Friday, November 29, 2024

DK ALICE AWASHUKURU WANANCHI KWA KUWAPATIA USHINDI CCM UCHAGUZI SERIKALI

MBUNGE wa Wafanyakazi Mkoa wa Pwani Dr Alice Kaijage amewashukuru wananchi wa Halmashauri ya Mji Kibaha kwa kuwachagua wenyeviti wote na wajumbe wa Serikali za Mitaa wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM)


Dk Kaijage ameyasema hayo wakati wa uapisho wa wenyeviti Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Mji Kibaha.

Amesema kuwa wananchi wamefanya jambo zuri kuwachagua viongozi hao kutoka CCM kwani wana uwezo mzuri wa kusimamia miradi ya maendeleo.

"Nawapongeza viongozi wetu wa Serikali za Mitaa kwa ushindi mlioupata nendeni mkafanye kazi kwa kuwatumikia wananchi na kazi zenu mnapozifanya mnapaswa kumtanguliza Mungu,"amesema Dk Kaijage.

No comments:

Post a Comment