
Aidha wamesema kuwa wanaiomba serikali kukabili changamoto ambazo zingetatuliwa basi vijana wengi wangeshiriki na kumaliza mafunzo hayo kwani baadhi wanashindwa kununua sare kutokana na hali ya kiuchumi.
Walitoa maombi hayo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga amnaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla fupi ya kufunga mafunzo ya Jeshi la akiba iliyofanyika kwenye uwanja wa Mwanakalenge.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi mshauri wa mgambo wa wilaya ya Bagamoyo Luteni Kanali Rahimu Tumbi alisema kuna baadhi ya changamoto wanazopata wahitimu wa mafunzo hayo kipindi wanapokuwa kwenye mafunzo hayo.
Mkuu wa wilaya ambae ndio mgeni rasmi Shaibu Ndemanga ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana waliomaliza mafunzo ya Jeshi la akiba wakaishi kiapo walicho kiapa kwa kuwa waadilifu na wasiyatumie mafunzo vibaya wanapokuwa kwenye jamii.
No comments:
Post a Comment