Monday, January 26, 2026

HALMASHAURI YAKABIDHI MADAWATI 4,000

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imetoa madawati viti na meza 4,000 kwa Shule za Msingi na Sekondari vikiwa na thamani ya shilingi milioni 400.

Akikabidhi madawati viti na meza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa Halmashauri imefanya jambo zuri la kukabili changamoto ya wanafunzi kukaa chini.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa idadi ya wanafunzi inaongezeka kutokana na wazazi kuhamia Kibaha.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa alisema kuwa walitenga kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kutengeneza madawati viti na meza 4,000 ikiwa kwa Shule za Msingi madawati 2,000 na Sekondari viti na meza 2,000.

No comments:

Post a Comment