Na
John Gagarini, Bagamoyo
VIONGOZI
wa serikali za mitaa na vijiji wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani waliochaguliwa hivi
karibuni wametakiwa kusoma mapato na matumizi ili kuepuka kuenguliwa kwenye
nafasi zao kama baadhi yao waliopita kukataliwa na wananchi.
Moja
ya changamoto zilizosababisha viongozi hao waliopita baadhi yao walienguliwa na
wananchi huku wengine wakishindwa kurudishwa kwenye kura za kuteuliwa kuwani
uongozi kwenye uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Hayo
yalisemwa Bagamoyo na katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kombo Kamoto alipozungumza
na wananchi wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo
Ridhiwani Kikwete kwenye vijiji vya kata
za Kibindu, Mbwewe, Mdaula, Bwiringu, Fukayosi, Miono na Kiwangwa.
Kamote alisema kuwa viongozi hao waliochaguliwa na wananchi hasa wale wanaotoka
chama hicho kwani hawana budi kuwatumikia wananchi ipasavyo kwa lengo la
kuwatatulia changamoto ambazo zinawakabili katika nyanja mbalimbali kwenye
huduma za kijamii.
“Mmechaguliwa
na wananchi kwa heshima ya chama chetu, hususani kusoma mapato na matumizi hivyo
niwasihi mchape kazi kama sheria na taratibu zinavyowaongoza, sitopenda kusikia
wananchi wakilalamikia kuhusu utendaji wenu, mtambue mwaka huu mmeapishwa na
mahakimu tofauti na miaka yote, hivyo yeyote atayekiuka kiapo hicho ataondolewa
kwenye nafasi yake,” alisema Kamote.
Alisema
kuwa viongozi hao watatakiwa kuitisha mikutano na kusoma mapato na matumizi kwa
wananchi ili waweze kujua yanayofanyika kwenye maeneo yao.
Viongozi
hao pia waliaswa kutokuwa madalali wa kuuza ardhi kiholela na kuwakandamiza
wananchi ambao wakati mwingine hawajui haki zao za msingi.
“Baadhi
waliondolewa kutokana na kushindwa kuitisha mikutano ikiwa ni pamoja na kushindwa
kusoma mapato na matumizi hali iliyowafanya waondolewa madarakani au kushindwa
kwenye uteuzi wa kuwania nafasi hizo, alisema Kamote.
Aidha
alisema kuwa inashangaza kuona baadhi ya viongozi wanakuwa vinara wa kuuza
maeneo na kama yupo kiongozi aliyekuwa anafanya hivyo wanapaswa kuacha na kuwa waadilifu
ili kulinda nafasi walizopata.
“Viongozi
huu si muda wa kuanza majigambo ama kujivunia nafasi mlizoshika bali mnatakiwa kutimiza wajibu wenu kwa
kusimamia ilani ya chama cha mapinduzi ili kuleta maendeleo kwa wananchi,”
alisema Kamote.
Kwa
upande wake Ridhiwani Kikwete aliwaomba viongozi hao kufanya kazi kwa bidii ili
chama kiendelee kuaminika na kushika dola .
“Fanyeni
kazi bila kubagua watu ,watumikieni pasipo kujali itikadi za kisiasa na hiyo
ndio sifa pekee ya kiongozi wa sasa asiyejali udini,ukabila wala chama alichopo,”alisema
Ridhiwani.
Ridhiwani
alisema kuwa yeye akiwa mbunge ataendelea kuwatumika ipasavyo katika kuwaondolea
changamoto zinazowakabili.
mwisho.
Na
John Gagarini,Chalinze
KILIO
cha baadhi ya wananchi wa Jimbo la Chalinze kukosa umeme huenda kikaisha baada
ya kuhakikishiwa kuwa watapata huduma hiyo kuanzia m,waka huu kupitia miradi ya
umeme vijijini kupitia wakala wa umeme Vijijini (REA).
Changamoto
hiyo itapungua kwenye maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo katika vijiji ambavyo
vipo kwenye awamu ya awamu ya tatu inayotarajiwa kuanza mwezi Juni mwaka huu
kupitia miradi hiyo ya REA.
Akiwahutubia
wananchi wa vijiji vya Kibindu, Mbwewe, Mdaula, Bwilingu, Fukayosi, Kiwangwa na
Chalinze mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa serikali ya
CCM imejipanga kuikabilia changamoto hiyo.
“Kila
maeneo niliyopita nimekutana na malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya kukosa umeme wakati
vijiji vingine vya kata hizo vikiwa vimepata umeme na kuhoji huku wao wakiona
kwa macho umeme umepita juu na kwenda maeneo jirani,” alisema Ridhiwani.
Ridhiwani
alise kuwa anatambua umuhimu wa umeme hivyo amekuwa akifanya jitihada za
kufuatilia na ndio maana amelazimika kufuatana na meneja wa miradi ya umemem
mkoani Pwani Leo Mwakatobe ambaye anatolea ufafanuzi suala hilo.
“Mfano
eneo la Kiwangwa halikuwepo katika umeme unaosambazwa na REA lakini baada ya
kufanya juhudi hizo fedha zimepatikana hivyo utakuwa wa REA ambapo tanesco
imetoa sh.milioni 420 na REA sh.milioni 800,” alisema Ridhiwani.
Aidha
alisema kuwa fedha hizo tayari ziko na kazi ya kuanza kusambaza umeme itaanza
wakati wowote, kwani anajua umuhimu wa umeme lakini wananchi na kuwaomba
wananchi wafahamu juhudi za serikali.
Kwa
upande wake mhandisi wa Tanesco mkoa wa
Pwani, Mhandisi Leo Mwakatobe, alisema wanaendelea kumalizia utekelezaji wa
awamu ya pili wa mradi wa REA na kazi iliyobaki ni mkandarasi kuanza kazi
wakati wowote kuanzia mwezi huu.
Mwakatobe
fedha kwa ajili ya mradi wa kusambaza umeme zimepatikana, hivyo wananchi wenye
kuhitaji waanze kuchukua fomu.kinachotakiwa wawe na picha mbili na kitambulisho
cha aina yoyote.
Mwisho