Hayo yalisemwa na Diwani wa Viti Maalum ambaye pia ndiye mwasisi wa mpango huo Josephine Gunda wakati wakukabidhi unga huo kwa viongozi wa Kata ili wasambaze kwenye shule husika.
Gunda alisema unga huo umetolewa na wadau mbalimbali kupitia mradio huo ambapo utasambazwa kwenye Shule ya Sekondari moja na Shule za Msingi tatu.
"Malengo ya kutoa chakula shuleni ni ili kupunguza utoro kwa baadhi ya wanafunzi kwani wanakumbana na changamoto ya chakula na kusababisha kutohudhuria masomo kutokana na hali ya kiuchumi,"alisema Gunda.
Alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakila mmlo mmoja ambapo mtoto anaenda shule bila ya kula chochote hadi jioni anaporudi kutoka shule hali ambayo inawafanya washindwe kuhudhuria masomo na kuwa watoro.
"Shuleni kukiwa na chakula hata kama nyumbani kuna changamoto mtoto atakula shuleni na atavutiwa kwenda shule na mafanikio tumeyaona kwani utoro ymepungua na ufaulu umeongezeka kwani mwanafunzi akila na akili inakuwa na uwezo mzuri,"alisema Gunda.
Aliongeza kuwa ifike wakati suala la chakula shuleni iwe ajenda ya kudumu na Halmashauri itenge sehemu ya fedha ya mapato ya ndani kwa ajili ya kununua chakula kwani hilo ni tatizo kubwa kwa watoto mashuleni.
Diwani wa Kata ya Kwala Mansuri Kisebengo alisema kuwa mbali ya changamoto lakini wazazi bado wana nafasi ya kuhakikisha lishe ya watoto wao inapatikana.
Kisebengo alisema kuwa anawapongeza wadau hao ambao wamejitolea unga huo kwani watawapunguzia wazazi gharama za chakula kwa watoto wao ambao ni wanafunzi.
Kwa upande wake mratibu huduma za lishe Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Coletha Chapile alisema kuwa lishe ni kitu muhimu sana kwa wanafunzi kwani endapo mtoto hatapata chakula uwezo wake wa kuelewa utapungua.
Chapile alisema kuwa suala la lishe kwa wanafunzi ni muhimu na ni jambo ambalo wazazi, walezi na wadau kulipa kipaumbe kwa kuhakikisha watoto wanapata chakula wakiwa shuleni ili kuongeza uelewa.
No comments:
Post a Comment