SERIKALI imetoa taadhari kwa wananchi waliopo katika wilaya za Rufiji na Kibiti unakopita Mto Rufiji kuondoka ili kuepuka athari za mafuriko baada ya milango ya mradi wa uzalishaji wa umeme wa bwana la Mwalimu Nyerere kufunguliwa.
Friday, March 15, 2024
WATAKIWA KUONDOKA KUEPUKA MAFURIKO MTO RUFIJI
Thursday, March 14, 2024
KATA YA TANGINI YAPATA MILIONI 120 KWA AJILI YA ZAHANATI
KATA ya Tangini Wilayani Kibaha imepata kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ambapo itakapokamilika itahudumia watu 20,146.
ZINGATIENI MTINDO BORA WA MAISHA ILI KULINDA FIGO ZENU
Wakati Tanzania inaungana na mataifa mengine ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Figo Duniani leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Dkt. Alphonce Chandika, amewashauri wananchi kuzingatia mtindo bora wa maisha ili kulinda figo zao.
Dkt. Chandika, ametoa wito huo jijini Dodoma, akisema wananchi wanapaswa wafanye mazoezi kuzingatia mlo usioathiri moyo ili kuzilinda figo.
"Mtindo bora wa maisha unaozingatia milo isiyoathiri moyo utaisaidia kuzilinda figo," amesema Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali.
Siku ya Figo Duniani mwaka huu inaadhimishwa ikiwa na kauli mbiu, 'Afya ya Figo kwa Wote pamoja na Upatikanaji Bora wa Matibabu.'
Dkt Chandika amesema wagonjwa 50 wenye tatizo la figo husafisha damu kwa siku katika Kitengo cha Kusafisha Damu katika Idara ya Magonjwa ya Figo katika BMH.
"Watu wenye tatizo la figo wanasafisha damu mara tatu (3) kwa wiki," ameongeza.
Dkt Chandika amesema mpaka sasa, BMH imeishafanya oparesheni za upandikizaji figo kwa watu 36 toka huduma hii ianze miaka sita (6) iliyopita.
Mwaka 2019, BMH ilikuwa Hospitali ya pili nchini kuanzisha huduma ya upandikizaji figo, lakini ndiyo Hospitali pekee kutoa huduma hiyo bila usaidizi wa Hospitali za nje.
CCWT YATANGAZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI
Na Wellu Mtaki, Dodoma.
Chama Cha Wafugaji Tanzania (CCWT) kimetangaza muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi kwa wanachama wake wanaotaka kugombea huku wakibainisha kuwa malipo ya uchukuaji wa fomu hizo yanapaswa kufanyika kupitia akaunti ya tume ya uchaguzi na sio kwenye akaunti ya chama hicho.
Hayo yameelezwa leo Machi 12, 2024 Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya CCWT Bw. Charles Lyuba alipokutana na waandishi wa habari katika ofisi ya chama hicho ambapo amesema kuwa lisiti za malipo zinapaswa kuambatanishwa katika fomu wakati wa kuzirejesha.
“Tangu mwaka jana tumeanza mchakato wa uchaguzi na hadi sasa tunaendelea na chaguzi za ngazi mbalimbali ikiwemo za wilaya, nawatangazia wafugaji na wanachama wote kuwa fomu za kugombea uongozi ndani ya chama chetu ngazi ya kanda na taifa zitaanza kutolewa Machi 13 - 25,2024 na mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea nafasi yeyote ya kanda anapaswa kuzingatia ratiba na kalenda nzima inayotolewa na tume,”amesema.
Amesema wanachama wao ni muhimu kuwa na taarifa sahihi zinazohusu uchaguzi ili kuepuka mikanganyiko na hasa wanapotoa ratiba isije kuonekana kuna watu wana ratiba zao binafsi.
“Hii ndio ratiba ya tume ya uchaguzi na sisi tunasema hiyo tarehe 13 kwa yaani kesho hadi tarehe hadi tarehe 25, Machi tunaanza kutoa hizo fomu za kanda sambamba na fomu za ngazi ya taifa,” amesema.
Aidha Bw. Lyuba amewasisitiza wagombea wote kufuata ratiba ya tume ipasavyo na kuchukua fomu kwa wakati kwa ngazi ya taifa uchaguzi utaanza Aprili 8,2024 utakao wahusisha viongozi wote wa wilaya na walaya ambayo haitakuwa imefanya uchaguzi wa ngazi haitaruhusiwa kufanya uchaguzi wa ngazi ya kanda pamoja na taifa kwasababu watakuwa hawajatimiza takwa la katiba ya wanachama hicho.
Kwa upande wake mjumbe wa tume ya uchaguzi George Kifuliko amewasisitiza wagombea na wanachama wote kuzingatia ratiba ili kuepusha vikwazo vitakavyojitokeza.
Wednesday, March 13, 2024
MADALALI WA KUPIGIA DEBE WAGOMBEA WATAKIWA KUACHA MARA MOJA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Wilayani Kibaha imewataka watu wanaojifanya madalali wa watu wanaotaka kugombea nafasi za uenyekiti wa serikali za mitaa waache kwani muda wa viongozi walio madarakani haujaisha.
Tuesday, March 12, 2024
WAFANYABIASHARA WA DODOMA WAIOMBA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BIASHARA
Na Anna Misungwi, Dodoma
EWURA KUMTUA MWANAMKE KUNI KICHWANI
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Dkt. James Andilile,amesema mamlaka hiyo ina wajibu kuhakikisha wanamtua mwanamke kuni na mkaa kichwani kwa kuhakikisha wanatoa leseni kwa wakati kwa wawekezaji wanaokuja nchini kuwekeza katika nishati safi ya kupikia.
Dkt. Andilile ameyasema hayo Machi 9,2024 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo kwenye Kongamano la wanawake la kugawa mitaji na vitendea kazi vya nishati safi ya kupikia.
Amesema taifa bado linatumia nishati isiyosafi kwa kupikia hivyo EWURA itahakikisha ina wajibu wa kuhakikisha inatekeleza mikataba ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza ikiwemo uharibifu wa mazingira na madhara ya afya yanayosababidhwa na moshi wakati wa matumizi ya kuni na mkaa.
“EWURA tutahakikiha tunahamasisha uwekezaji katika nishati safi kwa kutoa leseni kwa wawekezaji kwa wakati ili wawekeze katika eneo hilo, pia tunaangalia upatikanaji wake katika maeneo mengi kwa kuangalia mwenendo wa bei za bidhaa hiyo,” amesema Dkt. Andilile.
Ameongeza kuwa:”Sisi kama EWURA tutahakikisha kama ilivyo dhamira ya Rais kumtua ndoo mama kichwani, tutamtua mwanamke kuni kichwani kwa kuhakikisha anatumia nishati ambayo itamrahisishia kupata maendeleo badala ya kuhangaika na nishati chafu ya kupikia,”.