Na John Gagarini, Kibaha
Hayo yalisemwa hivi
karibuni mjini Kibaha na Waziri wa Ardhi na Makazi Wiliam Lukuvi wakati
alipofanya zaiara ya siku moja wilayani Kibaha kuangalia changamoto
zinazoikabili idara ya ardhi kwenye mkoa huo.
Lukuvi alisema kuwa utoaji hati za kumiliki ardhi kwa haraka
itasaidia kupunguza migogoro ambayo imejitokeza kutokana na kuchelewa kutolewa
kwa hati hizo ambapo watu wamekuwa wakivamia maeneo yaliyowazi.
“Upatikanaji wa hati unasaidia kuepusha migogoro pia uvamizi
kwani kutokana na uchelewaji wa kupatikana hati kunasababisha mtu kushindwa
kumiliki kihalali eneo lake hivyo tunataka tuondokane na ucheleweshaji huo,”
alisema Lukuvi.
Alisema kuwa majaribio hayo yataanza kwenye mikoa ya Dar es
Salaam, Pwani na Morogoro kupitia mfumo wa Kieletroniki ambapo mfumo huo endapo
utafanikiwa utasamabazwa nchi nzima na kuweza kufikia malengo ya kupima ardhi
ya nchi nzima.
“Utashangaa mfumo huu wa sasa kuna baadhi ya watu wamekuwa
kwenye mchakato wa kupatiwa hati kwa muda mrefu tangu mwaka 2013 lakini
wamekuwa wakitumia ofa pekee jambo ambalo hatulitaki tena,” alisema Lukuvi.
Aidha alisema ametoa hadi mwisho wa mwezi huu Halmashauri
kuhakikisha unawapatia hati watu wote walioomba hati kwani ofa hazitatambuliwa
tena hivyo wanatakiwa kufanikisha zoezi hilo ili kuondoa kero kwa wananchi.
“Tunataka tuondokane na kero ya kucheleweshwa kupatikana kwa
hati kwani mbali ya maeneo kuvamiwa na changamoto nyingine pia watu wanaweza
kuzitumia hati zao katika kukopa kwenye mabenki au taasisi za kifedha kwa ajili ya shughuli zao za maenedeleo,” alisema
Lukuvi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment