Na John Gagarini, Kibaha
Marufuku hiyo inakuja baada ya tukio la kufa vijana hao ambao
ni Alex Kapungu (18), Godfrey Ernest huku Omary Mohamed akijeruhiwa kwenye
tukio lililotokea januari 10 mwaka huu majira ya saa 2:50 usiku kwenye mtaa
huo, baada ya vijana hao kutuhumiwa kuwa ni wezi baada ya kuibuka kwa vurugu
zilizosababisha baadhi ya vijana waliokuwa kwenye mziko huo kufanya uporaji
kwenye maduka.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana diwani wa kata
ya Pangani Agustino Mdachi alisema kuwa kamati ya ulinzi na usalama ilifikia
hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa muziki huo umekuwa chanzo cha vurugu ambazo
zimesababisha vifo pamoja na wizi kwenye maeneo unakopigwa muziki huo.
Mdachi alisema kuwa hilo ni tukio la pili la mauaji ambayo
yametokeo kwenye muzikio huo ambao unatumiwa sana na waendesha pikipiki ambapo
imebainika kuwa waendesha bodaboda hao hasa wale wanaofanya biashara nyakati za
usiku maarufu kama Mapopo wengi wao ni wezi na hujificha kwenye mgongo wa kazi
hiyo.
“Uchunguzi umebaini kuwa wengi wa wa mapopo hao hujihusisha
na vitendo vya wizi kwani wakati muziki unaendelea huanzisha vurugu na na
kuwaibia watu ambapo wengi wao huwa na mapanga wanapokwenda kwenye muziki huo
ambao unatamba kwa sasa,” alisema Mdachi.
Alisema kuwa kutokana na kubaini kuwa muziki huo umekuwa
ukichangia vitendo vya uhalifu katika kata ya Pangani waliamua kwa pamoja
kuzuia upigwaji wa muziki huo kwa kipindi kisichojulikana ili kuepukana na
vitendo hivyo vya uhalifu pamoja na mauaji.
“Kwa ujumla Kigodoro mara nyingi hakiishi salama kwani mara
nyingi vurugu zimekuwa zikitokea na vijana wanauana kutokana na muziki huu
hivyo tumeamua kusitisha muziki huu ili kupunguza wimbi hili la uhalifu na
mauaji,” alisema Mdachi.
Aidha alisema kuwa kwa sasa wameamua kufanya doria kwa muda
wote kwa kushirikiana na vyombo vya dola ili kukabiliana na matukio hayo ya
kihalifu ambayo mengi yanafanywa na waendesha pikipiki.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment