Thursday, October 17, 2024

HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAKUSANYA MAPATO ASILIMIA 33 ROBO YA KWANZA


HALMASHAURI ya Mji Kibaha imefanikiwa kukusanya mapato kwa asilimia 33 ya malengo ya ukusanyaji kwenye robo ya kwanza ya makadirio ya makusanyo ya Halmashauri ya shilingi bilioni 8.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Halmashauri Dk Rogers Shemwelekwa  wakati wa kikao cha baraza la Madiwani cha robo ya kwanza ya Julai-Septemba 2024.

Shemwelekwa alisema kuwa kipindi kama hichi mwaka jana walikuwa wamekusanya kwa asilimia 25 hivyo kuvuka lengo kwa asilimia 8 ya makadirio ya shilingi bilioni 7.

"Tunawashukuru madiwani na wataalamu wa Halmashauri kwa kufikia makusanyo hayo ambayo ni mwanzo mzuri na tunategemea kufikia asilimia 100 tunaomba ushirikiano huu uendelee ili kufikia malengo tuliyoweka,"alisema Shemwelekwa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema huo ni mwanzo mzuri wa makusanyo hayo ni mazuri na ushirikiano huo uendelee ili kufikia malengo yaliyowekwa.

John alisema kuwa kwa upande wa uyoaji mikopo asilimia 10 ya Halmashauri dirisha limeshafunguliwa pia zoezi uchongaji barabara kwenye mitaa unaendelea ambapo Halmashauri imetoa milioni 10 kwa kila kata kwa ajili hiyo.

No comments:

Post a Comment