Monday, January 12, 2026

BARBERIAN YAICHAPA TMA

TIMU ya Soka ya Barberian imefanikiwa kuifunga timu ya TMA ya Arusha kwa magoli 2-1 kwenye mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza.

Mchezo huo uliokuwa mkali umefanyika kwenye uwanja wa Filbert Bayi uliopo Mkuza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Akizungumzia juu ya mchezo huo mwalimu wa timu ya Barberian Julio Elieza amesema kuwa waliweka mpango mzuri ambao ulifuatwa na wachezaji wake hadi kuibuka na ushindi licha ya kutanguliwa na wapinzani.

Kwa upande wake nahodha wa Barberian Kasim Haruna amesema ushindi wao ulitokana na kufuata maelekezo ya mwalimu wao. 

Mwalimu wa TMA Tiko Tiko alikiri kuzidiwa na wapinzani wao na kujikuta wakiambulia kipigo hicho.

Naye nahodha wa timu hiyo Fadhil Mahimbo amesema licha ya kuongoza walicheza chini na kuwapa nafasi wapinzani wao kurudi na kupata ushindi.

Timu ya Barberian ambayo inatumia uwanja huo wa Filbert Bayi inatarajiwa kucheza tena Januari 17 kwenye uwanja huo dhidi ya timu ya Songea United ambapo wameahidi kuendeleza wimbi la ushindi.


No comments:

Post a Comment