Saturday, July 2, 2016

johngagariniblog: WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI

johngagariniblog: WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI: Na John Gagarini, Kibaha   MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakuu wapya wa wilaya wlioteuliwa na Rais Dk John...

Friday, July 1, 2016

WAKUU WA WILAYA WAPYA WAAPISHWA PWANI


Na John Gagarini, Kibaha

 

MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakuu wapya wa wilaya wlioteuliwa na Rais Dk John Magufuli mkoani humo kuinua pato la wananchi wa mkoa huo kutoka milioni 1.2 kwa mwaka hadi milioni 3 kwa mwaka.

 

Aliyasema hayo jana mjini Kibaha wakati akiwaapisha wakuu hao wa wilaya wapya na kusema kuwa pato la mwananchi wa mkoa wa Pwani liko chini sana licha ya kuwa na fursa mbalimbali za kipato.

 

Ndikilo alisema kuwa kutoakana na pato hilo la wananchi kuwa dogo kiasi hicho hata mchango wa mkoa kwa Pato la Taifa ni dogo sana la asilimia 1.8 jambo ambalo linapaswa kuwekewa mkakati wa kupandisha pato hilo ili liwe na mchango mkubwa kwa mwananchi na Taifa kwa ujumla.

 

“Nawapongezeni kwa kuchaguliwa kwenye nafasi hizi na mkoa tayari umeandaa mpango kazi wake kwa ajili ya kuinua pato la mwananchi hivyo mnapaswa kuweka vipaumbele ambavyo vitasaidia kuinua uchumi wa wananchi wa wilaya unayoongoza,” alisema Ndikilo.

 

Alisema kuwa hakuna sababu ya mkoa kuendelea kuwa na pato dogo huku kukiwa na vyanzo vingi vya mapato ikiwa ni pamoja na rasilimali mbalimbali kama vile uvuvi, kilimo, korosho, maliasili ikiwa ni pamoja na mbuga za wanyama na madini mbalimbali.

 

“Mfano ni majumba mengi yanayojengwa Dar es Salaam kokoto na mawe yanatoka mkoa wa Pwani hivyo hakuna sababu ya kuwa maskini tuna zao la korosho ambapo kwa msimu uliopita wakulima waliuza korosho zenye tahamani ya shilingi bilioni 18,” alisema Ndikilo.

 

Aliwataka wahakikisha wanawajibika na kutowalea watumishi ambao ni kikwazo na wenye urasimu wa kuwahudumia wananchi ambao hufika ngazi ya mkoa kulalamika ili hali ngazi za chini kuna watendaji ambao wangeweza kutatua matatizo hayo.

 

“Changamoto ni nyingi ikiwa ni pamoja na suala la ulinzi na usalama, wahamiaji haramu, matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi nisingependa mambo haya yatokee tena hakikisheni mnatimiza wajibu wenu na kuwaondolea kero wananchi,” alisema Ndikilo.

 

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga alisema kuwa moja ya changamoto ambazo atakabiliana nazo ni pamoja na wahamiaji haramu kw akudhibiti bandari 19 ambazo zimekuwa ni njia ya wahamiaji hao haramu.

 

Naye Asumpter Mshama alisema kuwa moja ya mambo atayapaa kipaumbele ni kuhakikisha fedha kwa makundi ya vijana na akinamama asilimia 10 zinatoka ili wananchi waweze kujenga uchumi wao na ule wa Taifa.

 

Wakuu wapya walioapishwa jana ni pamoja na Shaibu Nunduma wilaya ya Mafia, Filberto Sanga Mkuranga, Gulamu Kifu wilaya ya Kibiti, Asumpter Mshama wilaya ya Kibaha, Juma Njwayo wilaya ya Rufiji na Majid Mwanga wilaya ya Bagamoyo huku Happyness William hakuweza kuapishwa kutokana na dharura.

 

Mwisho.


 MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo kushoto akimkabidhi zana za kufanyia kazi mkuu wa wilaya ya Kibiti Gulamu Kifu, baada ya kumwapisha kwenye hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu huyo wa mkoa

Mkuu mpya wa wilaya ya Kibaha Asumpter Mshama kulia akiapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo kushoto wakati wa hafla iliyofanyika mjini Kibaha ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya za mkoa huo ambao waliteuliwa hivi karibuni na Rais Dk John Magufuli

Mkuu mpya wa wilaya Rufiji Juma Njwayo kulia akiapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo wakati wakiapishwa wakuu wa wilaya za mkoa huo kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa huo. 



Saturday, June 25, 2016

WAKANUSHA KUPAKA KINYESI NA KUVUNJA OFISI YA KATA

Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI wa Mtaa wa Machinjioni Loliondoa au Sagulasagula waliobomolewa nyumba zao na Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani kwa tuhuma za kujenga nyumba kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko wamekanusha kuapaka kinyesi na kuvunja vioo vya ofisi ya kata ya Maili Moja.

Akizungumza na waandishi wa habari moja ya wahanga wa tukio la bomoa bomoa hiyo iliyofanyika Juni 16 na 17 mwaka huu ambapo watu hao walifanya uharibifu huu siku moja baada ya bomobomoa hiyo huku jumla ya nyumba 18 zilibomolewa, Said Tekelo amesema kuwa wao hawahusiki na tukio hilo na wamesikitishwa na kitendo hicho.

Tekelo amesema kuwa kitendo hicho kimefanywa na watu ambao walikuwa na malengo yao na hawaungi mkono watu waliofanya uharibifu huo kwani ni tukio ambalo ni kinyume cha sheria na hakistahili kuunga mkono.

Amesema kuwa wao kama wahanga wa bomobomoa hiyo hawawezi kufanya hivyo kwa sababu bado wako katika kutafuta haki yao waliyoipoteza baada ya nyumba zao kubomolewa pasipo kupewa fidia yoyote hivyo wasingeweza kufanya uharibifu.

Aidha amesema kuwa vi vema vyombo vya kisheria vikafanya yake ili kubaini wale waliofanya hivyo na kuwachukulia hatua kazi za kisheria kwani hao ni wahalifu kama wahalifu wengine na hawahusiani na waliobomolewa nyumba zao.

Amebainisha kuwa suala lao liko mahakamani tangu zoezi la kubomolewa nyumba zao lilipofanyika na hawaungi mkono watu waliofanya hivyo na wanawalaani vikali watu hao ambao wamejificha kwenye mwamvuli wa uhalifu.


MWISHO

ZEGERENI KUJENGA SHULE YA MSINGI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha umefayatua matufali 2,500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa shule ya Msingi katika mtaa huo ambao unategemea mtaa wa Visiga kuwapeleka watoto wao umbali wa kilometa nane.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa zoezi la kuwapa zawadi wanafunzi wa darasa la saba ambao wamefanya vizuri na kuwa kwenye 10 bora mwenyekiti wa mtaa huo Rashid Likunja amesema kuwa wanatarajia kuanza ujenzi wa shule hiyo kuanzia Julai Mwaka huu ili ifikapo mwakani watoto wao waanze kusoma kwenye shule hiyo.

Likunja amesema kuwa fedha za kununulia kiwanja chenye ukubwa wa hekari sita zimetokana na mchango wa shilingi 5,000 kila kaya ambapo hatua ya ujenzi itaanza kwa kutumia tofaali hizo huku wakiwa na mifuko 12 ya simenti wakianza na madarasa mawili, ofisi na matundu manne ya vyoo.

Amesema kuwa kwa sasa wako kwenye harakati za kupata kibali cha ujenzi pamoja na ramani toka Halmashauri ya Mji ili waweze kuanza ujenzi huo na utawapunguzia watoto wao kwenda kusoma mbali pia huwabidi kuvuka barabara ya Morogoro ambapo ni hatari kwao kwani wengine ni wadogo sana.

Aidha amewataka wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili waweze kutekeleza azma yao ya ujenzi wa shule hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa watoto wanaotoka mtaa huo ambao wanafikia zaidi ya 200 wanaosoma madarasa mbalimbali kutoka mtaa huo ambao wanasoma shule jirani ya Visiga.


Mwisho.   

Thursday, June 23, 2016

MILIKINI MAENEO KIHALALI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI-RC

Na John Gagarini, Kibaha

MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakazi wa mkoa huo kufuta taratibu na sheria za kumiliki ardhi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo kwa sasa imeshamiri na inaweza kuhatarisha amani.

Aidha amesema kuwa mkoa hautasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu ambao wanavamia maeneo ya watu na kuyauza kama wanavyofanya baadhi ya watu kwani ni kinyume cha sheria na watachukuliwa hatua kali ili waachane na tabia hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na baadhi wananchi kutoka wilaya ya Mkuranga Ndikilo alisema kuwa kumekuwa na migogoro mingi ambayo imesababisha wananchi kutokuelewana wao kwa wao.

“Moja ya mfano ni Kijiji cha Kazole Kitongoji cha Magodani Kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga kuna baadhi ya watu wanajifanya kamati ya ardhi ya Kijiji hicho kulivamia shamba la kampuni ya Soap Allied Industry ambalo lina ukubwa wa hekari 1,750 likiwa na hati ya umiliki 271 ambayo iliipata tangu mwaka 1988 ambalo lilitengwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,”alisema Ndikilo.

Ndikilo alisema kuwa kamati hiyo ambayo imekuwa ikiuza viwanja kwenye eneo hilo inafanya makosa kwa kuwauzia watu kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria kwani eneo hilo lina mmiliki halali ambaye anamiliki kisheria.

“Kama haitoshi watu hao walikwenda kwenye vyombo vya sheria lakini walishindwa na kuambiwa kuwa eneo hilo ni mali ya mtu hivyo hawapaswi kuingie kwenye eneo hilo lakini wanakamati hao bado wanaendelea kuwauzia watu na kujipatia mamilioni ambayo yote yanaingia mifukoni mwao na wamejinufaisha kupitia shamba hilo lakini wanawaibia watu kwani mmiliki mwenyewe yupo,” alisema Ndikilo.

Aidha alisema kuwa suala la shamba hilo linachukuliwa kisiasa lakini mwisho wa siku linaweza kusababisha uvunjifu wa amani kwani watu waliotoa fedha zao watakapoambiwa waondoke watadai fedha zao na hakuna mtu wa kuwarejeshea hivyo kuleta migogoro ambayo haitakiwi.

Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa ni vema watu wakafuata sheria bila ya shuruti kwani eneo hilo limeshatolewa maamuzi baada ya watu waliouziwa kwenda mahakamani na kuonekana kuwa kampuni hiyo ndiyo yenye uhalali wa kumiliki eneo hilo hivyo watu kuingia humo ni kuvunja sheria na wanaweza kukamatwa na polisi

Mushongi alisema kuwa watu hawapaswi kuingia kwenye eneo hilo ambapo hivi karibuni zaidi ya watu 20 waliingia kwenye shamba na kukamatwa na kwa kuwa hati ya umiliki bado haijatenguliwa watu wasiingie na kama wanaona wana haki ni vema wakaenda mahakama za juu kudai haki yao lakini si kulivamia.


Mwisho.       


KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho