Na John Gagarini, Kibaha
SERIKALI imelipa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) miezi mitatu kuhakikisha linapata kiasi cha dola za Kimarekani Milioni 2.1 kwa ajili ya kiwanda cha Viuadudu vya Kuua Viluwiluwi vya Mmbu wanaoeneza Ugonjwa wa Malaria Tanzania Biotech Product Ltd kilichopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Aidha alishangazwa na shirika hilo kwa kuajiri wafanyakazi 143 Julai mwaka 2015 ambao wanalipwa mishahara pasipo kuzalisha kitu chochote kwani wanapokea mishahara ya bure jambo ambalo alisema kuwa halipendezi.
Agizo hilo limetolewa jana mjini Kibaha na katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dk Adelhelm Meru alipotembelea kiwanda hicho ambacho kilizinduliwa Julai 2015 na Rais mstaafu Dk Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu wa Ethiopia.
Dk Meru alitoa agizo hilo kutokana na kutoridhishwa na maombi ya NDC kuomba kiasi hicho serikalini kutoka kwa Godwill Wanga Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika hilo kwa lengo la kufanya majaribio pamoja na kuanza uzalishaji.
“Serikali haiwezi kutoa kiasi hicho cha fedha ambazo zingetumika kwa ajili ya huduma za jamii hivyo fanyeni kila njia kwa kukopa kwa kufanya nini ombeni hata benki ya uwekezaji nchini TIB ili mhakikishe mnapata fedha hizo na majaribio yanaanza ili uzalishaji uanze tumechelewa kwa kipindi cha miaka minne,” alisema Dk Meru.
Alisema kuwa inatosha kwani serikali ililipa gharama zote za ujenzi wa kiwanda hicho dola milioni 22 na kilitakiwa kianze kazi tangu mwaka 2012 ikasogezwa hadi Julai 2015 lakini hadi sasa ni miezi sita imepita lakini uzalishaji bado.
“hatuwezi kuwa kioja tafuteni fedha hizo dola milioni 1 kwa ajili ya majaribio na dola milioni 1.2 kwa ajili ya mtaji kwani malengo ya serikali ilikuwa na lengo kiwanda kianze kazi kwa muda uliopangwa ili kiweze kukabiliana na ugonjwa wa Malaria na ziada ya dawa kuuzwa nje ya nchi hivyo kuweza kufikia malengo yaliyowekwa,” alisema Dk Meru.
“Nataka ifikapo Mei Mosi mwaka huu mimi nije na Waziri wangu ili tuone uzalishaji unaanza mara moja kwani moja ya sera za nchi hasa katika awamu hii ya tano ni kujenga uchumi kupitia viwanda na kuwa nchi yenye uchumi wa kati ili kuleta maendeleo ya wananchi pia iko kwenye dira ya mpango wa maendeleo wa miaka mitano,” alisema Dk Meru.
Awali akielezea juu ya maendeleo ya kiwanda hicho Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NDC Wanga alisema kuwa baadhi ya vifaa kwenye mashine ziliathiriwa na umeme kutokana na na kukatika katika hali ambayo ilisababisha uzalishaji ushindwe kuanza.
Wanga alisema kuwa kutokana na ucheleweshaji huo wa kuanza kufanya kazi ilibidi wataalamu kutoka nchi ya Cuba inakotoka teknolojia hiyo Labio Farm kudai gharama zaidi za ujenzi hivyo kudai fidia.
“Kiwanda hichi kinahitaji msaada hata kwa mkopo kiasi cha dola milioni 2.1 ili kuweza kukamilisha hatua zilizobakia kwani wataalamu wetu wameishiwa mtaji baada ya muda kuongezeka na kutokana na matatizo ya kuharibika vifaa vya mashine za kiwanda hichi,” alisema Wanga.
Alisema kuwa teknolojia hiyo ni mpya na mara uzalishaji utakapoanza itasaidia kukabiliana na ugonjwa wa Malaria kwani dawa hiyo ina uwezo wa kuua mazalia ya mbu na baadaye kitakuwa na uwezo wa kuzalisha bidhaa nyingine ikiwa ni pamoja na mbolea na madawa mbalimbali.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment