Na John Gagarini, Kibaha
MKULIMA wa Mtaa wa Sagare wilayani Kibaha mkoani Pwani Hassan
Omary ameokota bomu la kutupwa kwa mkono ambalo lilisahaulika wakati wa Operesheni
Tokomeza iliyofanyika nchini Julai mwaka 2015.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha kamanda
wa polisi mkoani Pwani Bonventura Mushongi alisema bomu hilo lilisahaulika
wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo la kukamata wahalifu mbalimbali waliokuwa
wakiiba Maliasili za nchi.
Mushongi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 31 mwaka
2015 majira ya saa 5 asubuhi wakati mke wa Omary alipokuwa akilima aligonga
kitu kigumu cha chuma na alipokitoa aliona kitu kama bomu na kumwita mumewe
aliye waita watu wakiwemo viongozi wa mtaa huo.
“Baada ya kuona hivyo Omary alitoa taarifa polisi na kusema
kuwa wameona bomu ndipo polisi walipofika na kubaini kuwa ni bomu la kutupwa
kwa mkono ambalo fuse yake ili haribika,” alisema Mushongi.
“Halikuweza kulipuka lakini endapo lingepata joto kali mfano
joto la moto lingeweza kulipuka lakini hata hivyo tumeshukuru Mungu kuwa
halikuweza kulipuka kwa muda wote huo kwnai endapo lingelipuka lingeweza kuleta
madhara,” alisema Mushongi.
Alisema kuwa baadaye ilibainika kuwa inawezekana bomu hilo la
kutupwa kwa mkono liliachwa kwa bahati mbaya wakati wa Operesheni Tokomeza iliyofanyika
Julai mwaka jana.
“Kwa kushirikiana na jeshi letu tutalipelekwa kwa wataalamu
wa mabomu ambao ni Jeshi la wananchi (JWTZ) kwa ajili ya kujua zaidi kuhusiana
na bomu hilo ikiwa ni pamoja na kuliharibu ili lisiweze kuleta madhara,”
alisema Mushongi.
Awali mwenyekiti wa mtaa wa Sagale Bernego alisema kuwa mama
huyo alikuwa akisafisha shamba kwenye eneo la Omary ambalo limekuwa likichimbwa
vitu vilivyoachwa zamani na watawala wa Kijerumani na Kiarabu maarufu kama
Tunu.
Bernego alisema kuwa machimbo hayo ya Tunu yalikuwa
yakifanywa na mmiliki huyo ambapo eneo hilo lilizua utata miaka michache
iliyopita kwani kumekuwa na mambo ya miujiza yamekuwa yakitokea kwenye machimbo
hayo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment