Na John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI ya Mji wa Kibaha imetoa muda wa miezi sita kwa
watu walionunua viwanja kwenye kitovu cha mji kujenga kama sheria za ujenzi
vinavyoonyesha na kwa sasa hawatakuwa tena na majadiliano kwa watakaoshindwa
kujenga watanyanganywa viuwanja hivyo.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hatua ambazo
watachukua kwa watu walioshndwa kuendeleza viwanja hivyo tangu walipovinunua
mwaka 2010 ofisa ardhi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Edward Mbala alisema
kuwa watu hao walipew ahadi mwaka 2015 wawe wamejenga.
Mbala alisema kuwa licha ya kupewa muda wote huo lakini watu
hao wameshindwa kujenga hadi sasa licha ya kuwa na maongezi ya mara kwa mara
kati ya Halmashauri na wawekezaji hao mara kwa mara lakini hadi sasa
wameshindwa kuyaendeleza maeneo hayo.
“Mara ya mwisho tuliwaita Aprili mwaka jana lakini walisema
kuwa tatizo kubwa lililowafanya washindwe kuanza ujenzi kwenye viwanja hivyo ni
hadi pale Halmashauri itakapokuwa imefanya ujenzi wa Stendi na Soko jambao
ambalo tuliwaambia kuwa wao waendelee na ujenzi huku sisi tukitafuta wabia kwa
ajili ya ujenzi wa vitu hivyo,” alisema Mbala.
Alisema tayari wameshapata benki ambayo itawakopesha kwa
ajili ya ujenzi wa soko pamoja na stendi ambapo zaidi ya bilioni 20
zinatarajiwa kutumika kujenga miuondombinu hiyo hivyo wale walionunua viwanja
waanze ujenzi.
“Tumesha waambia wayaendeleze maeneo hayo na tayari tumewapa
miezi sita kuhakikisha wanakamilisha
ujenzi huo na endapo watashindwa kujenga sheria itachukua mkondo wake kwa
kuwanyanganya na kuwapa wengine,” alisema Mbala.
Aidha alisema kuwa tayari wameshatoa matangazo sehemu
mbalimbali na kwa wamiliki hao ili waendeleze maeneo yao ambayo ndiyo
yanaonyesha sura ya mji wa Kibaha lakini
kwa sasa maeneo hayo bado ni vichaka.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment