Na John Gagarini, Kibaha KATIKA kukabiliana na changamoto mbalimbali za utoaji huduma
kwa wananchi Halmashauri ya Mji wa Kibaha imesema kuwa itatatua kero hizo
kadiri ya uwezo wa fedha za miradi ya maenedeleo zinavyopatikana.
Hayo yalisemwa na mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha
Gladys Dyamvunye alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na
kusema kuwa kuna changamoto za utoaji huduma kwani kila mwananchi anataka
maendeleo.
Dyamvunye alisema kuwa changamoto ni nyingi kwani ili kuondoa
kero lazima huduma ziboreke lakini kutokana na mahitaji ya huduma kuongezeka
kutokana na ongezeko la idadi ya watu kila wakati.
“Kadiri maendeleo yanavyokuja mahitaji ya huduma nayo yanaongezeka
hivyo kuonekana kama huduma ni kidogo lakini tutaendelea kutoa huduma kadiri ya
uwezo wetu ili kuwaondolea changamoto wananchi,” alisema Dyamvunye.
Alisema kuwa halmashuri itahakikisha huduma zinazotolewa kwa
wananchi zinaboreshwa ili kuondoa malalamiko yasiyo ya msingi kwani lengo ni
kuboresha utoaji huduma ambayo ndiyo kazi ya Halmashauri.
“Bajeti ya fedha inaweza kuwa ni tatizo hivyo baadhi ya
huduma zinaonekana kama hazitolewi kiufasaha lakini si lengo la Halmashauri
yetu kwani matazamio yetu ni huduma bora kwa wananchi ili waipende serikali yao,”
alisema Dyamvunye.
Aliwataka wananchi kushirikiana na halmashauri yao ili iweze
kutoa huduma ambazo zitakabili changamoto zilizopo kwa wananchi na kusema
wataendelea kuhudumia wananchi kadiri ya uwezo wao.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment