Tuesday, January 13, 2026

BINGWA

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

No comments:

Post a Comment