Wednesday, February 8, 2023

MAMLAKA YA USIMAMIZI BAHARI KUU KUJENGA KIWANDA KUCHAKATA SAMAKI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya kusimamia uvuvi wa Bahari Kuu inatarajia Kujenga Kiwanda kikubwa cha kuchakata Samaki Mkoani Tanga ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani zaidi ya 100 kwa siku ambacho kitagharimu Dola Milioni 10 na kutoa fursa ya ajira kwa Watanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo,Dk Emanuel Sweke wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka ya usimamizi wa Bahari Kuu. 

Sweke amesema kuwa katika kudhibiti uvuvi haramu  Mamlaka hiyo imeweza kuweka mifumo madhubuti ambayo inaendana na Teknolojia kwakufanya doria mbalimbali kwa ajili ya kukomesha uvuvi haramu.

"Kutokana na shughuli zake Mamlaka hiyo imeweza kuvunja rekodi ya kukusanya mapato mengi kwa kipindi cha mwaka 2022 hadi kufikia shilingi bilioni 4.1 na wametoa jumla ya leseni za uvuvi 5336,"alisema Sweke.

Mamlaka ya kusimamia uvuvi wa Bahari Kuu imeanzishwa rasmi Mwaka 2010 lengo lake likiwa ni kusimamia shughuli zote za uvuvi wa Bahari Kuu na ufuatiliaji.

WACHIMBA VISIMA VYA MAJI WATAKIWA KUWA NA VIBALI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

BODI ya Maji ya Bonde la Wami-Ruvu imewataka wadau wa maji nchini kuzingatia na kufuata taratibu za uchimbaji wa visima vya maji ikiwemo kupata vibali halali ili kupata maji yenye ubora na kuondokana na malalamiko mengi ya maji yasiyo na viwango.

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu Mhandisi Elibariki Mmasi ameeleza hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa miradi ya maji chini ya bodi hiyo.

Mmasi amesema wadau wa maji wanapaswa kufahamu madhara ya kuchimba visima bila vibali na kupelekea changamoto ya ubora wa maji kwenye maeneo mengi jambo linaloweza kuleta madhara kiafya.

"Baadhi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kutumia maji yasiyo na madhara kuwa ni pamoja na kuhakikisha maji yanayopatikana baada ya kuchimbwa yanapelekwa maabara kuchunguzwa iwapo yanafaa kwa matumizi au la,"amesema Mmasi

Aidha amesema kuwa bodi hiyo imejipanga kuhakikisha inamaliza changamoto ya tatizo la maji katika mikoa ya Dar es salaam,Pwani na Morogoro kwa kuchimba visima vya maji 

HUDUMA MTANDAO KUBORESHWA

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MAMLAKA ya Serikali Mtandao ( EGA ) kuandaa na kutelekeza mikakati madhubuti ili huduma za Mtandao zote kupatikana ili kudhibiti matishio ya usalama mtandaoni na kurahisisha utoaji wa huduma kwa umma.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi mkuu wa mamlaka ya serikali Mhandisi Benedict Benny Ndomba wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu kikao kazi cha tatu cha serikali Mtandao kinachotarajiwa kufanyika Februari 8 hadi 10 mwaka huu katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama ( mb).

Ndomba amesema kuwa takribani wadau 1,000 wa serikali Mtandao kutoka katika mashirika na taasisi za umma wakiwemo maafisa masuuli, wajumbe wa bodi, Wakuu wa vitengo vya tehama, maofisa tehama, rasilimali watu, mipango, mawasiliano, wahasibu pamoja na watumishi wote wa mifumo ya tehama serikali wanatatarajiwa kushiriki kikao hicho.

"Lengo la kikao hicho ni kijadiliana juu ya mafanikio, changamoto pamoja na kuweka mikakati mbalimbali ya kukuza serikali Mtandao nchin Ili kuhakikisha matumizi sahihi na salama ya tehama katika taasisi za umma,"alisema Ndomba.

Aidha alisema kuwa Mamlaka ya serikali Mtandao( (e-GA) ni taasisi iliyopewa jukumu la kuratibu, kusimamia na kukuza juhudi za serikali Mtandao pamoja na kuhimiza uzingatiwaji wa sera, Sheria, kanuni, viwango na miongozo ya serikali Mtandao katika taasisi za umma ili kuhakikisha matumizi sahihi na salama ya tehama yanazingatiwa katika taasisi hizo.

Monday, February 6, 2023

NJOMBE YATEKETEZA ILANI YA CCM KWA VITENDO



NJOMBE YATEKELEZA ILANI YA UCHAGUZI YA (CCM) KWA VITENDO

Na Elizabeth Paulo, Njombe

MKOA wa Njombe umeendelea na utekelezaji wa  Miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka amebainisha Utekelezaji wa miradi hiyo katika taarifa ya utekelezaji wa Ilani kwa Mkoa wa Njombe katika kipindi cha mwaka mmoja Julai 2021 hadi Disemba 2022.

Mtaka amesema Mkoa wa Njombe unaendelea kutekeleza mipango ya maendeleo kwa kuzingatia Ilani ya Chama ambapo na Dira ya Taifa ya maendeleo 2025 na malengo ya maendeleo endelevu ya Milenia yenye lengo la kuendelea kuwatumikia wananchi na kuboresha maisha ya wananchi wote.

"Kama ilani ya chama tawala inavyoelekeza Mkoa umekusudia kusimamia na kuelekeza rasilimali zake katika kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za Afya, Elimu, Maji, Umeme na Makazi vijijini na Mijini pamoja na kuleta mageuzi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi katika kujitegema kwa chakula wakati wote na kuchangia kikamilifu kwa maendeleo ya kiuchumi,"alisema Mtaka.

Amesema serikali ya Mkoa itajikita katika mambo matatu muhimu yatakayogusa maisha ya wananchi ikiwa ni pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kufuatilia wanafunzi ambao bado hawajaripoti mashuleni huku asilimia 90 ya wanafunzi kidato cha kwanza wameripoti katika shule mbalimbali ambapo awali ilikuwa asilimia12.

"Mkoa umeanzisha mkakati wa kuwaondoa wanufaika wa Tasaf baadaya miaka mitatu hadi miaka mitano kwa kuanza na Halmashauri ya Makambako ambapo katika ziara ya Waziri wa Kilimo Bashe alitoa miche ya parachichi 20,000 yenye thamani ya shilingi millioni 100 kwa wanufaika wa Tasaf hao ambapo kila kaya imepewa miche 10,"amesema Mtaka.

Aidha amesema kuwa kutokana na kero kubwa na changamoto inayowakabili wananchi na wakazi wa mkoa huo kutozwa ushuru mara mbili kuingia stendi kuu ametoa wito kwa viongozi na wakusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kutafuta vyanzo vya mapato na kuacha mapato kero kwa wananchi.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe Deo Sanga ameupongeza uongozi wa chama tawala chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha nyingi za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika mkoa wa Njombe. 

Katika kuwainua kiuchumi Halmashauri ya Mkoa imeendelea kutoa mikopo kwa Vikundi vya akina mama, Vijana na watu wenye ulemavu ambapo jumla ya shilingi bilioni 10.6 zimekopeshwa ambapo vikundi vya wanawake ni 382 vyenye wanufaika 4,062, Vijana vikundi 237 vyenye wanufaika 1,564 pamoja na watu wenye ulemavu kwa vikundi 72 vyenye wanufaika 207.

Maadhimisho ya Miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama cha mapinduzi kwa Mkoa wa Njombe imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama, akiwemo Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Pindi Chana, Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi anayeshughulikia Elimu na Afya Dkt Festo John Dugange, Wabunge, wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya, pamoja na wananchi wa Mkoa huo.


Saturday, February 4, 2023

RAIS DK SAMIA APONGEZWA MIRADI YA MAENDELEO



RAIS APONGEZWA KUHAMASISHA MAENDELEO KUINUA UCHUMI.                

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM NEC) Taifa Hamoud Jumaa amempongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhamasisha maendeleo na kukuza uchumi wa nchi.

Jumaa aliaysema hayo alipowaongoza wana CCM na wananchi kuadhimisha miaka 46 ya CCM Kibaha Vijijini na kuwa Tanzania ilipofikia kwa kipindi hicho kuna mengi ya kujivunia.

Alisema kuwa wumuunge mkono Rais na kuacha maneno kwani sekta zote zikiwemo afya, elimu kujengwa, vikundi vya ujasiliamali na machinga wanawezeshwa mikopo na miradi mikubwa ya kimkakati haijasimama ikiwa ni pamoja na reli ya mwendo Kasi SGR, Bandari kavu ya Kwala, Daraja la kisasa la Wami.

Jumaa aliwataka wana CCM kuwa wamoja kuimarisha ushirikiano ili kuiletea ushindi CCM uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 pia aliweka jiwe la msingi ujenzi wa ofisi ya kata Mtongani ambao ulianza tangu mwaka 2017 kwa njia ya kujitolea ambapo amechangia 500,000 na rafiki yake 500,000 kwa ajili ya ujenzi huo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu alieleza kuwa Rais Samia apewe ushirikiano na kuyaeleza yale aliyoyatekeleza nchini na alisisitiza kwa wana CCM kuwa na umoja na mshikamano na pasipo kutengana ili chama kiweze kusonga mbele.

Katibu wa CCM Kibaha Vijijini Safina Nchimbi alieleza kuwa maadhimisho hayo yameambatana na tukio la kuchangia damu kupanda miti kufanya usafi kituo cha afya Mlandizi na zahanati

Kwa upande wake Katibu wa CCM Mtongani Gloria Kirei alisema ujenzi huo mbali ya wanaCCM kujitolea pia wabunge viti maalum Hawa Mchafu ,Subira Mgalu, wilaya na Mwenyekiti wa UWT mkoa Zainabu Vullu nao walichangia vifaa mbalimbali.


Friday, February 3, 2023

MIAKA 46 CCM JUMUIYA YA WAZAZI BAGAMOYO YAPANDA MITI SHULENI

WAKAZI wa Chalinze wilayani Bagamoyo wametakiwa kupanda miti ili kutunza mazingira kuzuia upepo wa mara kwa mara unaoezua mapaa katika majengo yao.

Akizungumza wakati wa zoezi la upandaji wa miti katika shule ya msingi Bwilingu Kata ya Bwilingu Chalinze Mwenyekiti wa Wazazi wilaya ya Bagamoyo Aboubakary Mlawa alisema kuwa wananchi wanapaswa kuwa na utamaduni wa kupanda miti mara kwa mara na si kusubiri wakati wa sherehe ama ugeni.

Mlawa alisema kuwa kwa eneo la chalinze eneo kubwa lipo wazi kwa kutokuwa na miti kutoka na ujenzi hivyo ni muhimu sasa kila mkazi awe na utamaduni wa kupanda miti.

"Kumekuwa na matukio mengi ya upepo kuezua mapaa katika majengo ya watu binafsi sambamba na majengo ya taasisi zikiwemo shule dawa pekee kuzuia hali hii ni kupanda miti kwa wingi,"alisema Mlawa.

Alisema kuwa kama kila mtu akipanda mti mmoja katika maeneo yanayomzunguka ana hakika mazingira ya majengo yao yatakuwa na usalama.

"Wao kama Jumuiya ya Wazazi jukumu mojawapo walilopewa na Chma cha Mapinduzi ambalo pia katika dhumuni la kuwepo kwa jumuiya hiyo ni utunzaji wa nazingira hivyo ni muhimu kusimamia na kuhakikisha upandaji wa miti unakuwa endelevu,"alisema Mlawa.

Aidha alisema anaomba upandaji wa miti usiwe wakati wa ujio wa wageni ama wakati wa sherehe,zoezi la upandaji miti liwe la kila siku.

Awali Diwani wa kata ya Bwilingu Nasser Karama alisema kama Diwani alihakikisha kuwa maeneo mbalimbali ya Taasisi yanapata huduma ya maji kwa kuchimba visima vya kisasa. 

Karama alisema kuwepo kwa visima hivyo kutachochea utunzaji wa miti hiyo na uboreshaji wa mazingira.

Jumuiya wa Wazazi wilaya ya Bagamoyo katika kusherekea miaka 46 ya kuzaliwa kwake ilifanya shughuli mbalimbali ikiwemo utoaji misaada mbalimbali, upandaji miti na uchangiaji wa damu. 


MTAA WA BAMBA KUJENGA SEKONDARI

MTAA wa Bamba Kata ya Kongowe Wilayani Kibaha imesafisha eneo kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari kwa wanafunzi wanaotoka Mtaa huo ambapo hutembea umbali wa kilometa 16 kwenda Shule ya Sekondari Mwambisi.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi huo Mwenyekiti wa Mtaa huo Majid Kavuta amesema kuwa tayari wana vifaa kwa ajili ya kuanza ujenzi huo kwa awali madarasa manne.

Kavuta ametaja vifaa hivyo kuwa ni tofali 3,600, saruji mifuko 50, mchanga lori tatu, kokoto lori mbili na wanatafuta mdau ili awapatie nondo ambapo kila kaya inatakiwa kutoa tofali 10.

"Kutokana na wanafunzi hao kusoma mbali kunasababisha utoro na wanafunzi wa kike kurubuniwa na kujiingiza kwenye mapenzi na wale wa kiume kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya na uvutaji wa bhangi,"amesema Kavuta.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kongowe Simon Mbelea amesema ujenzi huo ni kutekeleza ilani ya chama kuhakikisha watoto wanapata elimu kwenye mazingira rafiki.

Mbelwa amesema pia ni kuunga mkono jitihada za Rais DK Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya elimu ambapo ametoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu nchini.