Saturday, July 2, 2016
johngagariniblog: WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI
johngagariniblog: WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI: Na John Gagarini, Kibaha MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakuu wapya wa wilaya wlioteuliwa na Rais Dk John...
Friday, July 1, 2016
WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI
Na John
Gagarini, Kibaha
MKUU wa Mkoa
wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakuu wapya wa wilaya wlioteuliwa na
Rais Dk John Magufuli mkoani humo kuinua pato la wananchi wa mkoa huo kutoka
milioni 1.2 kwa mwaka hadi milioni 3 kwa mwaka.
Aliyasema hayo
jana mjini Kibaha wakati akiwaapisha wakuu hao wa wilaya wapya na kusema kuwa
pato la mwananchi wa mkoa wa Pwani liko chini sana licha ya kuwa na fursa
mbalimbali za kipato.
Ndikilo alisema
kuwa kutoakana na pato hilo la wananchi kuwa dogo kiasi hicho hata mchango wa
mkoa kwa Pato la Taifa ni dogo sana la asilimia 1.8 jambo ambalo linapaswa
kuwekewa mkakati wa kupandisha pato hilo ili liwe na mchango mkubwa kwa
mwananchi na Taifa kwa ujumla.
“Nawapongezeni
kwa kuchaguliwa kwenye nafasi hizi na mkoa tayari umeandaa mpango kazi wake kwa
ajili ya kuinua pato la mwananchi hivyo mnapaswa kuweka vipaumbele ambavyo
vitasaidia kuinua uchumi wa wananchi wa wilaya unayoongoza,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa
hakuna sababu ya mkoa kuendelea kuwa na pato dogo huku kukiwa na vyanzo vingi
vya mapato ikiwa ni pamoja na rasilimali mbalimbali kama vile uvuvi, kilimo,
korosho, maliasili ikiwa ni pamoja na mbuga za wanyama na madini mbalimbali.
“Mfano ni
majumba mengi yanayojengwa Dar es Salaam kokoto na mawe yanatoka mkoa wa Pwani
hivyo hakuna sababu ya kuwa maskini tuna zao la korosho ambapo kwa msimu
uliopita wakulima waliuza korosho zenye tahamani ya shilingi bilioni 18,”
alisema Ndikilo.
Aliwataka wahakikisha
wanawajibika na kutowalea watumishi ambao ni kikwazo na wenye urasimu wa
kuwahudumia wananchi ambao hufika ngazi ya mkoa kulalamika ili hali ngazi za
chini kuna watendaji ambao wangeweza kutatua matatizo hayo.
“Changamoto
ni nyingi ikiwa ni pamoja na suala la ulinzi na usalama, wahamiaji haramu,
matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi nisingependa mambo haya yatokee tena
hakikisheni mnatimiza wajibu wenu na kuwaondolea kero wananchi,” alisema
Ndikilo.
Kwa upande
wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid
Mwanga alisema kuwa moja ya changamoto ambazo atakabiliana nazo ni pamoja
na wahamiaji haramu kw akudhibiti bandari 19 ambazo zimekuwa ni njia ya
wahamiaji hao haramu.
Naye Asumpter
Mshama alisema kuwa moja ya mambo atayapaa kipaumbele ni kuhakikisha fedha kwa
makundi ya vijana na akinamama asilimia 10 zinatoka ili wananchi waweze kujenga
uchumi wao na ule wa Taifa.
Wakuu wapya
walioapishwa jana ni pamoja na Shaibu Nunduma wilaya ya Mafia, Filberto Sanga
Mkuranga, Gulamu Kifu wilaya ya Kibiti, Asumpter Mshama wilaya ya Kibaha, Juma
Njwayo wilaya ya Rufiji na Majid Mwanga wilaya ya Bagamoyo huku Happyness
William hakuweza kuapishwa kutokana na dharura.
Mwisho.
Mkuu mpya wa wilaya Rufiji Juma
Njwayo kulia akiapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo
wakati wakiapishwa wakuu wa wilaya za mkoa huo kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu
wa mkoa huo.
|
Saturday, June 25, 2016
WAKANUSHA KUPAKA KINYESI NA KUVUNJA OFISI YA KATA
Na John
Gagarini, Kibaha
WAKAZI wa
Mtaa wa Machinjioni Loliondoa au Sagulasagula waliobomolewa nyumba zao na
Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani kwa tuhuma za kujenga nyumba kwenye
eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko wamekanusha kuapaka kinyesi na kuvunja
vioo vya ofisi ya kata ya Maili Moja.
Akizungumza na
waandishi wa habari moja ya wahanga wa tukio la bomoa bomoa hiyo iliyofanyika
Juni 16 na 17 mwaka huu ambapo watu hao walifanya uharibifu huu siku moja baada
ya bomobomoa hiyo huku jumla ya nyumba 18 zilibomolewa, Said Tekelo amesema
kuwa wao hawahusiki na tukio hilo na wamesikitishwa na kitendo hicho.
Tekelo amesema
kuwa kitendo hicho kimefanywa na watu ambao walikuwa na malengo yao na hawaungi
mkono watu waliofanya uharibifu huo kwani ni tukio ambalo ni kinyume cha sheria
na hakistahili kuunga mkono.
Amesema kuwa
wao kama wahanga wa bomobomoa hiyo hawawezi kufanya hivyo kwa sababu bado wako
katika kutafuta haki yao waliyoipoteza baada ya nyumba zao kubomolewa pasipo
kupewa fidia yoyote hivyo wasingeweza kufanya uharibifu.
Aidha amesema
kuwa vi vema vyombo vya kisheria vikafanya yake ili kubaini wale waliofanya
hivyo na kuwachukulia hatua kazi za kisheria kwani hao ni wahalifu kama
wahalifu wengine na hawahusiani na waliobomolewa nyumba zao.
Amebainisha kuwa
suala lao liko mahakamani tangu zoezi la kubomolewa nyumba zao lilipofanyika na
hawaungi mkono watu waliofanya hivyo na wanawalaani vikali watu hao ambao
wamejificha kwenye mwamvuli wa uhalifu.
MWISHO
ZEGERENI KUJENGA SHULE YA MSINGI
Na John Gagarini, Kibaha
MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha umefayatua matufali 2,500 kwa ajili ya
kuanza ujenzi wa shule ya Msingi katika mtaa huo ambao unategemea mtaa wa
Visiga kuwapeleka watoto wao umbali wa kilometa nane.
Akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa zoezi la kuwapa zawadi wanafunzi wa
darasa la saba ambao wamefanya vizuri na kuwa kwenye 10 bora mwenyekiti wa mtaa
huo Rashid Likunja amesema kuwa wanatarajia kuanza ujenzi wa shule hiyo kuanzia
Julai Mwaka huu ili ifikapo mwakani watoto wao waanze kusoma kwenye shule hiyo.
Likunja amesema
kuwa fedha za kununulia kiwanja chenye ukubwa wa hekari sita zimetokana na
mchango wa shilingi 5,000 kila kaya ambapo hatua ya ujenzi itaanza kwa kutumia
tofaali hizo huku wakiwa na mifuko 12 ya simenti wakianza na madarasa mawili,
ofisi na matundu manne ya vyoo.
Amesema kuwa
kwa sasa wako kwenye harakati za kupata kibali cha ujenzi pamoja na ramani toka
Halmashauri ya Mji ili waweze kuanza ujenzi huo na utawapunguzia watoto wao
kwenda kusoma mbali pia huwabidi kuvuka barabara ya Morogoro ambapo ni hatari
kwao kwani wengine ni wadogo sana.
Aidha amewataka
wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili waweze kutekeleza azma yao ya ujenzi
wa shule hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa watoto wanaotoka mtaa huo ambao
wanafikia zaidi ya 200 wanaosoma madarasa mbalimbali kutoka mtaa huo ambao
wanasoma shule jirani ya Visiga.
Mwisho.
Thursday, June 23, 2016
MILIKINI MAENEO KIHALALI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI-RC
Na John
Gagarini, Kibaha
MKUU wa
mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakazi wa mkoa huo kufuta
taratibu na sheria za kumiliki ardhi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo
kwa sasa imeshamiri na inaweza kuhatarisha amani.
Aidha amesema
kuwa mkoa hautasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu ambao wanavamia
maeneo ya watu na kuyauza kama wanavyofanya baadhi ya watu kwani ni kinyume cha
sheria na watachukuliwa hatua kali ili waachane na tabia hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa
na baadhi wananchi kutoka wilaya ya Mkuranga Ndikilo alisema kuwa kumekuwa na
migogoro mingi ambayo imesababisha wananchi kutokuelewana wao kwa wao.
“Moja
ya mfano ni Kijiji cha Kazole Kitongoji cha Magodani Kata ya Vikindu wilaya ya
Mkuranga kuna baadhi ya watu wanajifanya kamati ya ardhi ya Kijiji hicho
kulivamia shamba la kampuni ya Soap Allied Industry ambalo lina ukubwa wa
hekari 1,750 likiwa na hati ya umiliki 271 ambayo iliipata tangu mwaka 1988
ambalo lilitengwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,”alisema Ndikilo.
Ndikilo
alisema kuwa kamati hiyo ambayo imekuwa ikiuza viwanja kwenye eneo hilo inafanya
makosa kwa kuwauzia watu kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria kwani eneo
hilo lina mmiliki halali ambaye anamiliki kisheria.
“Kama
haitoshi watu hao walikwenda kwenye vyombo vya sheria lakini walishindwa na
kuambiwa kuwa eneo hilo ni mali ya mtu hivyo hawapaswi kuingie kwenye eneo hilo
lakini wanakamati hao bado wanaendelea kuwauzia watu na kujipatia mamilioni
ambayo yote yanaingia mifukoni mwao na wamejinufaisha kupitia shamba hilo
lakini wanawaibia watu kwani mmiliki mwenyewe yupo,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema
kuwa suala la shamba hilo linachukuliwa kisiasa lakini mwisho wa siku linaweza kusababisha
uvunjifu wa amani kwani watu waliotoa fedha zao watakapoambiwa waondoke watadai
fedha zao na hakuna mtu wa kuwarejeshea hivyo kuleta migogoro ambayo haitakiwi.
Kwa upande
wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa ni vema
watu wakafuata sheria bila ya shuruti kwani eneo hilo limeshatolewa maamuzi
baada ya watu waliouziwa kwenda mahakamani na kuonekana kuwa kampuni hiyo ndiyo
yenye uhalali wa kumiliki eneo hilo hivyo watu kuingia humo ni kuvunja sheria
na wanaweza kukamatwa na polisi
Mushongi
alisema kuwa watu hawapaswi kuingia kwenye eneo hilo ambapo hivi karibuni zaidi
ya watu 20 waliingia kwenye shamba na kukamatwa na kwa kuwa hati ya umiliki
bado haijatenguliwa watu wasiingie na kama wanaona wana haki ni vema wakaenda
mahakama za juu kudai haki yao lakini si kulivamia.
Mwisho.
KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI
Na John
Gagarini, Kibaha
WAKAZI 200
wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani
Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa
maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO)
wilaya ya Kibaha kukamilika.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto
Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na
uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya
kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.
Emanuel
alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo
hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya
kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa
wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.
“Maji
haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya
miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa
mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.
Awali wananchi
hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro
kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila
ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.
Wakizungumza
na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin,
Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika
kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya
mkopo toka Dawasco.
Walisema
kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba
kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani
ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna
kinachoendelea hadi sasa.
“Kinachotushangaza
ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji
huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji
uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa
kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.
Mwisho
KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI
Na John
Gagarini, Kibaha
WAKAZI 200
wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani
Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa
maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO)
wilaya ya Kibaha kukamilika.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto
Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na
uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya
kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.
Emanuel
alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo
hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya
kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa
wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.
“Maji
haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya
miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa
mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.
Awali wananchi
hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro
kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila
ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.
Wakizungumza
na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin,
Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika
kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya
mkopo toka Dawasco.
Walisema
kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba
kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani
ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna
kinachoendelea hadi sasa.
“Kinachotushangaza
ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji
huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji
uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa
kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.
Mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)