Thursday, October 17, 2024
HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAKUSANYA MAPATO ASILIMIA 33 ROBO YA KWANZA
Tuesday, October 15, 2024
MKUU WA MAJESHI AWAVISHANI NISHANI MAJENERALI, MAAFISA NA ASKARI WA JWTZ
Nishani hizo ni Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya Muungano pamoja na Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ.
Aidha,Jenerali Mkunda amewavisha nishani ya Jumuiya ya SADC Maafisa na Askari walioshiriki Ulinzi wa Amani nchini Msumbiji chini ya mwavuli wa Jumuiya hiyo.
Sunday, October 13, 2024
SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU NYERERE YAINGIA MAKUBALIANO NA CHUO CHA RENMIN CHA CHINA
SHULE ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere imeingia makubaliano ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Renmin katika nyanja mbalimbali zikiwemo za mafunzo utafiti na kubadilishana wataalamu.
Wakisaini makubaliano hayo kati ya Mkuu wa Shule ya Mwalimu Nyerere Profesa Marcellina Chijoriga na kiongozi mkuu wa Chama Tawala Cha China Cha (CPC) kwenye Renmin Zhang Donggang katika Shule hiyo iliyopo Kibaha Mkoani Pwani walifurahishwa na ushirikiano huo.
Chijoriga alisema kuwa makubaliano hayo yatakuwa ni kwa ajili ya kubadilishana wataalamu ambapo wao watakuja huku na wa Tanzania watakwenda kwao ikiwa ni sehemu ya kubadilishana uzoefu.
“Chuo hicho ni kikubwa sana na cha muda mrefu na kiko vizuri kwenye masuala ya utafiti wa uandishi wa vitabu na katika masuala ya uandishi wa vitabu ambapo ushirikiano huo utakuwa na manufaa makubwa sana kwa pande zote mbili,”alisema Chijoriga.
Alisema kuwa chuo hicho cha Renmin kinauwezo mkubwa wa kuwajengea uwezo viongozi wa chama na serikali kwani kiko vizuri sana katika ufundishaji masuala hayo na watatumia uzoefu ili kujifunza kupitia kwao kwani kimeanza muda mrefu.
“Faida hiyo ni kwa vyama sita vya ukombozi Kusini mwa Afrika ambapo China ni msaidizi mzuri kwani wamesaidia ujenzi wa shule hiyo ambavyo ni CCM, FRELIMO, SWAPO, ANC na ZANU-PF ambapo CPC .
Aidha alisema kuwa chuo hicho kilichopo Beijeng China kilianza ushirikiano mwaka jana ambapo uongozi wa Shule walikwenda na katibu mkuu wa CCM wakati ule Chongolo na sasa imeanza safari mpya na kina uzoefu mkubwa nani cha zamani sana.
“Tunashukuru sana kwani wametuonyesha ushirikiano mkubwa na makubaliano ya kutengeneza ushirikiano huu ni sasa safari mpya imeanz na leo waametupa vitabu tunawashukuru kwani maktaba yetu sasa itakuwa na vitabu vingi na wasomaji wataweza kujifunza masuala mbalimbali ya nchi ya China,”alisema Chijoriga.
Naye alisema Dk Evaristo Haule Naibu Mkuu wa Chuo Mipango Fedha na Utawala Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alisema kuwa China imefanikiwa na tumeona namna gani kutumia njia ili kuona wao wamefanyaje na kufikia hatua kubwa kiasi hicho kwenye maendeleo na CPC inavyotoa dira kuongoza nchi yao wanataka twende pamoja katika miradi yao mikubwa ya kidunia.
Haule alisema kuwa ili kwenda pamoja hivi karibuni Rais Dk Samia Suluhu Hassan alienda China kwenye mkutano wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika wao wana dira na kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya kazi na watu wawe na uzalendo wa nchi watu wanaangalia changamoto badala ya kuangalia fursa zilizopo.
Naye Dk Theresia Dominick kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam alisema kuwa Watanzania wanatakiwa kujifunza kwa kuwa nadhifu na wanaangalia masuala ya ulaji na wawe watu wa kujishusha na kuachana na matumizi yasiyo ya lazima na wasiwe na tamaa.
Dominick alisema kuwa badhi ya wafanyabiashara Watanzania wamekuwa wakienda China hivyo wanapaswa kujifunza tabia za Wachina za kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya jambo wanalolifanya ni mfano wa kuigwa.
Naye kiongozi huyo Zhang Donggang alisema kuwa ushirikiano uliopo baina ya China na Tanzania nan chi nyingine ni katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo ambapo wao wanaangalia sana maslahi ya wananchi.
Donggang alisema kuwa nchi za Afrika na China zinapaswa kushikana mkono katika kuhakikisha zinapiga hatua katika masuala ya kimaendeleoili kudumisha umoja uliopo kwani umoja uliopo umeleta mafanikio makubwa.
Mwisho.
BASHUNGWA ARDHISHWA UJENZI SEKONDARI MPYA YA MSANGANI
WAHITIMU KIDATO CHA NNE WATUMIE RASILIMALI ZILIZOPO NCHINI
WAHITIMU wa kidato cha nne nchini wametakiwa kuacha mawazo ya kwenda nje ya nchi kutafuta maisha badala yake watumie rasilimali za nchi kuongeza pato la Taifa.
Saturday, October 12, 2024
MILIONI 1.2 KUANDIKISHWA PWANI
WATU milioni 1.2 Mkoani Pwani wanatarajiwa kuandikishwa kwenye Daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.
Akizungumza baada ya kuzindua zoezi hilo kwenye Mtaa wa Mkoani A uliopo Kata ya Tumbi Wilaya ya Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alisema kuwa idadi hiyo inatokana na sensa iliyofayika ambapo alisema kuwa vijana wengi watakuwa wamefikisha miaka 18 hivyo kuwa na sifa za kujiandikisha kupiga kura.
Kunenge alisema kuwa mkoa una jumla ya vituo vya kuandikisha wapiga kura 2,374 na kuna Vijiji 417, vitongoji 2,028 na Mitaa 72 ambapo wananchi kwenye maeneo hayo wanapaswa kwenda kujiandikisha ili wapate fursa ya kupiga kura itakapofika wakati wa uchaguzi.
“Tumeweka vituo vingi vya kujiandikisha kupunguza msongamano ili kila mtu apate haki ya kujiandikisha ili aje apate fursa ya kupiga kura ambayo ni haki yako ya kikatiba kwa mujibu wa kanuni taratibu na sheria za nchi yetu hivyo wananchi mjitokeze kwa wingi,”alisema Kunenge.
Alisema kuwa viongozi wa kwanza ni wale wa ngazi za chini hivyo kuchagua viongozi hawa ni wa muhimu sana kwani wao wako na wananchi kuanzia chini kabisa hivyo wananchi wanapaswa kujitokeza kuwachagua lakini waanze kujiandikisha kwanza kwani kama mwananchi hajajiandikisha hatapata fursa ya kupiga kura.
“Viongozi tunaoanza nao ni wa ngazi za chini kwa ajili ya kutuletea maendeleo na ndipo msingi wa utawala bora unapoanzia na hawa watatusaidia kutuletea maendeleo hivyo tuhakikishe tunashiriki kwenye uchaguzi huu ni muhimu sana ili kuchagua viongozi wanaotufaa,”alisema Kunenge.
Aidha alisema kuwa wananchi wajipange kushiriki uchaguzi kwani hiyo ni haki ya kikatiba hivyo wale wote waliofikia umri kuanzia miaka 18 wahakikishe wanajitokeza kujiandikisha ili wapate fursa ya kuchagua viongozi wanaowapenda.
“Hii ni fursa nzuri ya kuchagua viongozi ambao watatuongoza kwa kipindi cha miaka mitano na tukichagua viongozi bora watatuletea maendeleo ndani ya maeneo yetu kuanzia ngazi ya chini kabisa hivyo hii ni fursa kwetu sote kwa maendeleo yetu,”alisema Kunenge.
Kwa upande wake mmoja ya watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha ambaye ni moja ya watu waliokwenda kujiandikisha Simon Mwaiteleke alisema kuwa hiyo ni nafasi yake ya kumfanya ili aweze kuja kupiga kura kwa viongozi kwenye mtaa wake.
Mwaiteleke alisema kuwa uchaguzi ni hatua ya kupata viongozi watakaowatumikia wananchi hivyo anawaomba watu kujitokeza kwa wingi ili kutumia fursa hiyo ambayo hujitokeza kila baada ya miaka mitano.
Naye Saumu Almasi alisema kuwa hiyo ni fursa kwao wananchi kuchagua viopngozi wa Mtaa kuanzia mwenyekiti na wajumbe wake hivyo anaona ni fursa ya kumchagua kiongozi ambaye ana sifa ya kuongoza mtaa anaotoka.
Almasi alisema kuwa wananchi watumie fursa hiyo kumpata kiongozi bora na wasibaki kulalamika wakati hawashiriki uchaguzi kwani kiongozi bora anapatikana kwa kupigiwa kura na siyo kukaa pembeni na kulalamika.
Thursday, September 12, 2024
*KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ELIMU, UTAMADUNI YAIFAGILIA KIBAHA MJI KWA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO*
Na Mwandishi Wetu, Kibaha
Kamati ya Kudumu ya Bunge inayosimamia Wizara ya Elimu na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imeridhika na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Shimbo iliyopo Kata ya Mkuza,Halmashauri ya Mji Kibaha.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Husna Sekiboko amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ndoto na maono yake ni kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata Elimu bora kwenye Mazingira rafiki ili kuandaa Wataalam kulitumikia Taifa lao na kwamba Kibaha Mji wamesimamia Ujenzi wa shule hiyo kwa viwango na thamani ya fedha inaonekana.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Leah Lwanji ameieleza Kamati kuwa Jumla ya Shilingi 528,998,425 kupitia Mradi wa SEQUIP zilipokelewa ajili ya Ujenzi wa miundombinu 27 na tayari imekamilika na tayari Wanafunzi 281 kati yake wavulana 149 na Wasichana 132 wameanza kunufaika kwa kuwapunguzia umbali mrefu wa zaidi ya kilometa 8 kuifuata shule Mama ya Nyumbu.
Mhe.Hamisi Shabani Taletale ameipongeza Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa Mradi na kushauri kujengwa kwa uzio ili kuwawekea utulivu wanafunzi wakati wa Masomo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Husna Sekiboko ametoa maelekezo ya Kamati kama ifuatavyo;
Mosi, Shule zote nchini ziwe na utaratibu wa kukagua maudhui ya vitabu kama vinaendana na maadili ya Watanzania kuelekeza vitabu vihakikiwe na kugongwa mihuri wa kuridhia Matumizi na Kamishina wa Elimu nchini.
Pili,Serikali iangalie upya mgawanyo wa fedha zinazotolewa kwa ajili ya Miradi kwani yapo maeneo wanakamilisha Ujenzi na maeneo mengine hawakamilishi ama Kujenga chini ya Kiwango na kuathiri matarajio na malengo.Ameitaka Wizara ya Elimu kufanya tathmini ya kimaeneo ili fedha zinazotolewa zitosheleze ili kuongeza tija ya Miradi husika.
Waziri wa Elimu Prof.Adolf Mkenda ameishukuru Kamati kwa kazi nzuri na kupokea maelekezo yote ya Kamati kwa ajili ya kufanyia kazi.
Aidha,Mwenyekiti wa Kamati Mhe.Sekiboko amempongeza sana Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa Mkurugenzi wa Mji Kibaha kwa usimamizi mzuri wa Miradi ya Maendeleo kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani kuhakikisha Mabilioni ya fedha yanayotolewa na Dkt.Samia Suluhu Hassan yanafanyakazi zinazoonyesha matokeo kwa Watanzania.







