Na John Gagarini, Kibaha
KUFUATIA baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Mwanalugali wilayani
Kibaha mkoani Pwani kulalamika mbele ya Waziri wa Ardhi na Makazi Wiliam Lukuvi
juu ya kushindwa kulipwa fidia ya viwanja vyao vilivyochukuliwa na Halmashauri
kwa zaidi ya miaka 18 iliyopita wakazi hao sasa watalipwa ifikapo Machi mwaka
huu.
Ahadi hiyo ilitolewa na Halmashauri mbele ya Waziri Lukuvi
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Bwawani Maili Moja
wilayani hapa kujua kero mbalimbali zitokanazo na masuala ya ardhi na kusema
kuwa ofisa ardhi wa Mji huo endapo atashindwa kutekeleza hilo basi atakuwa
amejifukuzisha kazi mwenyewe.
Akitoa ahadi hiyo ofisa ardhi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha
Edward Mbala baada ya kubanwa na wananchi hao ambao walisema kuwa wamekuwa
wakizungushwa kwa kipindi hicho huku wakiwa hawajui hatma yao.
Moja ya wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Merry Yohana
alisema kuwa maeneo yao yalichukuliwa na Halmashauri kipindi hicho na kuahidiwa
kuwa wangelipwa fidia na wengine wangepewa viwanja katika maeneo hayo lakini
hakuna utekelezaji wowote uliofanyika licha ya kuwa viwanja hivyo tayari
walishaviuza kwa watu wengine.
“Tunapata shida sana kwani walichukua maeneo yote licha ya
kuwa ni jambo zuri la maendeleo lakini kwa kipindi cha miaka 18 tumekuw
atukifuatilia bila ya mafanikio kwani tunazungushwa tu na hakuna majibu ya
uhakika kuwa ni lini tutalipwa kwenye
eneo la Kitalu E,” alisemaYohana.
Kufuatia malalamiko hayo Waziri Lukuvi alimwita ofisa ardhi
ili atoe majibu ambapo alisema kuwa ni kweli watu hao wamekuwa wakidai kwa
kipindi hicho lakini Hlamashauri iko kwenye utaratibu wa kuwalipa majibu ambayo
hayakumridhisha waziri.
“Mkuu ni kweli kuna watu wanadai fidia na wengine wanadai
viwanja na huu ulikuwa ni mradi lakini tuko kwenye utaratibu wa kuwalipa na
tutawalipa wakati wowote mara taratibu zitakapokamilika kwani tunahangaika
kuhakikisha madai yao yanapata majibu,” alisema Mbala.
Hata hivyo waziri alimwambia atoe ahadi kuwa ni lini watakuwa
wamekamilisha zoezi hilo ambapo alisema kuwa baada ya miezi miwili kutoka sasa
fedha hizo zitakuwa zimepatikana kiasi cha shilingi bilioni 1.4 pamoja na
kuwapatia viwanja wengine.
Kwa upande wake Waziri Lukuvi alisema kuwa haipendezi
wananchi kukaa muda mrefu bila ya kulipwa fidia ya maeneo yao ambayo
yalichukuliwa na Halmashauri kwani kuchelewesha kulipa kunasababisha migogoro
isiyo ya lazima.
“Wananchi ofisa ardhi ameahidi hapa mbele yangu na ninyi
hivyo msiwe na wasiwasi Bw Ardhi kwa kuwa umeahidi mwenywe muda mtkaowalipa
hawa wananchi endapo utashindwa utakuwa umejifukuzisha kazi mwenyewe,” alisema
Lukuvi.
Lukuvi aliwataka wananchi hao kukubali muda huo wa miezi
miwili kwani walishakaa muda wa miaka 18 hivyo atahakiki wanaodai fidia na wale
wanaodai viwanja kwani muda umekuwa mrefu sana na watu wanataka wafanye
maendeleo yao.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment