Monday, December 4, 2023

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI YAWATAKA WANAWAKE KUMUENZI BIBI TITI MOHAMED KWA KULETA MAENDELEO

WANAWAKE nchini wametakiwa kupambana kuiletea nchi maendeleo kama alivyofanya Bibi Titi Mohamed ambaye aliasidiana na Mwasisi wa Taifa Julius Kambarage Nyerere kuleta uhuru wa Tanzania.

Aidha amewataka kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuwapatia fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo. 

Hayo yamesemwa Mlandizi Wilayani Kibaha na Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani Omary Punzi wakati wa mafunzo kwa wanawake ya Ijue Kesho yako.

Punzi amesema kuwa katika kupigania nchi kupata uhuru alishirikiana na Bibi Titi Mohamed hadi Uhuru ukapatikana hivyo wanawake nao wawe mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya nchi.

"Nyerere alijenga misingi ya maendeleo na aliona umuhimu wa mwanamke na ndiyo sababu alishirikiana na Bibi Titi katika mapambano ya Uhuru hivyo nanyi msikae nyuma lazima mpambane kuleta maendeleo ya nchi,"amesema Punzi.

No comments:

Post a Comment