Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Lutumo amesema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 28 majira ya saa 11:45 alfajiri eneo la Mbwewe Chalinze Wilayani Bagamoyo.
Amesema kuwa watu hao waliofariki walikuwa kwenye gari lenye namba za usajili T 395 DWE aina ya Alphard likiendeshwa na Mohamed Athuman (40) mkazi wa Jijini Dar es Salaam.
"Gari hilo lilikuwa likuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Kabuku mkoani Tanga ambapo liligonga kwa nyuma gari lenye namba za usajili T 300 CLE na tela namba T 399 AUP aina ya FAW lililokuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara,"amesema Lutumo.
Aidha amewataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni Zakia Mohamed (36) ambaye ni mwalimu, Goletha (23) msichana wa kazi na Nadim Nurdin miezi (8) wote wakazi wa Kabuku.
Amewataja majeruhi kuwa ni dereva wa gari hilo Athuman na Alice Sangule (8) ambaye ni mwanafunzi na mkazi wa Kabuku.
"Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari lililosimama Alphonce Bosco (55) Mkazi wa Mabawa Tanga, kuegesha gari pembezoni mwa barabara bila ya kuweka alama za tahadhari kwa watumiaji wengine wa barabara,"alisema Lutumo.
Aliongeza kuwa miili ya marehemu na majeruhi walipelekwa Hospitali ya Mkata Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga kwa hifadhi na matibabu.
"Jeshi la Polisi linatoa rai kwa madereva kuendelea kuchukua tahadhari na kuheshimu sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazosababishwa na uzembe katika kipindi hichi cha sikukuu kwani watu wengi wanasafiri kuelekea mikoa mbalimbali kwa ajili ya kusherehekea na familia zao,"amesema Lutumo.
ReplyReply allForward |
No comments:
Post a Comment