwa apambane na rushwa kwani serikali inatumia gharama kubwa hivyo tutatoa elimu kupitia mikutano na semina.

"Wananchi nao ni sehemu ya mapambano ambapo viashiria vya rushwa ni kama vile kupewa simu, ajira, fedha, ahadi mbalimbali au vitu vya thamani katika hatua za mwanzo tulipata taarifa za vitendo vya rushwa lakini hakuna ushahidi ambao unaweza kutumika kwani ili kufungua shauri lazima kusiwe na shaka,"alisema Myava.

Aliwataka viongozi wanaowania nafasi za uongozi wazingatie sheria, masharti, kanuni na utaratibu wa uchaguzi ili wasije kujikuta wanaingia kwenye changamoto kwa kukiuka miongozo iliyowekwa.

Friday, November 1, 2024

WAHITIMU MAFUNZO JESHI LA AKIBA WAOMBA AJIRA HALMASHAURI

WAHITIMU wa mafunzo Jeshi la akiba Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani wameomba kufikiriwa katika kupata ajira kwenye Halmashauri walipo badala ya kufanya kazi katika makampuni binafsi ambayo huwalipa mishahara ambayo haiendani na mali wanazolinda.
Aidha wamesema kuwa wanaiomba serikali kukabili changamoto ambazo zingetatuliwa basi vijana wengi wangeshiriki na kumaliza mafunzo hayo kwani baadhi wanashindwa kununua sare kutokana na hali ya kiuchumi.

Walitoa maombi hayo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga amnaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla fupi ya kufunga mafunzo ya Jeshi la akiba iliyofanyika kwenye uwanja wa Mwanakalenge.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi mshauri wa mgambo wa wilaya ya Bagamoyo Luteni Kanali Rahimu Tumbi alisema kuna baadhi ya changamoto wanazopata wahitimu wa mafunzo hayo kipindi wanapokuwa kwenye mafunzo hayo.

Mkuu wa wilaya ambae ndio mgeni rasmi Shaibu Ndemanga ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana waliomaliza mafunzo ya Jeshi la akiba wakaishi kiapo walicho kiapa kwa kuwa waadilifu na wasiyatumie mafunzo vibaya wanapokuwa kwenye jamii.


Tuesday, October 29, 2024

VIJANA NCHINI KUPEWA ELIMU SERA YA VIJANA

ILI kuwapa ufahamu juu ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka (2007) toleo la mwaka 2024 Kamati ya Vijana Wazalendo itafanya makongamano kwenye mikoa 10 hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari mratibu wa Kamati ya Vijana Wazalendo Omary Punzi amesema kuwa Makongamano hayo yatakutanisha makundi ya vijana ambayo yatapatiwa elimu juu ya sera hiyo.

Punzi amesema kuwa sera hiyo ya vijana ni nzuri lakini vijana wengi hawaifahamu hali ambayo inawafanya vijana wengi kutotambua haki zao za msingi na makongamano hayo yatawafikia vijana zaidi ya milioni nane na tisa.

Mwenyekiti wa Kamati ya vijana Wazalendo Farida Kongoi amesema kuundwa kwa sera ya taifa ya maendeleo ya vijana lengo lilikuwa ni vijana wapate mwongozo wa kuendana na masuala ya siasa na kijamii ikiwa ni pamoja na mwelekeo wa kiteknolojia.

Mwanasheria wa Kamati ya vijana Wazalendo Godfrey Kizito amesema pia vijana watafafanuliwa kuhusu Sheria zinazohusu haki na masuala ya vijana.

Naye Mkurugenzi wa Great leaders organization na Mratibu na Mwandaaji wa kongamano la Wazazi na Walezi nchini Dubai Dk Debora Nyamlundwa amesema katika kongamano hilo kuna kujifinza fursa mbalimbali zilizopo katika taifa hilo kuja kuendeleza hapa nchini



Sunday, October 27, 2024

NISHIBISHE PROJECT YAKUSANYA UNGA KILO 1,115 WANAFUNZI KUNUFAIKA CHAKULA SHULENU

MPANGO wa Nishibishe umefanikisha kupatikana kwa unga wa mahindi kiasi cha kilogramu 1,115 kwa ajili ya kuwapatia lishe wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari kwenye Kata ya Kwala Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

Hayo yalisemwa na Diwani wa Viti Maalum ambaye pia ndiye mwasisi wa mpango huo Josephine Gunda wakati wakukabidhi unga huo kwa viongozi wa Kata ili wasambaze kwenye shule husika.

Gunda alisema unga huo umetolewa na wadau mbalimbali kupitia mradio huo ambapo utasambazwa kwenye Shule ya Sekondari moja na Shule za Msingi tatu.

"Malengo ya kutoa chakula shuleni ni ili kupunguza utoro kwa baadhi ya wanafunzi kwani wanakumbana na changamoto ya chakula na kusababisha kutohudhuria masomo kutokana na hali ya kiuchumi,"alisema Gunda.

Alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakila mmlo mmoja ambapo mtoto anaenda shule bila ya kula chochote hadi jioni anaporudi kutoka shule hali ambayo inawafanya washindwe kuhudhuria masomo na kuwa watoro.

"Shuleni kukiwa na chakula hata kama nyumbani kuna changamoto mtoto atakula shuleni na atavutiwa kwenda shule na mafanikio tumeyaona kwani utoro ymepungua na ufaulu umeongezeka kwani mwanafunzi akila na akili inakuwa na uwezo mzuri,"alisema Gunda.

Aliongeza kuwa ifike wakati suala la chakula shuleni iwe ajenda ya kudumu na Halmashauri itenge sehemu ya fedha ya mapato ya ndani kwa ajili ya kununua chakula kwani hilo ni tatizo kubwa kwa watoto mashuleni.

Diwani wa Kata ya Kwala Mansuri Kisebengo alisema kuwa mbali ya changamoto lakini wazazi bado wana nafasi ya kuhakikisha lishe ya watoto wao inapatikana.

Kisebengo alisema kuwa anawapongeza wadau hao ambao wamejitolea unga huo kwani watawapunguzia wazazi gharama za chakula kwa watoto wao ambao ni wanafunzi.

Kwa upande wake mratibu huduma za lishe Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Coletha Chapile alisema kuwa lishe ni kitu muhimu sana kwa wanafunzi kwani endapo mtoto hatapata chakula uwezo wake wa kuelewa utapungua.

Chapile alisema kuwa suala la lishe kwa wanafunzi ni muhimu na ni jambo ambalo wazazi, walezi na wadau kulipa kipaumbe kwa kuhakikisha watoto wanapata chakula wakiwa shuleni ili kuongeza uelewa.



Thursday, October 17, 2024

HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAKUSANYA MAPATO ASILIMIA 33 ROBO YA KWANZA


HALMASHAURI ya Mji Kibaha imefanikiwa kukusanya mapato kwa asilimia 33 ya malengo ya ukusanyaji kwenye robo ya kwanza ya makadirio ya makusanyo ya Halmashauri ya shilingi bilioni 8.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Halmashauri Dk Rogers Shemwelekwa  wakati wa kikao cha baraza la Madiwani cha robo ya kwanza ya Julai-Septemba 2024.

Shemwelekwa alisema kuwa kipindi kama hichi mwaka jana walikuwa wamekusanya kwa asilimia 25 hivyo kuvuka lengo kwa asilimia 8 ya makadirio ya shilingi bilioni 7.

"Tunawashukuru madiwani na wataalamu wa Halmashauri kwa kufikia makusanyo hayo ambayo ni mwanzo mzuri na tunategemea kufikia asilimia 100 tunaomba ushirikiano huu uendelee ili kufikia malengo tuliyoweka,"alisema Shemwelekwa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema huo ni mwanzo mzuri wa makusanyo hayo ni mazuri na ushirikiano huo uendelee ili kufikia malengo yaliyowekwa.

John alisema kuwa kwa upande wa uyoaji mikopo asilimia 10 ya Halmashauri dirisha limeshafunguliwa pia zoezi uchongaji barabara kwenye mitaa unaendelea ambapo Halmashauri imetoa milioni 10 kwa kila kata kwa ajili hiyo.

Tuesday, October 15, 2024

MKUU WA MAJESHI AWAVISHANI NISHANI MAJENERALI, MAAFISA NA ASKARI WA JWTZ




Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan amewavisha nishani mbalimbali Majenerali, Maafisa na Askari wa JWTZ Jijini Mwanza tarehe 15 Oktoba 2024.

Nishani hizo ni Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya Muungano pamoja na Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ.

Aidha,Jenerali Mkunda amewavisha nishani ya Jumuiya ya SADC Maafisa na Askari walioshiriki Ulinzi wa Amani nchini Msumbiji chini ya mwavuli wa Jumuiya hiyo.



Sunday, October 13, 2024

SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU NYERERE YAINGIA MAKUBALIANO NA CHUO CHA RENMIN CHA CHINA

SHULE ya Uongozi  ya Mwalimu Nyerere imeingia makubaliano  ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Renmin katika nyanja mbalimbali zikiwemo za mafunzo utafiti na kubadilishana wataalamu.

Wakisaini makubaliano hayo kati ya Mkuu wa Shule ya Mwalimu Nyerere Profesa Marcellina Chijoriga na kiongozi mkuu wa Chama Tawala Cha China Cha (CPC) kwenye Renmin Zhang Donggang katika Shule hiyo iliyopo Kibaha Mkoani Pwani walifurahishwa na ushirikiano huo.

Chijoriga alisema kuwa makubaliano hayo yatakuwa ni kwa ajili ya kubadilishana wataalamu ambapo wao watakuja huku na wa Tanzania watakwenda kwao ikiwa ni sehemu ya kubadilishana uzoefu.

“Chuo hicho ni kikubwa sana na cha muda mrefu na kiko vizuri kwenye masuala ya utafiti wa uandishi wa vitabu na katika masuala ya uandishi wa vitabu ambapo ushirikiano huo utakuwa na manufaa makubwa sana kwa pande zote mbili,”alisema Chijoriga.

Alisema kuwa chuo hicho cha Renmin kinauwezo mkubwa wa kuwajengea uwezo viongozi wa chama na serikali kwani kiko vizuri sana katika ufundishaji masuala hayo na watatumia uzoefu ili kujifunza kupitia kwao kwani kimeanza muda mrefu.

“Faida hiyo ni kwa vyama sita vya ukombozi Kusini mwa Afrika ambapo China ni msaidizi mzuri kwani wamesaidia ujenzi wa shule hiyo ambavyo ni CCM, FRELIMO, SWAPO, ANC na ZANU-PF ambapo CPC .  

Aidha alisema kuwa chuo hicho kilichopo Beijeng China kilianza ushirikiano mwaka jana ambapo uongozi wa Shule walikwenda na katibu mkuu wa CCM wakati ule Chongolo na sasa imeanza safari mpya na kina uzoefu mkubwa nani cha zamani sana.

“Tunashukuru sana kwani wametuonyesha ushirikiano mkubwa na makubaliano ya kutengeneza ushirikiano huu ni sasa safari mpya imeanz na leo waametupa vitabu tunawashukuru kwani maktaba yetu sasa itakuwa na vitabu vingi na wasomaji wataweza kujifunza masuala mbalimbali ya nchi ya China,”alisema Chijoriga.

Naye alisema Dk Evaristo Haule Naibu Mkuu wa Chuo Mipango Fedha na Utawala Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alisema kuwa China imefanikiwa na tumeona namna gani kutumia njia ili kuona wao wamefanyaje na kufikia hatua kubwa kiasi hicho kwenye maendeleo na CPC inavyotoa dira kuongoza nchi yao wanataka twende pamoja katika miradi yao mikubwa ya kidunia.

 Haule alisema kuwa ili kwenda pamoja hivi karibuni Rais Dk Samia Suluhu Hassan alienda China kwenye mkutano wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika wao wana dira  na kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya kazi na watu wawe na uzalendo wa nchi watu wanaangalia changamoto badala ya kuangalia fursa zilizopo.

Naye Dk Theresia Dominick kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam alisema kuwa Watanzania wanatakiwa kujifunza kwa kuwa nadhifu na wanaangalia masuala ya ulaji na wawe watu wa kujishusha na kuachana na matumizi yasiyo ya lazima na wasiwe na tamaa.

Dominick alisema  kuwa badhi ya wafanyabiashara Watanzania wamekuwa wakienda China hivyo wanapaswa kujifunza tabia za Wachina za kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya jambo wanalolifanya ni mfano wa kuigwa.

Naye kiongozi huyo Zhang Donggang alisema kuwa ushirikiano uliopo baina ya China na Tanzania nan chi nyingine ni katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo ambapo wao wanaangalia sana maslahi ya wananchi.

Donggang alisema kuwa nchi za Afrika na China zinapaswa kushikana mkono katika kuhakikisha zinapiga hatua katika masuala ya kimaendeleoili kudumisha umoja uliopo kwani umoja uliopo umeleta mafanikio makubwa.

Mwisho.