Tuesday, January 13, 2026

BINGWA

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

Monday, January 12, 2026

BAGAMOYO SUGAR MABINGWA DARAJA LA TATU MKOA WA PWANI

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

BAGAMOYO SUGAR YATWAA UBINGWA MKOA WA PWANI




TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

BARBERIAN YAICHAPA TMA

TIMU ya Soka ya Barberian imefanikiwa kuifunga timu ya TMA ya Arusha kwa magoli 2-1 kwenye mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza.

Mchezo huo uliokuwa mkali umefanyika kwenye uwanja wa Filbert Bayi uliopo Mkuza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Akizungumzia juu ya mchezo huo mwalimu wa timu ya Barberian Julio Elieza amesema kuwa waliweka mpango mzuri ambao ulifuatwa na wachezaji wake hadi kuibuka na ushindi licha ya kutanguliwa na wapinzani.

Kwa upande wake nahodha wa Barberian Kasim Haruna amesema ushindi wao ulitokana na kufuata maelekezo ya mwalimu wao. 

Mwalimu wa TMA Tiko Tiko alikiri kuzidiwa na wapinzani wao na kujikuta wakiambulia kipigo hicho.

Naye nahodha wa timu hiyo Fadhil Mahimbo amesema licha ya kuongoza walicheza chini na kuwapa nafasi wapinzani wao kurudi na kupata ushindi.

Timu ya Barberian ambayo inatumia uwanja huo wa Filbert Bayi inatarajiwa kucheza tena Januari 17 kwenye uwanja huo dhidi ya timu ya Songea United ambapo wameahidi kuendeleza wimbi la ushindi.


Tuesday, January 6, 2026

KIDULI FC YAJIPANGA KUPINDUA MATOKEO ILI KUTWAA UBINGWA WA MKOA WA PWANI

TIMU ya Soka ya Kiduli Fc ya Kibaha licha ya kupoteza mchezo wa fainali ya kwanza dhidi ya Bagamoyo Sugar ya Bagamoyo kwa 1-0 imejipanga kupindua matokeo ili kutwaa ubingwa wa mkoa wa Pwani.

Kiduli inatarajia kucheza mchezo wa marudiano Januari 12 kwenye uwanja wa Mwendapole na mshindi wa jumla ndiye atakayekuwa bingwa wa ligi daraja la Tatu mkoa wa Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa timu hiyo Ally Masimike amesema wamepoteza mchezo huo kwa bahati mbaya.

Masimike amesema kuwa watarudi kwenye uwanja wa mazoezi na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mchezo wao wa kwanza.

"Lengo letu ni kupambana na kuhakikisha tunashinda ili kuwa mabingwa na kuuwakilisha Mkoa wetu kwenye michuano ya Mabingwa wa Mikoa,"amesema Masimike.

Bagamoyo Sugar iliifunga Kiduli Fc kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa fainali ya kwanza kwenye uwanja wa Mwendapole Kibaha huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa kwenye uwanja huo huo ikiwa ni fainali ya pili ili kupata bingwa wa Mkoa.

Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Nasoro Mbilinyi amesema kuwa ligi hiyo ilikuwa ni kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20.


Mbilinyi amewataka wadau wa michezo kujitokeza kwa wingi kwenye fainali hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza.


Bingwa wa ligi hiyo atapata kombe na atawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya ligi ya Mabingwa wa mikoa.

PWANI YAMUUNGA MKONO RAIS KUTOA AJIRA KWA WANANCHI

KONGANI ya viwanda ya Gaini Company Limited iliyopo Kata ya Kikongo Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajiwa uzalisha na kutoa ajira 1,500 ifikapo Machi mwaka huu itakapoanza uzalishaji.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alipotembekea Kongani hiyo ambapo uwekezaji huo unaendana kikamilifu na mkakati wa Serikali wa kukuza uchumi wa viwanda pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa wananchi, hususani vijana.

Kunenge amesema kuwa Mkoa unaendelea kutekeleza vipaumbele vya Serikali kwa vitendo hususani katika eneo la uzalishaji wa ajira kwa vijana ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.

"Hatua hii inayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Pwani na kuongeza mapato ya Taifa kwa ujumla huku Mkoa ukiendelea kushirikiana na taasisi wezeshi zikiwemo TANESCO, DAWASA na TANROADS ili kuhakikisha hakuna urasimu wowote katika utekelezaji wa masuala ya uwekezaji,"amesema Kunenge.

Amesema kuwa ushirikiano na taasisi hizo ni kuwezesha upatikanaji wa mahitaji muhimu ikiwemo nishati ya umeme, maji pamoja na miundombinu ya barabara na kuwa mradi wa bomba la gesi kutoka Kinyerezi hadi Chalinze tayari umefanyiwa upembuzi yakinifu wa bilioni 2.3 na TPDC jambo litakaloongeza ufanisi wa upatikanaji wa nishati kwa viwanda mkoani humo.

Naye Meneja wa Mradi katika Kongani hiyo QS Bradley Cuthbert Muro amesema kuwa ujenzi wa viwanda viwili umefikia hatua za mwisho ambapo kiwanda cha chuma kimefikia asilimia 85 ya ujenzi huku kiwanda cha cubes kikifikia asilimia 95.

Muro amesema kuwa Kongani hiyo itakuwa na viwanda mbalimbali ikiwemo heavy duty industry, medium industry na light duty industry vikiwemo viwanda vya uzalishaji wa Nondo, Mabati, Steel Pipes, Hallow Sections (RHS) Squqre, Hallow Sections (SHS) Circular, Hallow Sections (CHS) Flat bars pamoja na Misumari.

mwisho

Saturday, December 27, 2025

VIJANA WATAKIWA KULINDA NA KUTUNZA AMANI YA NCHI

MWANADIPLOMASIA Omary Punzi amewataka Vijana kulinda na kutunza amani umoja uzalendo na mshikamano katika nyakati zote ili kuleta Maendeleo ya Taifa.

Punzi ameyasema hayo katika Bonanza la Michezo kwa Vijana liliratibiwa na Kamati ya Vijana Wazalendo Bonanza lililofanyika kwenye viwanja Soko la Ndizi vya Mabibo (Las Vegas) Jijini Dar es Salaam

Punzi ambaye pia ratibu wa Makongamano amesema kuwa lengo la Bonanza hilo ni kuhimiza amani na utulivu nchini. 

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika Bonanza hilo Mwenyekiti wa Mtaa wa Jitegemee  Abdallah Kilema aliwaomba vijana wapende michezo na kuwakumbusha michezo ni Ajira Upendo na Afya hivyo wanamichezo wanawajibu wa kutunza amani ya Taifa.

Naye mratibu kutoka mtandao wa YAS Neema aliwaomba vijana wajitokeze kwa wingi katika fursa mbalimbali za kimaendeleo na wao kama Taasisi wataendelea kudhamini mashindano mbalimbali.

Aidha Gervas Pai alishukuru kwa maandalizi mazuri na vijana kuwa na uwezo mkubwa na kuomba walinde Amani, Umoja na Mshikamano wa Taifa na wajitokeze kwa wingi kushiriki michezo.

Kocha wa Timu ya 7 lite Zayd Rashid aliwaomba wadau wa michezo waendelee kuongeza nguvu katika kuwatafutia vijana vifaa vya michezo ambavyo ni kero kubwa na kumshukuru muaandaji wa Bonanza hilo. 

Naye mchezaji Isack Rashid mchezaji bora wa mashindano hayo anesema kuwa ndoto yake ni kuwa mchezaji mkubwa hapa Tanzania ili kuweza kusaidia nchi yake 

Kwenye Bonanza hilo michezo ya vijana chini ya miaka15 kati ya Las Vegas na 7 lite mshindi ni 7 lite 4-0 mchezo wa pili ilikuwa kati ya Las Vegas na 7 lite ambapo Las Vegas imeshinda magoli 3-2

Mshindi wa kwanza alipatiwa mipira 5 na mshindi wa pili mipira 2 kwa upande wa mchezaji bora na goli kipabora kila mmoja aliibuka na shilingi 5,000.Bonanza hilo likishirikisha timu nne za Las Vegas na 7 lite miaka 15 na Las Vegas na 7 lite chini ya miaka 20.