Sunday, December 31, 2023

ALIYEESHINDA TUZO YA MALKIA WA UINGEREZA ATAKA DIASPORA WAPEWE HADHI MAALUM WAWEZE KULETA MAENDELEO NCHINI.





MTANZANIA ambaye alipata Tuzo ya Malkia Elizabeth || wa Uingereza, Prudence Kimiti amesema kuwapa hadhi maalum Diaspora itasaidia waweze kuwekeza nchini.

Kimiti aliyasema hayo Jijini Dar es Salaam alipotua nchini akitokea Uingereza anapoishi ambapo  hadhi hiyo ikitolewa itasaidia sana kwa Diaspora kufanya uwekezaji ili kuleta maendeleo.

Prudence ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere ambaye pia aliwahi kuwa Mkuu wa baadhi ya Mikoa hapa nchini alisema kuwa yeye anaipenda Tanzania hivyo anatamani kutoa mchango wake wa maendeleo kwa nchi. 

"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa jinsi anavyopambana kuwaletea Watanzania maendeleo hivyo watoe hadhi hiyo maalum kwa Watanzania wanaoishi nje ya nchi na ikiwa hivyo itasaidia kuwekeza ndani ya nchi yao,"alisema Kimiti.

Alisema kuwa suala kupewa hadhi maalumu kwa Watanzania wanaoishi nje ya nchi ni zuri kwani litasaidia kuleta maendeleo kwenye nchi yao.

Akizungumzia kuhusu tuzo aliyoipata ya Malkia wa Uingereza ya (MBE) aliipata kutokana na kutetea haki za watu weusi hasa wafanyakazi ambapo kuna baadhi ya changamoto wanazipata kutokana na rangi zao.

"Tuzo hii inafaida kubwa kwani inanipa moyo kuendelea kupigania haki za watu dunia nzima siyo Uingereza hata sehemu nyingine kwani napenda kila mtu apate haki yake,"alisema Kimiti.

Aidha alisema kuwa anatarajia kuanzisha shirika kwa ajili ya kusaidia makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto na wale waishio kwenye mazingira magumu.

"Tunaendeleza falsafa za mwasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Nyerere ambaye Waingereza wanampenda hivyo najivunia kuwa Mtanzania na tutaendeleza mazuri aliyoyaacha Nyerere,"alisema Kimiti.

Kwa upande wake Mzee Paul Kimiti alisema kuwa wanajivunia tuzo aliyoipata mtoto wao kwani imeiheshimisha familia na nchi kwa ujumla.

Kimiti alisema kuwa tangu mwanae akiwa mdogo alikuwa hapendi kuona mtu anaonewa na hilo amekwenda nalo hadi kufikia kupata tuzo hiyo na si bahati bali ni kitu kiko kwenye damu yake.

Alisema kuwa hata babu yake aliwahi kupata tuzo  mwaka 1950 na sasa mwanae naye anapata tuzo hiyo hivyo ni jambo la kujivunia sana kwa nchi kutokana na tuzo hiyo.

Prudencia Kimiti alipata tuzo hiyo ya malkia hiyo wakati wa malkia kutimiza miaka 70 ya uongozi wa Malkia ambapo hutolewa kila mwaka.

Saturday, December 30, 2023

SIKU YA LISHE YA KIJIJI GAIRO DC


GAIRO DC

SIKU YA AFYA NA LISHE YA KIJIJI

NIMEPATA FURSA YA KUZUNGUMZA NA WAKINA MAMA. 

NIMESISITIZA KUHUSU LISHE, NIMEWAKUMBUSHA MALEZI YA WATOTO KWA KUWALINDA DHIDI YA UKATILI. UZOEFU UNAONESHA KUWA MATUKIO MENGI YA UKATILI YANAANZIA KWENYE NYUMBA ZETU KWA KUWAAMINI NDUGU TUNAOWAKARIBISHA HADI KUWALAZA KITANDA KIMOJA NA WATOTO WETU.

GAIRO DC - KAZI INAENDELEA

@ortamisemi 

@wizara_afyatz 

@rs_morogoro 

@jabiri_makame

Thursday, December 28, 2023

WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA GARI WALILOKUWA WAKISAFIRIA KULIGONGA GARI LINGINE KWA NYUMA

WATU watatu wamefariki dunia na wawili kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuligonga gari lingine kwa nyuma ambalo lilikuwa limesimama.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Lutumo amesema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 28 majira ya saa 11:45 alfajiri eneo la Mbwewe Chalinze Wilayani Bagamoyo.

Amesema kuwa watu hao waliofariki walikuwa kwenye gari lenye namba za usajili T 395 DWE aina ya Alphard likiendeshwa na Mohamed Athuman (40) mkazi wa Jijini Dar es Salaam.

"Gari hilo lilikuwa likuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Kabuku mkoani Tanga ambapo liligonga kwa nyuma gari lenye namba za usajili T 300 CLE na tela namba T 399 AUP aina ya FAW lililokuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara,"amesema Lutumo.

Aidha amewataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni Zakia Mohamed (36) ambaye ni mwalimu, Goletha (23) msichana wa kazi na Nadim Nurdin miezi (8) wote wakazi wa Kabuku.

Amewataja majeruhi kuwa ni dereva wa gari hilo Athuman na Alice Sangule (8) ambaye ni mwanafunzi na mkazi wa Kabuku.

"Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari lililosimama Alphonce Bosco (55) Mkazi wa Mabawa Tanga, kuegesha gari pembezoni mwa barabara bila ya kuweka alama za tahadhari kwa watumiaji wengine wa barabara,"alisema Lutumo.

Aliongeza kuwa miili ya marehemu na majeruhi walipelekwa Hospitali ya Mkata Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga kwa hifadhi na matibabu.

"Jeshi la Polisi linatoa rai kwa madereva kuendelea kuchukua tahadhari na kuheshimu sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazosababishwa na uzembe katika kipindi hichi cha sikukuu kwani watu wengi wanasafiri kuelekea mikoa mbalimbali kwa ajili ya kusherehekea na familia zao,"amesema Lutumo.


Saturday, December 16, 2023

ATFT KUENDELEZA VIPAJI KUPITIA KIPAJI BILA MIPAKA








KITUO cha kuendeleza vipaji Africa Talent Forum-TZ (ATFT) cha Mkoani Pwani imewakutanisha wasanii wa fani mbalimbali ili kujadili namna ya kuendeleza vipaji vya wasanii ili viweze kutoa ajira.

Akizungumza kwenye kikao maalumu kujadili masuala mbalimbali ya namna ya wasanii wanavyoweza kupata fursa za kuinua vipaji vyao Mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho Rosemary Bujash amesema kuwa vipaji hivyo bila ya kuendelezwa havitaweza kufika mbali

Bujash amesema kuwa lengo la kuanzisha kituo hicho ni kusaidia wasanii na watu wenye vipaji au ndoto mbalimbali waweze kuzifikia ili kujiletea maendeleo kupitia vipaji vyao.

"Katika kuhakikisha vipaji vinaendelea na ndoto za watu zinatimia tumekuja na mradi wa Kipaji bila Mpaka ambapo tutahakikisha Tunaibua, Kukuza na Kuvitangaza ili wafikie malengo na kujiajiajiri kwani kipaji ni ajira,"amesema Bujash.

Kwa upande wake ofisa utamaduni wa Halmashauri ya Mji Kibaha Evarista Kisaka amesema kuwa moja ya changamoto kwa wasanii wachanga ni kutojitangaza hivyo kituo hicho wakitumie ili kutangaza kazi zao.

Kisaka amesema kuwa wasanii hao wanapaswa kujisajili na kutumia fursa mbalimbali zilizopo zinazotokana na sanaa na utamaduni na sanaa siyo uhuni bali ajira kama ajira nyingine na wao ni kioo cha jamii.

Naye mwenyekiti wa Wasanii Kibaha Jimanne Kambi amesema kuwa wasanii wako wengi lakini hawapati fursa kuonyesha vipaji vyao hivyo watashirikiana na kituo hicho kuinua wasanii.

Kambi amesema moja ya njia wanazotumia kutangaza kazi za wasanii ni kuwashirikisha kwenye matamasha mbalimbali ili kazi zao zionekane ambapo katika usajili wameandikisha wasanii zaidi ya 700.

Awali Ofisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Mkuza Victoria Andrea amesema kuwa wasanii wanapaswa kuwa wabunifu ili kuboresha kazi zao ziweze kuvutia watu.

Andrea amesema sekta ya sanaa ina ajira kubwa endapo itatumika ipasavyo kwani ina fursa nyingi zikiwemo za mikopo kwa ajili ya wasanii hivyo ni wao kujisajili ili watambulike kisheria.

Wednesday, December 6, 2023

TPFNET CHALINZE WATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO DOLPHINE.

 

Jeshi la Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze, Mkoa wa Pwani, Disemba 05, 2023 wametoa msaada kwa watoto wenye uhitaji katika kituo cha Dolphine kilichopo Kijiji cha Kipera, Kitongoji cha Mwanabele Wilayani humo.

Akizungumza akiwa kituoni hapo,  Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Sophia Lyidenge alisema jukumu la ulezi wa watoto wenye uhitaji na kuwatunza ni la jamii nzima hivyo wao wakiwa ni sehemu ya wazazi wameguswa katika siku 16 za maadhimisho ya kupinga ukatili wa Kijinsia kufikia kwa watoto hao wenye uhitaji na kuweza kutoa msaada wa vitu mbalimbali. 

"Jamii inapaswa kutambua malezi ya watoto na kuwatunza na kuwatembelea mara kwa mara kujua changamoto walizonazo na kuzitafutia ufumbuzi watoto wenye uhitaji kwenye vituo vya malezi ni la watu wote na kufanya hivyo ni kuwapa faraja watoto walio kwenye vituo hivyo kuona jamii ina wajali na kuwathamini".Alisema Lyidenge.

Lyidenge amewapongeza wasimamizi wa kituo hicho kwa malezi ya watoto hao akiweka wazi kuwa jambo wanalolifanya la kuwalea watoto kwenye maadili mema ni kubwa sana mbele ya Mungu na la kupongezwa. 

Amesema kuwa watoto hao endapo wangeachwa bila ulezi kwenye kituo hiki wangeweza kuwa katika makuzi mabaya hivyo kutumbukia kwenye makundi ya kihalifu na hivyo kupeleka Jamii kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili.

Aidha, Lyidenge amewaasa watoto hao kuwa wasikivu kwa walezi wao na kutambua kuwa wao ni taifa la kesho akiwasisitiza kusoma kwa bidii ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za changamoto walizonazo kwa walezi wao bila woga ili ziweze kupatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa jamii  Bi. Linna Jackson Mlay ameahidi kuendeleza ushirikiano na walezi wa kituo hicho katika kutatua changamoto mbalimbali walizonazo.

Nae msimamizi wa kituo hicho Anna Munisi amelishukuru Jeshi la Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze kwa msaada waliowapatia na kuomba wananchi wengine kuendelea kusaidia kituo hiko kwani uhitaji ni mkubwa katika maelezi ya watoto waliopo kituoni hapo.

Msaada uliotolewa na Jeshi la Polisi kituoni hapo ni unga wa sembe, mchele, sabuni,  madaftari, kalamu na taulo za watoto.

Monday, December 4, 2023

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI YAWATAKA WANAWAKE KUMUENZI BIBI TITI MOHAMED KWA KULETA MAENDELEO

WANAWAKE nchini wametakiwa kupambana kuiletea nchi maendeleo kama alivyofanya Bibi Titi Mohamed ambaye aliasidiana na Mwasisi wa Taifa Julius Kambarage Nyerere kuleta uhuru wa Tanzania.

Aidha amewataka kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuwapatia fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo. 

Hayo yamesemwa Mlandizi Wilayani Kibaha na Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani Omary Punzi wakati wa mafunzo kwa wanawake ya Ijue Kesho yako.

Punzi amesema kuwa katika kupigania nchi kupata uhuru alishirikiana na Bibi Titi Mohamed hadi Uhuru ukapatikana hivyo wanawake nao wawe mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya nchi.

"Nyerere alijenga misingi ya maendeleo na aliona umuhimu wa mwanamke na ndiyo sababu alishirikiana na Bibi Titi katika mapambano ya Uhuru hivyo nanyi msikae nyuma lazima mpambane kuleta maendeleo ya nchi,"amesema Punzi.

TASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI YAWAPONGEZA WAANDAJI WA MAFUNZO YA IJUE KESHO YAKO KWA WANAWAKE MLANDIZI KIBAHA

 


Pongezi hizo zilitolewa na Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Punzi wakati wa mafunzo ya Ijue Kesho yako kwa wanawake wa mkoa wa Pwani yaliyofanyika Mlandizi Wilayani Kibaha.

Punzi alipata nafasi ya kuwashukuru na kuwaambia wanawake kuwa Mwalimu Nyerere alijenga misingi ya Uzalendo, kujituma na kujitoa kwa hali na mali katika nchi na misingi ambapo misingi hiyo ilitokana na nguvu ya Mwanamke katika kuleta maendeleo.

Alisema Mwalimu Nyerere katika Uongozi wake alijitahidi sana kuwainua wanawake mfano mzuri ni Bibi TITI MOHAMMED ambaye alikuwa karibu sana na Mwalimu katika kupigania Uhuru wa Taifa  na hakuna Taifa lolote linaloendelea ikiwa Mwanamke atawekwa nyuma.

"Ushauri wangu serikali inatakiwa kuwekeza nguvu kubwa ya kuhakikisha mwanamke anapatiwa mahitaji yote ya msingi endelevu ya kumwezesha katika kumuinua kiuchumi,"alisema Punzi.

Kwa upande wake mgeni rasmi Mkali Kanusu mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini ambaye alimwakilisha Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM NEC Hamoud Jumaa, aliwapongeza waandaji na wawezeshaji kwa mada zilizokuwa zinatolewa ni nzuri na mahiri kwa wakati tulionao kwa Serikali ya Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kanusu alishauri matukio kama hayo yafanyike mara mbili kwsa mwaka kwani itasaidia kuwakumbusha watu maadili ya Watanzania na kama chama wamelipokea na kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za maendeleo kwa wanawake wa Kibaha na Tanzania kwa ujumla.

Naye Mwakilishi wa Taasisi ya IJUE KESHO YAKO Ndugu Martha Kyoka alisema lengo kuu la Taasisi hiyo ni kuhakikisha wanamjengea uwezo mwanamke kujitambua na kutekeleza malengo katika maisha na jamii kwa ujumla ambapo takribani wanawake 100 walipatiwa mafunzo hayo.

Masomo waliyofundishwa ni pamoja na Afya ya Akili, malezi ya mume na mtoto nyumbani, nafasi ya kujitambua, Uwekezaji, Maono na Mikopo na Ujasiriamali.

Sunday, November 26, 2023

*KATENI UMEME KWA WADAIWA - DKT. BITEKO AIAGIZA TANESCO*

*📌Akemea vikali wahujumu wa miundombinu ya umeme, Asema Serikali iko kazini, Itawashughulikia*

*📌Ataka TANESCO  kusikiliza na kujibu Wateja kwa haraka*

*📌Asisitiza utunzaji wa Mazingira*

Arusha

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kukata umeme kwa wadaiwa wote wasiolipa gharama za kutumia umeme ambapo Shirika hilo linadai jumla ya Shilingi Bilioni 224 kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali, Binafsi na waliohama na madeni kutoka mita za zamani za umeme kwenda za kisasa hali inayopelekea changamoto katika utekelezaji wa majukumu ya TANESCO.

Amesema hayo tarehe 26 Novemba 2023, wilayani Arumeru mkoani Arusha, wakati alipokagua kituo cha umeme cha Lemuguru mkoani Arusha ambacho ujenzi wake ni sehemu ya mradi  wa ujenzi  wa njia  kuu ya umeme  ya msongo wa kV 400 kutoka Singida mpaka Namanga kuelekea Kenya ( Kenya- Tanzania Power Interconnection Project (KTPIP).

“Hapa Arusha tu, TANESCO anadai wateja wake shilingi bilioni 7.7, na mara nyingi wanaodaiwa si wanachi wadogowadogo bali Taasisi za Serikali na Wawekezaji wanaojiita wawekezaji wakubwa ambao ukiwakatia umeme wanakwambia unaua ajira,  wepesi wa kujificha kwenye kisingizio cha kulipa kodi na ajira; TANESCO anahitahi fedha ili awekeze na kisha awapelekee umeme wananchi, TANESCO nawaambia kateni umeme kwa mtu yeyote mnayemdai ili mradi unamdai kwa haki.” Amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko pia ameagiza wadaiwa wote wa madeni ya bili za umeme wakalipe madeni hayo ili zipatikane fedha za kuwahudumia wananchi na ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kushughulikia changamoto za umeme nchini kwa aina mbalimbali ikiwemo kuendelea kutekeleza miradi ya uzalishaji umeme ukiwepo wa Julius Nyerere (MW 2115), ambao umefikia asilimia 94 ambapo amesema kuwa, Mkandarasi ameshafunga mashine mbili tayari kwa kuanza majaribio ya kuzalisha umeme.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amekemea vikali watu wote wanaohujumu miundombinu ya umeme akitolea mfano wizi wa shaba na mafuta ambapo kati ya tarehe 25 Novemba, 2023 na 26 Novemba, 2024 kuna matukio 14 katika Ukanda wa Pwani ya kuharibu au kuhujumu miundombinu ya umeme, ambapo ameeleza kuwa, Serikali itawashughulikia kwa kuendesha msako na watakapopatikana sheria itachukua mkondo wake.

Aidha, Dkt. Biteko ameitaka TANESCO kuwasikiliza na kuwapatia majibu kwa haraka wananchi wanaopiga simu kwenye Shirika hilo ili kupata huduma za umeme na mahali penye matatizo waambiwe, “huu utaratibu wa watu kupiga simu anaambiwa subiri, hii tumekubaliana kuwa haiwezekani ikaendelea na ndio maana nimewaambia kituo cha Huduma kwa Mteja tukiimarishe kutoka miito 65 na ziongezwe kufika 100 na zaidi.” 

Dkt. Biteko ametaka Watanzania  kulinda vyanzo vya maji ambavyo vinazalisha umeme, amesema vyanzo hivyo visipolindwa vitapelekea athari mbalimbali zikiwemo kwenye uzalishaji umeme, na pia ameitaka TANESCO kutokukaa nyuma  katika masuala ya utunzaji wa mazingira bali washirikiane na Wizara inayoshughulika na suala la mazingira na NEMC ili wote kwa pamoja washirikiane kusimamia mazingira.

Kuhusu utekelezaji wa kituo hicho cha umeme cha Lemuguru kilichopo wilayani Arumeru Mkoa wa Arusha, Dkt. Biteko amesema kuwa mradi huo ni mkubwa na unagharimu Dola za Marekani milioni 258.8 na kina faida mbalimbali ikiwemo kupelekea wananchi umeme usiokatika mara kwa mara na kituo kitaimarisha hali ya umeme mkoani Kilimanjaro na Arusha.

Dkt. Biteko vilevile ameipongeza TANESCO kwa hatua mbalimbali inazochukua ili kupunguza makali ya mgawo wa umeme pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kuongeza kiwango cha Gesi Asilia kinachozalisha umeme.

Awali, akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa njia Kuu ya kusafirisha umeme wenye msongo wa Kilovoti 400 kutoka Singida hadi Namanga kuelekea Kenya, Msimamizi wa Mradi huo Mhandisi Peter Kigadye, amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuongeza uwezo wa kusafirisha umeme kwenda mikoani na migodi ya uchimbaji madini na hivyo kuwezesha kufikia uwezo wa juu wa megawati 2000 katika kusafirisha umeme.

Amesema, utekelezaji wa mradi unahusisha vipengele Sita  ikiwemo ujenzi wa njia 8 za laini ya kV 400/33 kutoka Kituo kipya cha kupoza umeme, ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa kV 400 kutoka Singida hadi Namanga kupitia Arusha yenye urefu wa kilomita 414.3, Babati -Arusha kilomita 150, Arusha –Namanga, Kilomita 114.3 ambao umefikia asilimia 96.

Ameeleza mradi huo pia unahusisha, upanuzi wa vituo vya kupoza umeme ambao umefikia asilimia 98.72, mradi wa usambazaji umeme kwa vijiji vilivyopitiwa na mradi vijiji na ujenzi wa vituo vyq kupoza umeme vya Dodoma, Singida, ambavyo vimekamilika.

*DKT. BITEKO ATUNUKU VYETI KWA WAHITIMU 439 CHUO CHA MWEKA*

 

*📌Awataka kuchukia rushwa na kulinda Maliasili kwa Wivu Mkubwa*

*📌Apongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa usimamizi wa Sekta*

*Kilimanjaro* 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametunuku vyeti vya ngazi mbalimbali kwa wahitimu 439 wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori cha Mweka, mkoani Kilimanjaro ambapo amewaasa kuwa chochote watakachofanya kuchukia rushwa, kutojitajirisha katikati ya hali ngumu za wananchi na walinde maliasili za nchi kwa wivu mkubwa na kuwa walinzi wa wenzao.

Amesema hayo tarehe 25 Novemba, 2023 wakati alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mahafali ya 59 ya Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka, mkoani Kilimanjaro ambapo Mahafali hayo yameenda sambamba na Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Chuo hicho.

“Chuo hiki ni kiungo muhimu katika Sekta ya Maliasili na Utalii, kuanzishwa kwake kulitokana na  tamko la Baba wa Taifa, Hayati, Mwl. Julius Kambarage Nyerere katika Kongamano la Uhifadhi wam Wanyama Pori mwaka 1961, na kupitia tamko hilo alionesha dhamira na utayari wake wa kuifanya Afrika kuwalinda wanyama na mazingira yao kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo, hivyo nyinyi ndio mnaoendeleza kazi lengo hilo la Baba wa Taifa.” Amesema Dkt. Biteko

Amesema kuwa, Chuo hicho pia ni kielelezo cha ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na nchi nyingine duniani kwani Chuo hicho kinapata wanafunzi kutoka nchi mbalimbali duniani.

Amesema kuwa, Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua mchango wa Chuo hicho katika ukuaji wa Sekta ya Maliasili na Utalii nchini na hivyo ameahidi kuwa kama kuna changamoto zozote Serikali itazichukua na kuzifanyia kazi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kusimamia vyema sekta ya Maliasili na Utalii ambayo amesema kuwa ni kiungo kikubwa kwenye uchumi wa nchi kwani bila Sekta hiyo mapato na fedha zinazohitajika kuendeleza miradi mbalimbali zinaweza kuwa na changamoto ya upatikanaji.

Amesema, Utalii unachangia takribani asilimia 21 ya Pato la Taifa, na asilimia 25 ya fedha za kigeni, pia ni chanzo kikubwa cha ajira nchini kwani unachangia ajira milioni 1.5 na zaidi ya asilimia 11 ya ajira zote hapa nchini.

Dkt. Biteko aliongeza kuwa, asilimia 80 ya Utalii nchini unatokana na Wanyama pori, ambao wametokana na mazingira yetu tuliyoyahifadhi, mapori ya akiba, mapori tengefu, misitu pamoja na hifadhi za wanyama.

Katika Mahafali hayo wahitimu 439 walitunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali za masomo ikiwemo Shahada ya Uzamili ya Mipango na Usimamizi wa Utalii, Shahada ya Usimamizi wa Wanyamapori, Stashahada ya Juu ya Utalii wa Wanyamapori, Astashahada ya Usimamizi wa Wanyamapori na Cheti cha Msingi cha Usimamizi wa Wanyamapori.  

Mahafali hayo yalihudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania, Ricardo Mtumbuida.

Thursday, November 23, 2023

MAOFISA KILIMO PWANI WAPEWA VISHKWAMBI KUBORESHA UTENDAJI KAZI

MKOA wa Pwani umewakabidhi Vishkwambi 345 kwa Maofisa Kilimo wa Wilaya za mkoa huo ili kuleta tija na kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge wakati akikabidhi vifaa hivyo ambavyo vimetolewa na Serikali.

Kunenge amesema kuwa matumizi mengine ni kusajili wakulima ambao bado hawajaingizwa kwenye mfumo na kuboresha taarifa za wale waliosajiliwa ili wahudumiwe kwa idadi na kujua mahitaji yao ya pembejeo.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala wa mkoa wa Pwani Shangwe Twamala amesema wanaishukuru Wizara ya Kilimo kwa kuwapatia vifaa hivyo.

Naye Ofisa Kilimo wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Joseph Njau amesema kuwa vifaa hivyo vitawawezesha kutekeleza majukumu yao na kuongeza uzalishaji na kuleta tija kwa wakulima kwenye maeneo yao.

Wednesday, November 22, 2023

JAMII MKOANI PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO

JAMII Mkoani Pwani imetakiwa kuhakikisha ulinzi na usalama wa mtoto kwa kumuondolea vikwazo na kutoa taarifa kwa wanaofanya vitendo vya ukatili ili mtoto aweze kutimiza ndoto zake.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu Tawala wa Mkoa huo Rashid Mchatta alipokuwa akizindua mradi wa Usalama wa Watoto (UWAWA) awamu ya pili unaosimamiwa na Christian Social Services Commission (CSSC).  

Mchatta amesema watoto wanakabiliwa na changamoto nyingi ambapo jamii inatakiwa kuwalinda kwani nao wana ndoto zao za kuwa nani katika jamii mara wamalizapo masomo yao.

"Mradi wa uwawa una lengo la kuimarisha usalama wa watoto utasaidia kuanzishwa dawati la kushughulikia changamoto za watoto kukabiliana na ukatili kwa watoto shuleni na sehemu yoyote wawapo watoto,"amesema Mchatta. 

Naye Ofisa elimu Mkoa wa Pwani Sara Mlaki amesema kuwa vitendo vya ukatili kwa watoto wakati mwingine vinatokana na utandawazi na baadhi wanafanyiwa na wazazi wa kuwazaa kama kuwanyima chakula na watoto hujikuta wakifanya vibarua ili wapate fedha.

Kwa upande wake Meneja wa Kanda ya Mashariki wa (CSSC) Makoye Wangeleja amesema kuwa wanaushukuru mkoa kwa kutoa ushirikiano kwani vita hiyo siyo lelemama kwani watu wanaowafanyia vitendo hivyo ni watu ambao huwezi kuwafikiri na inabidi kujipanga ili kukabili vitendo hivyo vya ukatili kwa watoto na watafuata taratibu ili kuweka misingi mizuri ya kuwalinda watoto.







PWANI YAMSHUKURU RAIS KWA KUIPATIA FEDHA ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

SERIKALI Kuu imeupatia Mkoa wa Pwani kiasi cha shilingi  trilioni 1.1 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imeainishwa kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hayo yamesemwa na Kamisaa ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge  wakati akiwasilisha taarifa ya miradi iliyotekelezwa mkoani humo katika kipindi cha Machi 2021 hadi Juni 2023 kwenye kikao cha Kamati kuu ya Chama hicho mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kwa Mfipa wilayani Kibaha.

Kunenge amesema utekelezaji wa miradi hiyo ni mafanikio makubwa yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya utawala wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambayo imetoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta za afya, elimu, nishati, maji na miundombinu ya barabara.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao amesema chama kimeridhika na miradi  iliyotekelezwa na serikali imetimiza  matakwa yaliyopo kwenye Ilani ya CCM  katika kuwaletea  maendeleo wananchi wake.

Kwa upande wake Katibu  wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Pwani  Benard Ghatty amesema hadi sasa serikali imefikisha asilimia 98 ya  utekelezaji wa miradi na kwamba sehemu iliyosalia ni ndogo ambapo wanaamini ifikapo mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu miradi yote itakamilika.

Monday, November 20, 2023

MAOFISA TARAFA NA WATENDAJI KATA PWANI WATAKIWA KUWA WABUNIFU KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewataka Maofisa Tarafa na Watendaji Kata kuwa wabunifu kwa kutafuta suluhisho la kutatua changamoto za wananchi.

Ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ili kuboresha utendaji kwa maofisa hao kutoka Halmashauri tisa za mkoa huo.

Kunenge amesema kuwa kazi kubwa ya kiongozi ni kutatua changamoto ili kuwaletea wananchi maendeleo kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo pia kujua jamii inataka nini.

"Inashangaza kuona Rais anapelekewa malalamiko kutoka kwa wananchi na sisi tupo ambapo tungeweza kutatua changamoto husika lazima tuwe na ubunifu na kufanya kazi kwa weledi,"amesema Kunenge.

Naye Mkurugenzi msaidizi idara ya serikali za mitaa Ibrahim Minja amesema kuwa mafunzo hayo yana lengo la kuwaendeleza kiuwezo katika utekelezaji wa majukumu yao, kuwajengea uwezo na ufanisi na kujua na kuzifuata taratibu  kanuni, sheria na miongozo ya utumishi wa umma.

Minja amesema kuwa yanawahusisha maofisa hao 160 ambapo waliofika ni 152 ambapo ni ya awamu ya pili kwa Kanda ya Mashariki Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Mtwara awamu ya kwanza yalifanyika kwenye mikoa ya Songwe, Njombe, Rukwa na Katavi na timu nyingine ikifanya kwenye mikoa ya Singida, Tabora na Shinyanga.

Naye mshiriki wa mafunzo hayo Jane Mwanamtwa ofisa Mtendaji kata ya Kawawa wilaya ya Kibaha amesema yana umuhimu kwa sababu wanakumbushwa wajibu wao pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo kukamilika kwa wakati pamoja na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wananchi wanaowahudumia.



Friday, November 17, 2023

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA NYERERE YAADHIMISHA SIKU YA WATOTO NJITI DUNIANI YATOA MISAADA





KATIKA kuadhimisha siku ya watoto waliozaliwa kabla ya muda (Watoto Njiti) Duniani Tasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na baadhi ya wadau imetoa misaada kwa watoto njiti kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila.

Aidha imetoa misaada kwenye sekta ya elimu ili kuboresha mazingira ya usomaji na vifaa kwa wanafunzi wa baadhi ya shule Wilayani Kibaha.

Misaada hiyo ambayo ni saruji, sabuni, mafuta ya watoto na mavazi ya michezo vimetolewa leo  mbali ya Hospitali ya Mloganzila ni pamoja na Shule ya Msingi Kambarage na Mlandizi.

Katibu wa Taasisi hiyo ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani Omary Punzi amesema kuwa wamefikia hatua hiyo ili kuendelea kutimiza malengo ya Taasisi hiyo ambayo ni mapambano dhidi ya ujinga, maradhi na uamsikini.

Punzi amesema kuwa mbali na hilo pia hatua hiyo inalenga kuikumbusha jamii ili kutambua kuwa bado tatizo la watoto njiti lipo na linaendelea kuwaandama wajawazito wengi hivyo ni vema likapewa kipaumbele na kuongeza nguvu katika kukabiliana nalo.

Amesema kuwa Taasisi hiyo imeendelea kutekeleza malengo yake kwa kujiweka karibu na jamii ambapo katika msaada huo imeshirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki wanathamini wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi huduma za tiba wa Hospital ya Mloganzila Dk Faraja Chiwanga amesema kuwa sababu mbalimbali zinatajwa kuchangia hali hiyo ni pamoja na magonjwa yasiyoambukiza na ukosefu wa lishe bora.

Naye mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage Happynes Tesha amesema kuwa msaaada wa mifuko 50 ya saruji iliyotolewa na taasisi hiyo itaongeza nguvu ya ujenzi wa vyumba vya madarasa unaoendelea shuleni hapo.

Monday, November 13, 2023

KAMATI YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA YARIDHISHWA MRADI WA MAJI WAMI AWAMU YA TATU.

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma imetembelea mradi wa Maji wa Wami awamu ya tatu kwenye chanzo Mto Wami na kufurahishwa na jitihada za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuhakikisha huduma ya upatikanaji maji inakuwa ya uhakika.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Deus Sangu wakati wa ziara iliyofanywa kutembelea mradi huo kuangalia maendeleo ya mradi huo ambao kwa awamu zote umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 160.

Sangu amesema kuwa wameridhishwa na jitihada za Dawasa na kuahidi kuendelea kuipambania ili iweze kukabili changamoto za upungufu wa maji na kupitia Bunge kati ya maazimio 14 mawili ni ya kuisaidia mamlaka hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa upatikanaji wa maji kwa mkoa huo ni asilimia 86 ambapo aliomba miradi itekelezwe vizuri ikizingatiwa ni mkoa wa uwekezaji wa viwanda na mahitaji ya maji kwa sasa ni makubwa kwani kuna ongezeko la watu na uwekezaji mkubwa ambapo bila ya maji hakuna uwekezaji.

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameishukuru kamati hiyo kwa kupambani Chalinze kupata maji kwani kwenye mikutano yake hakuna jambo ambalo lilikuwa kero kwa wananchi kuhitaji maji ambapo kwa sasa changamoto ya maji imepungua kwa kiasi kikubwa.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi huo wa awamu ya tatu Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Kiula Kingu amesema kuwa maji yatazalishwa kutoka lita milioni saba hadi lita milioni 21 ambapo mabomba yatatandazwa kwa kilometa 124 na matenki 18 na kutakuwa na vituo vikubwa vya maji Miono, Msoga na Mboga.


Mwisho.

Monday, November 6, 2023

WAFANYABIASHARA WATAKIWA KULIPA KODI KWA HIYARI

WAFANYABIASHARA nchini wametakiwa kulipa kodi kwa hiyari ili wawe huru kufanyabiashara na kuchangia mapato ya serikali ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Taifa Hamis Livembe alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa Wilaya ya Kibaha wakati wa ziara yake kutembelea Mkoa wa Pwani.

Livembe alisema kuwa kila upande una wajibu kwa mwenzake ambapo serikali inaweka mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na kwa wafanyabiashara kazi yao ni kulipa kodi.

"Naombeni wafanyabiashara mlipe kodi kwa hiyari kwani serikali imeweka mazingira mazuri ya sisi kufanya biashara na hata kama kuna changamoto imeacha milango wazi kwa ajili ya majadiliano kama kuna kero kuhusiana na kodi,"alisema Livembe.

Alisema kuwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan ameamua kufungua milango ya biashara ili wafanyabiashara wafanye biashara zao kwa uhuru na hataki kuona wanabughudhiwa.

"Tumuunge mkono jitihada za Rais anazo zifanya kwa wafanyabiashara kwa kutatua kero zetu hivyo tukilipa kodi vizuri nchi itasonga mbele kwenye suala la maendeleo na nchi itafunguka,"alisema Livembe.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta alisema kuwa Jumuiya hiyo inafanya kazi kubwa ya kizalendo kwani nchi inapokusanya vizuri mapato yanarudi kwa wananchi kwa kutoa huduma kwa ufanisi.

Mchatta alisema kuwa wajibu wa kulipa kodi ni muhimu na kama kuna changamoto watashirikiana na wafanyabiashara kuzitatua kwa pamoja ili mazingira ya biashara yawe rafiki.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara (JWT) Mkoa wa Pwani Abdala Ndauka alisema kuwa wanaishukuru serikali kwa kutatua baadhi ya changamoto za wafanyabiashara.

Ndauka alisema kuwa changamoto zao zikitatuliwa watafanyabiashara kwa uhuru na kuwezesha biashara kukua hivyo kulipa kodi kwa hiyari na kuleta maendeleo ya nchi.

Moja ya wafanyabiashara ambaye ni mwanachama wa Jumuiya hiyo Mkoani humo Hassan Msemo alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata ni baadhi ya viwanda kutokuwa na stoo za kuuzia bidhaa wanazozizalisha ambapo nyingi ziko Jijini Dar es Salaam hivyo kuwagharimu kuzifuata.

Msemo alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo husababisha kuzifuata Jijini Dar es Salaam hivyo gharama kuwa kubwa na hata bei za kuuzia nazo zinakuwa juu.

Friday, November 3, 2023

MAGONJWA YAONGEZEKA MWINGILIANO WA BINADAMU WANYAMA NA MAZINGIRA

 

DODOMA.

SHUGHULI za kijamii na kiuchumi, mwenendo na mifumo ya maisha na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi kumekuwa na ongezeko la magonjwa yanayoibuka kutokana na mwingiliano uliopo baina ya binadamu, wanyama na mazingira.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama , wakati akifungua kongamano la kitaifa la Afya Moja ambapo amesema kuwa duniani kote takriban visa bilioni 1 vya ugonjwa na mamilioni ya vifo hutokea kila mwaka kutokana na magonjwa yanayotoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Aidha amezisihi Wizara za Kisekta kuwa na mipango ya kutekeleza na kuimarisha ushirikiano wa kisekta kwa kutumia mbinu ya Afya Moja na kila sekta kushiriki kikamilifu katika tafiti kuhusu magonjwa yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, utunzaji wa mazingira, usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema kuwa dhana ya Afya moja faida yake ni njia inayowaleta pamoja na sekta mbalimbali ambapo ni afya, mifugo na wanyamapori ili kukabiliana na changamoto zinazohusiana na afya.

Kila ifikapo Novemba 3 ya kila mwaka wadau mbalimbali huadhimisha siku ya Afya Moja kwa lengo la kuimarisha uratibu na utendaji uliopo baina ya sekta katika kuzuia na kupunguza madhara pamoja na kujiandaa kukabiliana na majanga ya milipuko ya magonjwa ya binadamu, wanyama na mimea ambapo kauli mbiu mwaka huu inasema “Afya Moja: Mbinu ya Pamoja kuboresha afya ya binadamu, wanyama, mimea na mfumo wa ikolojia kwa ustahimilivu wa maafa.

SHUGHULI ZA KIJAMII NA KIUCHUMI ZACHANGIA ONGEZEKO LA MAGONJWA

 

DODOMA.

IMEELEZWA kuwa shughuli za kijamii na kiuchumi, mwenendo na mifumo ya maisha na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi kumekuwa na ongezeko la magonjwa yanayoibuka kutokana na mwingiliano uliopo baina ya binadamu, wanyama na mazingira.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama , wakati akifungua kongamano la kitaifa la Afya Moja ambapo amesema kuwa duniani kote takriban visa bilioni 1 vya ugonjwa na mamilioni ya vifo hutokea kila mwaka kutokana na magonjwa yanayotoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Aidha amezisihi Wizara za Kisekta kuwa na mipango ya kutekeleza na kuimarisha ushirikiano wa kisekta kwa kutumia mbinu ya Afya Moja na kila sekta kushiriki kikamilifu katika tafiti kuhusu magonjwa yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, utunzaji wa mazingira, usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema kuwa dhana ya Afya moja faida yake ni njia inayowaleta pamoja na sekta mbalimbali ambapo ni afya, mifugo na wanyamapori ili kukabiliana na changamoto zinazohusiana na afya.

Kila ifikapo Novemba 3 ya kila mwaka wadau mbalimbali huadhimisha siku ya Afya Moja kwa lengo la kuimarisha uratibu na utendaji uliopo baina ya sekta katika kuzuia na kupunguza madhara pamoja na kujiandaa kukabiliana na majanga ya milipuko ya magonjwa ya binadamu, wanyama na mimea ambapo kauli mbiu mwaka huu inasema “Afya Moja: Mbinu ya Pamoja kuboresha afya ya binadamu, wanyama, mimea na mfumo wa ikolojia kwa ustahimilivu wa maafa.

Tuesday, October 31, 2023

TAKUKURU PWANI YAFANIKISHA MTENDAJI KUREJESHA MILIONI 4 ZA KIJIJI ALIZOZICHUKUA ZA MAUZO YA ARDHI

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kurejesha kiasi cha shilingi milioni nne za Kijiji cha Kanga zilifanyiwa ubadhirifu na kaimu mtendaji wa Kata ya Kanga wilayani Mafia.

Aidha fedha hizo ambazo ni asilimia tano ni tozo ya mauzo ya kiwanja cha Kijiji hicho ambacho kiko ufukweni mwa Bahari ya Hindi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Sadiki Alli akitoa taarifa ya miezi mitatu ya utendaji kazi kuanzia Julai hadi Septemba mwaka huu. 

Alli amsema kuwa mtuhumiwa huyo jina linahifadhiwa fedha hizo hakuziwasilisha ofisini wala kuzipeleka benki kwenye akaunti ya kijiji.

Amesema mtuhumiwa huyo ambaye pia ni ofisa mazingira wa kata alibainika kwenye mkutano wa Takukuru Rafiki ambapo wananchi waliibua kero hiyo na ndipo walipofanya uchunguzi juu ya tukio hilo na kufanya ufuatiliaji.

"Baada ya uchunguzi tulibaini kuwa tukio hilo ni la kweli na alirejesha fedha hizo na tumemwandikia mwajiri wake ili achukuliwe hatua zaidi za kisheria kuhusu tukio hilo,"amesema Alli.

Amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na mkutano wa Takukuru Rafiki na kuwataka wananchi watumie mikutano hiyo ili kutoa kero zao juu ya vitendo vya rushwa.

"Wananchi watoe kero zao za rushwa kupitia mikutano tunayoiandaa kupitia Takukuru Rafiki kwani hapo ni moja ya sehemu wanazoweza kutoa taarifa kama watashindwa kutuletea taarifa ofisini,"amesema Alli.

Katika hatua nyingine amesema kuwa jumla ya matukio 126 ambapo 92 yalihusu masuala ya rushwa huku 34 hayakuhusu rushwa na 27 wahusika walipewa ushauri manne yalifungwa na matatu yalihamishiwa idara nyingine.

Ameanisha idara ambazo zinaongoza kwa malalamiko kuwa ni Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) yenye malalamiko 44, na elimu 17, ardhi 15, ushirika sita, binafsi tano na polisi nne.

Ameongeza kuwa idara nyingine ni afya na kilimo tatu, bandari, fedha, madini, maji, misitu na utawala malalamiko mawili kila moja, idara ya biashara, ofisi ya mkuu wa wilaya, mifugo, maendeleo ya jamii, Mamlaka ya Mapato TRA, uchukuzi, ujenzi, Tanesco, utalii na viwanda lalamiko moja moja kila idara.

Wednesday, October 25, 2023

RC KUNENGE ATAKA UJENZI WA MALL YA HALMASHAURI YA MJI UKAMILIKE NDANI YA SIKU 14


MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametoa siku 14 kwa Mkandarasi anayejenga Maduka Makubwa (Mall) inayomilikiwa na Halmashauri ya Mji Kibaha kukamilisha ujenzi wa mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni nane.

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Halmashauri hiyo ambapo mradi huo uko kwenye kitovu cha mji karibu na stendi mpya ya Maili Moja Kibaha.

Kunenge amesema kuwa mradi huo ni mkubwa ambao utakapokamilika utagharimu kiasi cha shilingi bilioni nane hivyo lazima ukamilike ndani ya muda huo ambapo matarajio ni kuingiza kiasi cha shilingi milioni 450 kwa mwaka.

"Nataka mkandarasi Elray asizidishe zaidi ya wiki mbili ahakikishe anakamilisha ndani ya muda huo tunachotaka akamilishe mradi huu ili biashara zianze kufanyika na Halmashauri ianze kupata mapato,"amesema Kunenge.

Kwa upande wake Mhandisi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Brighton Kisheo amesema kuwa Halmashauri hiyo ilitengewa kiasi cha shilingi bilioni nane mwaka 2018-2019 kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo ambapo wafanyabiashara 253 watapata fursa za biashara na litahudumia watu zaidi 2,000 na unatarajiwa kukamilika Novemba mwaka huu.

Naye mwenyekiti wa Wamachinga Mkoa wa Pwani Filemon Maliga amesema kuwa wanaishukuru serikali kwa kuwapatia eneo jirani na Mall hiyo ili wafanye biashara zao na wanamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kulirasimisha kundi lao ambapo sasa wanatambulika na wanapata fursa mbalimbali zikiwemo za mikopo.

Miradi mingine aliyoitembelea mkuu huyo wa mkoa ni barabara, ujenzi wa madarasa ya sekondari kata ya Mkuza na maandalizi ya ujenzi wa kiwanda cha utengenezaji wa mitungi ya gesi ya kampuni ya Taifa Gas.


Mwisho.

Wednesday, October 18, 2023

SOKO LA KISASA KUJENGWA MLANDIZI BILIONI 7 KUTUMIKA

KATIKA kuhakikisha Mji wa Mlandizi unavutia Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha inatarajia kujenga soko kubwa na la kisasa kwa ajili ya wakazi wa mji wa Mlandizi ambalo litagharimu kiasi cha shilingi bilioni saba.

Hayo yamesemwa Mlandizi na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Michael Mwakamo wakati wa kuhitimisha kampeni ya Simika Bendera kwenye Jimbo hilo.

Mwakamo alisema kuwa eneo maarufu kama kwa Mama Salmini tayari limeshapatikana baada ya kununuliwa na mkandarasi wa ujenzi amepatikana na utaratibu unaanza kwa ajili ya ujenzi.

"Soko la sasa ni dogo lakini eneo tulilopata ni kubwa na litachukua wafanyabiashara wengi na litakuwa na huduma nyingi tofauti na la sasa ambalo hata sehemu ya magari kupaki hakuna,"amesema Mwakamo.

Amesema fedha hizo zimetengwa kwenye baheti ya mwaka wa fedha 2023/2024 na tayari bilioni mbili zimetolewa kwa ajili ya kuanza kazi na litaubadilisha Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlandizi.

Naye Mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu alisema kuwa chama kinataka viongozi waliopo kwenye madarakani wawe na mahusiano mazuri na wananchi.

Kwa upande wake katibu wa CCM Kibaha Vijijini Zainabu Mketo amesema kuwa hamasa ya Simika Bendera imeleta mafanikio kwani wamevuna wanachama wapya 3,500 na kupitia mabalozi wote lengo likiwa ni kuimarisha chama ndani ya chama.


Mwisho.

Sunday, October 15, 2023

MAOFISA TEHAMA WATAKIWA KUENDANA NA TEKNOLOJIA

MAOFISA TEHAMA nchini, wameaswa kwenda na wakati ,kupenda kujifunza kulingana na teknolojia inavyobadilika ili kujiongezea uzoefu na ujuzi.

Aidha wawe wabunifu ,wajitume ili kuacha alama na tija katika kada hiyo kwenye maeneo ya kazi

Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala mkoa wa Pwani Rashid Mchatta, wakati alipomwakilisha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, kufungua kikao kazi cha mwaka 2023 ,ambacho kimefanyika Kibaha Mkoani Pwani na kukutanisha maofisa hao kutoka mikoa mbalimbali nchini ili kujadili changamoto zinazokikabili kitengo Cha TEHAMA.

 "IT ina mambo mengi sana, inabadilika kama mtu wa Tehama hufanyi updating itakupa wakati mgumu, someni masomo ya ziada kuongeza uzoefu,mkoa wa Pwani ndio mwenyeji mwaka huu tumejipanga kuhakikisha tuliyoyajadili yanafanikiwa"anasema Mchatta.

Mchatta alieleza, kada ya TEHAMA imekua kwa kasi kubwa na kupelekea kuwa mhimili mkubwa katika utendaji kazi na Serikali na Taasisi nyingine binafsi kwenye mifumo mbalimbali ikiwemo ukusanyaji mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za mitaa ,mfumo wa kusimamia huduma za hospitali.

"Serikali - TAMISEMI imeipa kada hii umuhimu mkubwa kwa kuanzisha wizara rasmi inayoshughulikia TEHAMA ,hivyo tusimuangushe mh Rais"

Awali Melchiory Baltazary, Mkurugenzi Msaidizi-TEHAMA TAMISEMI alieleza kikao hicho ni kikao kazi ambacho kitafanyika siku mbili.




Mwisho

Saturday, October 14, 2023

LIONS CLUB YATOA MISAADA YA VIFAA VYA SHULE


KLABU ya Lions ya Jijini Dar es Salaam imetoa vifaa kwa Shule 15 za Msingi na Sekondari Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo zenye thamani ya zaidi ya milioni sita ili kukabiliana na uhaba wa vifaa kwenye shule hizo.

Hayo yalisemwa kwenye  shule ya msingi Ruvu Darajani kata ya Vigwaza na Rais wa zamani wa klabu hiyo Muntazir Bharwani wakati wa kukabidhi vifaa hivyo kwa shule ambapo ziliwakilishwa na walimu wakuu wa shule hizo.

Bharwani amesema kuwa klabu yao inajihusisha na kusaidia masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kwenye sekta za elimu, afya na maji na masuala mengine ya kimaendeleo.

"Tumetoa vifaa vikiwemo vitabu vya walimu kwa ajili ya kufundishia, madaftari pamoja na mipira kwa ajili ya kuwaweka wanafunzi kwenye utimamu wa akili,"amesema Bharwani.

Akipokea misaada hiyo ofisa elimu msingi na awali wa Halmashauri ya Chalinze Miriam Kihiyo ameishukuru klabu hiyo na kuomba iendelee kusaidia kwenye sekta hiyo.

Kihiyo amesema kuwa mahitaji kwenye sekta ya elimu ni kubwa kutokana na kuwa na wanafunzi wengi na kuomba wadau wengine waendelee kujitolea misaada mbalimbali.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Vigwaza Musa Gama amesema kuwa anashukuru kwa misaada hiyo ambayo itasaidia kupunguza sehemu ya baadhi ya changamoto.

Gama amesema kuwa msaada huo ni motisha kwa walimu na wanafunzi katika kuhakikisha elimu inaboreka na kuwataka wananchi wawasimamie watoto wao ili wapate elimu ipasavyo.

WATAKA JITIHADA ZIONGEZWE WATU KUKUA KUSOMA KUHESABU NA KUANDIKA

IMEELEZWA kuwa watu wanaojua kusoma kuandika na kuhesabu nchini kwa sasa ni asilimia 77.8 ikilinganishwa na mwaka 1980 ambapo watu hao ilikuwa ni asilimia 9.6.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Profesa Michael Ng'umbi Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Nchini wakati wa ufunguzi wa Kongamano la maadhimisho ya kitaifa ya juma la elimu ya watu wazima kitaifa.

Ng'umbi alisema kuwa mwaka 1980 Tanzania iliweza kufikia kiwango cha juu cha kufuta ujinga kwa watu wasiojua kuandika kuhesabu na kusoma na kufikia asilimia hiyo.

Akifungua mafunzo hayo kaimu mkurugenzi elimu msingi wizara ya elimu sayansi na teknolojia Josephat Luoga alisema kuwa mafunzo hayo yatawezesha kuamsha hamasa ya kutafakuri kuwa tunakwenda wapi katika utoaji elimu.

Luoga alisema kuwa mfumo wa elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi utaweza kubadilisha mtizamo juu ya uendeshaji na usimamizi na tathmini ili kuendana na dira ya maendeleo ya 2025 pamoja na mpango wa maendeleo endelevu 2030.

PROFESA MKENDA AFURAHISHWA TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA INAVYOBORESHA MFUMO HUO

WAZIRI wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha elimu ya watu wazima nchini.

Mkenda aliyasema hayo wakati wa kufunga Kongamano la maadhimisho ya kitaifa ya juma la elimu ya watu wazima kitaifa lililofanyika Wilayani Kibaha.

Alisema kuwa serikali itaendelea kujenga uwezo na watendaji kwenye Halmashauri kwenye mikoa zitoe kipaumbele kwa program zote za elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Elimu kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi Dk Charles Msonde alisema kuwa moja ya mkazo uliowekwa ni kuhakikisha wanafunzi wa darasa la kwanza wanajua kusoma kuandika na kuhesabu.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Profesa Caroline Nombo alisema kuwa jumla ya wanafunzi milioni 5.7 walidahiliwa kwenye elimu changamani kwenye vituo 405.

Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alisema kuwa baadhi ya changamoto katika utekelezaji wa baadhi ya program ni pamoja na walimu wa kujitolea kutokuwa na mafunzo ufinyu wa bajeti, upungufu wa vitendea kazi na kushindwa kulipa wa wezeshaji.


Mwisho.

MKUU WA MKOA WA PWANI KUNENGE ATAKA VIONGOZI WALIOHUSIKA UUZAJI VIWANJA ENEO LA MITAMBA WAKAMATWE

KUFUATIA viongozi 24 kujihisisha kuwatapeli watu na kuwauzia eneo la shamba la Mitamba mali ya Wizara ya mifugo na uvuvi Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametoa  siku 14  kukamatwa viongozi hao.

Aidha viongozi hao ni pamoja na mabalozi, wenyeviti wa mitaa, watendaji  walioshirikiana na madalali  waliohusika kuwauzia  wananchi viwanja katika eneo la shamba hilo lililopo Halmashauri ya Mji Kibaha.

Kunenge alitoa maagizo hayo wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya Pangani uliowahusisha watalaam kutoka Halmashauri ya Mji Kibaha na mkoa kwa ajili ya kutoa msimamo wa serikali kuhusu maamuzi ya eneo hilo ambalo limevamiwa na wananchi kwa ajili ya makazi.

Alisema orodha na majina ya viongozi hao na madalali  waliohusika kuwauzia kinyemela wananchi viwanja katika eneo hilo ambalo linamilikiwa na serikali na kwamba anayakabidhi kwa Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru pamoja na Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

Naye Mpimaji Ardhi Halmashauri ya Mji Kibaha Aron Shushu alisema kuwa kiwanja hicho kilipimwa upya kwa kuzingatia sheria namba 8 ya mipango miji na kwamba  mwaka 2021 kilifanyika kikao na wananchi hao kwa ajili ya kutoa katazo la kutovamia shamba hilo.

Shushu alisema kuwa jitihada za kuwakataza wazanchi hao ziliendelea huku baadhi wakionekana kuendelea na shughuli za ujenzi   na kukaidi na walipokea mapendekezo kutoa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Alisema kuwa kuhusu upimaji wa eneo hilo hekta 150 zilitolewa kwa ajili ya Matumizi ya Wakala wa Maabara ya Vetenari Tanzania (TVLA) hekta 188 kwa ajili ya matumizi ya Taasisi za  Umma, 486  uwekezaji wa viwanda na 200  makazi.