Tuesday, July 11, 2023
MAOFISA UTUMISHI WAONYWA
Monday, July 10, 2023
HALMASHAURI YA MJI YAPONGEZWA KUPITIA TASAF
HALMASHAURI ya Mji Kibaha imepongezwa kwa kutekeleza kwa vitendo uhawalishaji wa fedha kwa kaya maskini kiasi kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) cha shilingi bilioni 3.1 kwa kaya 2,583.
TASAF YATAKIWA KUANDAA TAARIFA ZINAZOAKISI MAFANIKIO YA TASAF
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete amewataka waratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwenye wilaya nchini kuandaa taarifa zinazoakisi mafanikio au changamoto ya mfuko huo.
MHE.MASANJA AFANYA MKUTANO WA HADHARA SENGEREMA, AGUSA MAKUNDI MAALUM
MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja amekabidhi baiskeli tano zenye thamani ya shilingi milioni tatu kwa wananchi wenye ulemavu wa miguu Wilayani Sengerema na kuahidi kuwalipia bima ya afya, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukutana na makundi maalum katika Jamii Mkoani Mwanza.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika eneo la Stendi ya zamani Mhe. Masanja amesema Serikali ya Awamu Sita inayoongozwa na Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweka mikakati ya kutatua changamoto za makundi maalum yasiyojiweza katika jamii hivyo msaada huo ni utekelezaji wa ilani ya CCM.
Mhe. Masanja amewaelekeza Madiwani na viongozi wengine wa Serikali kuibua wananchi wenye changamoto mbalimbali za ulemavu ili Serikali iwafikie na kuwasaidia.
"Kama kuna wananchi huko hawawezi kutembea wengine mmewaficha ndani, na kama kuna watoto wadogo hawawezi kwenda shule waleteni Serikali itawahudumia" Mhe. Masanja amesisitiza.
Aidha, Mhe. Masanja amewataka wananchi kuhakikisha wanaiunga mkono Serikali na kuipigia kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu unaokuja.
Katika mkutano huo, Mhe. Masanja amesikiliza changamoto za baadhi ya wananchi kuhusu kero ya watumishi wa maliasili kukamata baiskeli na pikipiki za wananchi, kero za maji, kero ya uhaba wa vifaa vya kujifungulia katika vituo vya afya,ardhi, uhaba wa walimu kero za wafanyabiashara ndogondogo.
Mhe. Masanja ameahidi kuziwasilisha kero hizo katika Sekta husika na kufanyia kazi kero zinazohusu Sekta ya Maliasili na Utalii.
UWEKEZAJI BANDARI MANUFAA UCHUMI WA NCHI
Halmashauri kuu ya ccm Taifa ( NEC) imepokea na kujadili kwa kina taarifa ya makubaliano ya Uwekezaji na uendeshaji wa bandari na kuazimia kwamba Uwekezaji na uendeshaji wa bandari hiyo ni kwa manufaa ya uchumi wa Nchi pamoja na utekelezaji wa vitendo vya Ilani ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma katibu wa Halmashauri kuu ya Ccm Itikadi na Uenezi Bi Sofia Mjema amesema halmashauri kuu ya Ccm imekutana Katika kikao Chake Cha kawaida chini ya mwenyekiti wa Ccm na RAIS wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasani.
Mjema amesema kikao hicho kimeazimia kwamba serikali iongeze kasi ya kutoa Elimu kwa wananchi juu ya uhalisia uliomo Katika makubaliano ya Uwekezaji na uendeshaji wa bandari.
Sunday, July 9, 2023
VYAMA VYA SOKA VYATAKIWA KUWA NA UTAWALA BORA
VYAMA vya Soka Nchini vimetakiwa kuzingatia utawala bora ili kuhakikisha sheria miongozo na taratibu za mpira zinafuatwa ili soka liweze kuimarika na kupata timu na wachezaji bora.
Saturday, July 8, 2023
RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN MGENI RASMI MIAKA 60 YA JKT
RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri jeshi mkuu Mhe, Dkt,Samia Suluhu Hasani anatarajiwa kuwa mgeni rasmi Katika maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la kujenga Taifa JKT.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Mhe, Innocent Bashungwa wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
Mhe, Bashungwa amesema kilele Cha maadhimisho ya Miaka 60 ya JKT kinatarajiwa kuadhimishwa rasmi julay 10 2023 Katika viwanja vya Jamuhuri jijini Dodoma ambapo wageni mbalimbali watashiriki kutoka ndani na nje ya Nchi.
Aidha amewaalika viongozi wote wa serikali, taasisi mbalimbali za umma na binafsi,watumishi,wananchi wa mkoa wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kuhudhuria siku ya kilele Cha maadhimisho Hayo.
Hata hivyo Maadhimisho Hayo yanatarajiwa kuanza saa kumi na Mbili Asubuhi ambapo kutakuwa na maonyesho ya vifaa mbalimbali vya SUMA JKT, burudani za ngoma kutoka vikundi vya JKT na wasanii Mbalimbali.