Sunday, October 13, 2024

BASHUNGWA ARDHISHWA UJENZI SEKONDARI MPYA YA MSANGANI


WAZIRI wa Ujenzi Innocent Bashungwa ametaka kukamilishwa kwa ujenziwa Shule mpya ya Sekondari iliyopo mtaa wa Msangani Kata ya Masangani Wilayani Kibaha Mkoani Pwani yenye thamani ya shilingi milioni 528 iliyojengwa kwa fedha zitokanazo na mradi wa Seqip.

Bashungwa ameyasema hayo alipoweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo ambayo iko kwenye hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na upauaji wa baadhi ya majengo mengine yakiwa kwenye hatua ya linta.

Amesema wajenzi hao wahakikishe ujenzi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa ambapo ni Novemba mwaka huu ili Januari mwakani wanafunzi waanze kusoma ili kuwapunguzia umbali wanaotembea kutoka nyumbani na kwenda shule.

Amebainisha kuwa huo ni mwéndelezo wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan wa kuwekeza kwenye sekta ya elimu ambapo hakuna kijiji wala kata ambayo haijajengwa shule na hilo ni jambo la kupongezwa
na anaonyesha jinsi gani anavyothamini na kulipa  umuhimu suala la elimu kwa watoto.

"Wakala wa Barabaraba Nchini (TANROADS) Mkoa wa Pwani hakikisheni manaandika barua wizarani
mkandarasi alipwe ili arudi kazini kukamilisha ujenziwa kipande cha lami kuja Msangani kilichobaki kinakamilka na barabaraba za Tarura nazo mziangalie kupitia mfuko wa barabara ili kuwaondole a kero wananchi,"a lisema Bashungwa.

Aidha amesema kuwa kuhusu barabara ya njia nane wako kwenye mchakato wa kupata wawekezaji ili kuondoa changamoto ya foleni Kibaha ambapo kwa sasa imekuwa kero kubwa kwa wasafiri lengo ni kurahisisha usafiri maeneo yote.

Katika hatua nyingine amesemna kuwa ataongea na Waziri wa Maji ili kufanikisha kujengwa kisima
kwenye shule hiyo ambayo bado haina miundombinu ya maji ili kukabiliana na changamoto ya jami kwani hata maji ya ujenzi yanatolewa mbali.

Kwa upande vwake mkuu wa mkoa wa Pwani
Abubakari Kunenge amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya utawala wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan jumla ya Shule 10 za Sekondari na Shule 10 za Msingi zimejengwa Wilayani Kibaha.

Kunenge amesema kuwa anamshukuru Rais kwa kuupatia mkoa huo fedha za maendeleo kiasi cha
shilingi trilioni 1.3 kwa ajili ya miradi mbalimbali
ya maendeleo hali ambayo inafanya mkoa huo kupiga hatua kubwa ya maendeleo kwa kipindi hichi cha awamu ya sita.

Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Lilian Marandu amesema kuwa mradi huo ulitambulishwa mwezi
mmoja uliopita na unatarajiwa kukamilika Novemba ukiwa na awamu saba za ujenzi ambapo kwa sasa umefikia hatua mbalimbali zikiwemo kupaua, lita na msingi.

Marandu amesema kuwa mradi huo una majengo yakiwemo ya utawala, maabara za masomo ya
5 sayansi, madarasa manne, vyoo matundu 12 kichomea taka na mnara wa tanki la maji na ofisi mbili za walimu ambazo wanategemea kukamilika ndani ya muda uliopangwa.

No comments:

Post a Comment