Thursday, November 23, 2023

MAOFISA KILIMO PWANI WAPEWA VISHKWAMBI KUBORESHA UTENDAJI KAZI

MKOA wa Pwani umewakabidhi Vishkwambi 345 kwa Maofisa Kilimo wa Wilaya za mkoa huo ili kuleta tija na kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge wakati akikabidhi vifaa hivyo ambavyo vimetolewa na Serikali.

Kunenge amesema kuwa matumizi mengine ni kusajili wakulima ambao bado hawajaingizwa kwenye mfumo na kuboresha taarifa za wale waliosajiliwa ili wahudumiwe kwa idadi na kujua mahitaji yao ya pembejeo.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala wa mkoa wa Pwani Shangwe Twamala amesema wanaishukuru Wizara ya Kilimo kwa kuwapatia vifaa hivyo.

Naye Ofisa Kilimo wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Joseph Njau amesema kuwa vifaa hivyo vitawawezesha kutekeleza majukumu yao na kuongeza uzalishaji na kuleta tija kwa wakulima kwenye maeneo yao.

No comments:

Post a Comment