Na Mwandishi Wetu Dodoma
Wednesday, February 15, 2023
TBA YAENDELEA NA MIPANGO YA UJENZI KWA NYUMBA WATUMISHI
WANANCHI WATAKIWA KUKOPA KWA MALENGO
Na Mwandishi Wetu Dodoma
Tuesday, February 14, 2023
MFUKO WA MAWASILIANO KWA WOTE KUPELEKA VIFAA VYA TEHAMA SHULE MAHITAJI MAALUM
Na Mwandishi Wetu Dodoma
MFUKO wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) unatarajia kutumia shilingi milioni 575 kwa ajili ya mradi wa kupeleka vifaa maalum vya TEHAMA vya kujifunzia kwa Shule 16 zenye watoto wenye mahitaji maalum hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Mtendaji mkuu wa mfuko wa mawasiliano kwa wote ( UCSAF) Justina Mashimba leo Februari 13,2023 Jijini Dodoma, wakati akielezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za mfuko huo.
Mashimba amesema kuwa vifaa vitakavyopelekwa katika shule hizo ni pamoja na TV, mashine ya (Nukta Nundu) Orbit reader (Machine za Kisasa), Laptops, (Printa ya nukta nundu).
"Jumla ya shule 811 zimefikishiwa vifaa vya TEHAMA ambapo kwa wastani kila shule imepewa Kompyuta 5, Printa 1 na Projekta 1 kwa mwaka wa fedha wa 2022/23 ambapo Shule 150 zitafikishiwa vifaa vya TEHAMA bajeti yake ikiwa ni shilingi 1.9 na vifaa hivyo vitasaidia wanafunzi kusoma katika shule hizo,"amesema Mashimba
Amezitaka Shule hizo zitakazonufaika ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Mpwapwa (Mpwapwa-Dodoma), Sekondari ya Mkolani (Mwanza), Sekondari ya Kashaulili (Mpanda-Katavi), Sekondari ya Morogoro (Morogoro), Sekondari ya Shinyanga (Kishapu-Shinyanga), Sekondari ya Wavulana Songea (Songea), Sekondari ya Kazima (Tabora) na Sekondari ya Haile Selassie (Mjini Magharibi)
Aidha akizungumzia hali ya mawasiliano nchini amesema kuwa mwaka 2009 Huduma za Simu ilikuwa asilimia 45 wakati kwa sasa imeongezeka hadi kufikia asilimia 96,Teknolojia ya 2G ni asilimia 96,3G ni asilimia 72,4G ni asilimia 55 na Geographical Coverage ya 2G ni asilimia 69; 3G ni asilimia 55 na 4G ni asilimia 36.
Amesema kuwa upande wa ujenzi wa minara Vijiji UCSAF imeingia mikataba kufikisha huduma katika kata 1,242 zenye Vijiji 3,654, Wakazi 15,130,250 ambapo Minara 1,087 yenye Vijiji 3,378 na wakazi 13,320,750 na Utekelezaji unaendelea katika Minara 155 yenye Vijiji 276 na wakazi 1.8 kwa ruzuku iliyotolewa ya shilingi bilioni 199 ikiwemo pia mradi wa kimkakati wa Zanzibar Minara 42, Shehia 38 ruzuku bilioni 6.9
BARAZA LA TAIFA LA UJENZI LATATUA MIGOGORO YA MIRADÍ YA UJENZI
Na Mwandishi Wetu Dodoma
BARAZA la Taifa la ujenzi limeendesha mafunzo ya kusimamia mikataba ya ujenzi na utatuzi wa migogoro katika miradi ya ujenzi kwa wadau 155 kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Hayo yasemwa Mtendaji Mkuu wa baraza la taifa la ujenzi Dkt.Matiko Mturi wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa baraza hilo katika serikali ya awamu ya sita.
Dkt Mturi amesema wameandaa rasimu ya mapendekezo ya gharama za msingi za ujenzi wa barabara kwa kila mkoa wa Tanzania Bara na kuwakilisha katika kikao cha wadau wa ndani ya serikali ili kupata maoni na ushauri wao.
"Baraza limefanikiwa kuratibu ,kuandaa na kuwasilisha Wizara ya ujenzi na uchukuzi(sekta ya ujenzi) andiko dhana lenye mapendekezo ya kuboreshwa kwa mfumo wa sheria zinazosimamia ujenzi wa nyumba na majengo nchini,"amesema Mturi.
Amesema mwelekeo wa taasisi katika kutekeleza majukumu ni pamoja na kufuatilia utekelezaji wa sera ya ujenzi nchini,kuandaa na kutekeleza mpango mkakati wa maendeleo wa sekta ya ujenzi,kutoa miongozo mbalimbali ya kitaalam ya maeneo mbalimbali ya ujenzi.
Aidha amesema Taasisi inaendelea kutoa mafunzo kwa wadau wa ujenzi kuhusu maadili na utekelezaji wa miradi ya ujenzi, sanifu jenga na usimamizi wa mikataba ya ujenzi kwa wadau mbalimbali pamoja na kutoa mafunzo yanayolenga kukuza na kujenga wataalam mahiri katika sekta ya ujenzi.
Monday, February 13, 2023
REDIO ZITANGAZE HABARI ZA VIJIJINI
Na Mwandishi Wetu Dodoma
Friday, February 10, 2023
12 WAFA 63 WAJERUHIWA AJALINI
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.
WATU 12 wamefariki dunia na wengine 63 kujeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea usiku wa kuamkia Alhamisi Februari 9, 2023 Wilayani Kongwa mkoani Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema kuwa ajali hiyo imehusisha magari mawili na kusababisha vifo vya watu 12 (wanaume nane , wanawake wanne) na majeruhi 63 (wanaume 40 wanawake 23).
Senyamule amesema ajali hiyo imetokea usiku Kata ya Pandambili Kijiji cha Silwa wilayani Kongwa, barabara ya Dodoma - Morogoro.
"Majeruhi wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kongwa na Kituo cha Afya Gairo na miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkoa wa Morogoro na majeruhi wawili wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma,"amesema Senyamule.
Amesema ajali hiyo imetokea majira ya saa 6 usiku na imehusisha lori la mizigo lenye namba za usajili T 677 DVX na basi la abiria la Kampuni ya Frester lenye namba za usajili T 415 DPP lililokuwa likitokea Bukoba kwenda Dar es Salaam.
Akizungumza na wakazi wa Pandambili eneo ambapo ajali ilipotokea Senyamule ametoa rai kwa jamii kutii sheria bila shuruti ili kuepuka ajali.
"Serikali ilikuwa na nia njema ya kuruhusu vyombo vya usafiri kutembea usiku, lakini sasa baadhi ya madereva wanaanza kutozingatia Sheria za usalama barabarani, tutaendelea kuwachukulia hatua kali,"amesema Senyamule.a
Pia mewatembelea majeruhi katika Hospitali ya Kongwa na Kituo cha Afya Gairo na kutoa pole na kuwatakia uponyaji wa haraka.
Naye Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Kamishna Awadh Haji ametaja chanzo cha ajali hiyo kuwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva wa basi kutaka kulipita gari la mbele yake bila ya kuchukua tahadhari na kugongana na lori hilo lililokuwa limebeba saruji.
WATUMISHI HOUSING A YAJENGA NYUMBA KWA WATUMISHI
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WATUMISHI Housing Investment (WHI) imeweza kujenga nyumba 983 kwa ajili ya watumishi wa umma katika mikoa mbalimbali nchini.
Aidha kupitia kampuni yake ya ujenzi imeshiriki katika ujenzi wa mji wa serikali Jijini Dodoma pomoja na majengo ya taasisi za serikali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa chuo Cha utumishi wa umma katika mkoa wa Singida.
Hayo yamesemwa na Mkurugezi mtendaji wa WHI Dkt Fred Msemwa wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu mwenendo wa taasisi hiyo ambapo kumekuwa na ongezeko la kushuka kwa bei ya nyumba kutoka asilimia 10 hadi asilimia 30.
Amesema kuwa wanategemea kuwa na miradi mipya ya ujenzi katika mwaka wa fedha 2022/2023 ambayo ni Kawe, Dodoma, Gezaulole, mradi wa viwanda Arusha pamoja na nyumba za watumishi Halmashauri mpya.
"Yapo baadhi ya mafanikio ambayo taasisi imefanikiwa ikiwa ni pamoja na kupata vifaa vya upimaji wa ardhi vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.5 kutoka serikalini kupitia mkopo wa benki ya dunia unaoratibiwa na benki kuu ya Tanzania,"amesema Msemwa.
Watumishi Housing Investment ni taasisi ya umma iliyo chini ya ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (OR-MUUUB) iliyoanzishwa Mwaka 2014 na ilianzishwa na serikali kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii ikiwemo mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma (PSSSF), mfuko wa hifadhi ya jamii ( NSSF) pamoja na shirika la nyumba la Taifa na mfuko wa bima ya Afya (NHIF)