Sunday, August 6, 2023

UMWELANI MABINGWA MICHO CUP

TIMU ya soka ya Umwelani imetwaa ubingwa wa Micho Cup baada ya kuifunga timu ya Wapolo kwa penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana 1-1 hadi dakika 90 zinamalizika.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.

Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.

Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.

Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.

Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili. 

UMWELANI WATWAA KOMBE MICHO CUP

TIMU ya soka ya Umwelani imetwaa ubingwa wa Micho Cup baada ya kuifunga timu ya Wapolo kwa penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana 1-1 hadi dakika 90 zinamalizika.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.

Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.

Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.

Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.

Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili. 

Saturday, August 5, 2023

WAKULIMA WATAKIWA KULIMA KILIMO CHA KIBIASHARA NA SIYO CHA KUJIKIMU

 

SEARIKALI imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha biashara ambapo mabadiliko hayo yanafanyika kwa kuzingatia malengo ya kitaifa kama yalivyoainishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo 2025 na kuhakikisha kilimo ichangie ipasavyo Katika vita dhidi ya umasikini na kulenga kukuza sekta hiyo kufikia asilimia 10 ifikapo Mwaka 2030.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo  Mhe. Balozi Pindi Chana katika ufunguzi wa kongamano la zao la Mtama Jijini Dodoma kwenye maonesho ya nanenane.

Chana amesema kuwa mipango hiyo yote ya kitaifa imeweka mkazo kwenye mapinduzi ya viwanda na kubainisha sekta ya Kilimo kama mhimili imara utakaowezesha upatikanaji wa maligrafi za viwanda.

Amesema kuwa Mikoa ya kanda ya kati kama iliyo kwa Nchi na Dunia nzima inakabiliwa na mabadiliko ya tabia Nchi ambapo Mkoa wa Dodoma na Singida imeamua kwa dhati kuendeleza zao la Mtama ambalo limekuwa likistawi vizuri kwa hali ya hewa ya Mikoa hiyo.

Kanda ya kati imeamua kufanya uhamasishaji kupitia kongamano Hilo kuhusu matumizi ya teknolojia Bora Katika uzalishaji wa Zao la Mtama lengo likiwa ni kuunga mkono na kutekeleza kwa vitendo jitihada za Dkt. Mhe. Samia Suluhu Hassan Katika kuongeza Kasi ya ukuaji wa sekta ya Kilimo kutokana na kuhakikisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi.

Thursday, August 3, 2023

WANNE WAFA AJALINI PWANI

MKURUGENZI wa benki ya APSA Nechi Msuya (45- 50) mkazi wa Dar es Salaam na watu wengine watatu wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuligonga gari lingine uso kwa uso.

Akizungumza na waandishi wa habari wa ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alisema watu hao walifariki papo hapo.

Lutumo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Agosti 3 mwaka huu majira ya saa 2.30 kijiji cha Mapatano Kata ya Mbwewe wilaya ya kipolisi chalinze.

Alisema kuwa marehemu alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Prado lenye namba za usajili T 104 CBU likitoka Dar es Salaam kwenda Same mkoani Kilimanjaro.

"Gari lake liligongana na lori lenye namba T 881 DWU na tela namba T 888 DWU aina ya Scania likitoka Arusha kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Philipo Mtisi (43) mkazi wa Mafinga,"alisema Lutumo.

Aliwataja watu wengine waliokufa kuwa ni Dayana Mgeta (40-45) mfanyabiashara, Nora Msuya (40-45) mwalimu wa chuo kikuu cha Mzumbe tawi la Dar es Salaam na abiria wa kike ambaye jina lake bado halijafahamika (30-35).

Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa Prado kuhama upande wake wa kushoto wa barabara kwenda upande wa kulia kisha kugongana uso kwa uso na lori hilo.

Aidha alisema kuwa miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye zahanati ya Lugoba kwa uchunguzi na kusubiri ndugu kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi.

"Tunawashauri watumiaji wa barabara wakiwemo wale wanaotumia vyombo vya moto kuwa makini ili kupunguza ajali ambazo zinazuilika,"alisema Lutumo.

Monday, July 31, 2023

MAKONGAMANO YA NANE NANE KUWA NA TIJA


Na Manase Madelemu, Dodoma 

MKUU wa mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamle amesema kuwa tofauti na maonesha ya miaka iliyopita ya nane nane mwaka huu 2023 yatahusisha matukio muhimu na makongamano yanayoongeza wigo wa uzalishaji bora.

Senyamule amesema hayo leo julai 31,2023 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya nane nane mwaka kikanda.

Amesema kutakuwa na makongamano ya tasnia ya alizeti,kongamano la zao la mtama ambapo mikoa ya Dodoma na singida ilikabidhiwa jukumu la kuzalisha alizeti Kwa wingi ili kupunguza nakisi ya mafuta ya kula nchini na hivyo kuokoa fedha za kigeni.

Aidha ameongeza kuwa kutakuwepo na siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji hasa katika mkoa wa Singida unafahamika katika mikoa mbalimbali hapa nchini hadi kufikia watu kuwaita kuku wa Singida 

Pia Senyamule amesema kuwa Katika maonesho ya mwaka huu kutakuwa na huduma za Afya na matibabu ya kibingwa zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na huduma hizi zitatolewa bure.

Kauli mbiu ya maonesha na sherehe za nane nane kitaifa Kwa mwaka 2023 ni Vijana na wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula"na kauli mbiu kikanda Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.

Saturday, July 29, 2023

PINDA KUZINDUA MAONYESHO NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Friday, July 28, 2023

WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA MGENI RASMI NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.