Tuesday, June 13, 2023

SENYAMULE AAGIZA CHEMBA KUJIPANGA UPYA

 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema hajaridhishwa na kasi ya ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi katika Kijiji cha Magungu Kata ya Mpendo Wilaya ya Chemba na kukemea vikali uongozi wa Kijiji kukusanya fedha kwa wananchi bila kufuata utaratibu.

Senyamule ameyasema hayo leo tarehe 13/06/2023 mara baada ya kufanya ziara yakukagua utekelezaji wa miradi ya boost katika Wilaya ya Chemba.

"Sijaona dhamira ya dhati katika ukamilishaji wa mradi huu kwa muda tuliokubaliana wa tarehe 30/6/2023, tumekubaliana sote kuwa miradi hii ikamilike kwa wakati lakini leo nimesikitishwa sana hatua hii ya ujenzi ambao uko katika hatua za awali" Senyamule amefafanua

Amesema hayuko tayari kuona dhamira njema ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea wananchi maendeleo hususan katika nyanja ya elimu haifikiwi kutokana na watu wachache kutotimiza wajibu wao.

"Katika mradi huu Chemba hamjafika hata asilimia 20 na mna siku 18 zimesalia, fedha zilitolewa kwa wakati mmoja nchi nzima, Wilaya nyingine za Mkoa wa Dodoma wako katika hatua za upauji, siko tayati kumuangusha Mhe. Rais, ujenzi ufanyike mchana na usiku" Senyamule ameagiza.

Katika hatua nyingine Mhe. Senyamule amekemea vikali utaratibu unaotumiwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Magungu Bw. Bernard Kapaya kuchangisha fedha wananchi bila kibali cha Mkuu wa Wilaya.

“Naomba kuwakumbusha kuwa Serikali imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule mpya, vyumba vya madarasa ya awali na msingi, nyumba za walimu na ujenzi wa Vyoo. Wananchi wasishurutishwe kuchangia fedha, wachangie kwa hiari yao wenyewe na utaratibu ufuatwe ikiwa ni pamoja na kuambatanisha muhtasari wa mkutano wa Serikali ya Kijiji na barua iliyopitishwa kwa Mkurugenzi kwenda kwa Mkuu wa Wilaya. Ni kinyume kuchangisha fedha bila kufuata utaratibu huo” Senyamule ameonya

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Chemba Bw. Gerald Mongella amesema kumekuwa na ucheweshaji kutokana na kusuasua kwa mchango wa nguvu za wananchi hali iliyopelekea ucheleweshaji wa upatikanaji wa madini.

Mkoa wa Dodoma kupitia mradi wa Boost umepokea kiasi cha Shilingi Bilioni 10.6 kwa ajili ujenzi wa Shule mpya 16, vyumba vya madarasa ya msingi 163, madarasa ya awali 16, ujenzi wa vyoo 106, nyumba za walimu 03 na darasa 01 la elimu maalumu. Wilaya ya Chemba imepokea kiasi cha shilingi Bilioni 1.3.

Katika ziara yake Mhe. Senyamule amekagua maendeleo ya ujenzi wa Shule mpya ya Magungu, Ujenzi madarasa katika Shule ya Msingi Birise, ujenzi wa madarasa Lahoda na Ujenzi wa shule mpya Handa ‘B’.

Saturday, June 10, 2023

PWANI BINGWA VIWANDA

 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt Samia Suluhu Hassan ameutaja Mkoa wa Pwani kuwa bingwa viwanda nchini.

Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo Juni 9, 2023 wakati akiwatambulisha Wakuu wa Mikoa waliohudhuria kwenye mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Ikulu jijini Dar es Saalam.

Katika Mkutano huo Rais amewataka wakuu wa mikoa nchini kuweka mazingira rafiki kwa ajili ya kuvutia wawekezaji na kwamba ataandaa tuzo kwa ajili ya mkoa kinara wa ukusanyaji mapato.

Mkoa wa Pwani una jumla ya viwanda 1522 kati ya hivyo  vikubwa ni 117 na 120 vya kati.

PWANI BINGWA WA VIWANDA NCHINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt Samia Suluhu Hassan ameutaja Mkoa wa Pwani kuwa bingwa viwanda nchini.

Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo Juni 9, 2023 wakati akiwatambulisha Wakuu wa Mikoa waliohudhuria kwenye mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Ikulu jijini Dar es Saalam.

Katika Mkutano huo Rais amewataka wakuu wa mikoa nchini kuweka mazingira rafiki kwa ajili ya kuvutia wawekezaji na kwamba ataandaa tuzo kwa ajili ya mkoa kinara wa ukusanyaji mapato.

Mkoa wa Pwani una jumla ya viwanda 1522 kati ya hivyo  vikubwa ni 117 na 120 vya kati.

SERIKALI YAWAGAWIA ARDHI WANANCHI


SERIKALI imewagawia wananchi sehemu ya eneo  waliolivamia kwenye Hifadhi ya Chemchem ya Maji ya Moto Wilayani Rufiji na kumaliza mgogoro baina ya wananchi na hifadhi hiyo.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge wakati akitoa tamko la kuhitimisha Mgogoro huo ikiwa ni Utekelezaji wa maazimio la Baraza la Mawaziri nane wa kisekta walioshughulikoa mgogoro huo ambapo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele alisoma taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa.

Kunenge alisema kufuatia wananchi hao kumegewa sehemu ya ardhi kutoka kwenye hifadhi hiyo aliwataka wananchi wanaozunguka maeneo hayo kutovamia tena eneo hilo.

"Naagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Kamishna Msaidizi wa Ardhi kupima upya eneo hilo la Hifadhi na kuandaa GN mpya,"alisema Kunenge.

Aidha aliwataka TFS kuchonga Barabara kuzunguka eneo hilo ili Kuweka kinga ya mipaka kati ya wananchi na Hifadhi hiyo.

Katika hatua nyingine Mkoa umetoa taarifa ya kuhitimisha mgogoro wa ardhi kwenye eneo la Delta ya Mto Rufiji Wilayani Kibiti na kuwataka wananchi kutofanya shughuli za kibinadamu katika hifadhi ya Misitu ya Mikoko na mazalia ya samaki.

Akisoma taarifa ya Mkuu wa mkoa ambapo mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Samwel Kolombo aliisoma amepiga marufuku ukataji wa Misitu ya Mikoko kwenye hifadhi hiyo ya Delta ya Mto Rufiji.

Alimtaka Mkurugenzi wa Halmshauri ya Kibiti kutoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi na kuwawezesha vifaa vya kuvulia samaki kwenye maji marefu.

Alisisitiza pia  kuanzisha kwa vikundi vya uhifadhi (BMU) ili kuimariasha ulinzi wa hifadhi hiyo ambayo ina mikoko mingi.

Friday, June 9, 2023

WADHAMINI WA MICHEZO WATAKIWA KUBORESHA ZAWADI ZA WASHINDI




WADHAMINI wa Michezo Mkoani Pwani wametakiwa kutoa zawadi ambazo zitakuwa kumbukumbu kwa washindi wa michezo mbalimbali ili kuleta hamasa kwa vijana kushiriki kwenye michezo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na  mdhamini wa mashindano ya Umoja wa Michezo Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) Mkoa wa Pwani Musa Mansour na kwa kuwa michezo ni ajira wadhamini waangalie kwa kuboresha upande wa zawadi ili ziwe kivutio.

Mansour alisema kuwa ili vijana wafikie malengo ya kuwa wachezaji bora na kufanikiwa lazima wawe na nidhamu ambapo kwa sasa michezo inawaletea maisha mazuri wachezaji na mamlaka husika ziboreshe viwanja na kuwapatia vifaa vya michezo na kuboresha maeneo ya wazi.

Naye ofisa michezo wa mkoa huo Grace Bureta alisema kuwa jumla ya wachezaji 120 wamechaguliwa kuunda timu ya  Mkoa ambayo itashiriki mashindano ya Taifa yatakayofanyika  mkoani Tabora ambapo timu hiyo imeiingia kambini kwenye shule ya sekondari Kibaha.





HALMASHAURI ZATAKIWA KUTENGA BAJETI ZA MICHEZO


HALMASHAURI za Mkoa wa Pwani zimetakiwa kutenga bajeti kwa ajili ya shughuli za michezo ili kuinua vipaji vya vijana kwenye michezo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Katibu Tawala wa Mkoa huo Rashid Mchata wakati akifunga mashindano Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) Mkoa wa Pwani.

Mchata alisema kuwa mbali ya bajeti pia Halmashauri zihakikishe kila shule inatenga eneo kwa ajili ya michezo ili wanafunzi wapate sehemu ya kucheza.

Naye ofisa michezo wa mkoa huo Grace Bureta alisema kuwa jumla ya wachezaji 120 wamechaguliwa kuunda timu ya  Mkoa ambayo itashiriki mashindano ya Taifa yatakayofanyika  mkoani Tabora ambapo timu hiyo imeiingia kambini kwenye shule ya sekondari Kibaha.

Naye mdau wa michezo Musa Mansour alisema kuwa kwa kuwa michezo ni ajira wadhamini waangalie kwa kuboresha upande wa zawadi ili ziwe kivutio kwa vijana kushiriki michezo.

Thursday, June 8, 2023

WAKAZI CHANGWAHELA WARIDHIA KUHAMA


WAKAZI wa Kitongoji Changwahela wilayani Bagamoyo wameridhia kutekeleza agizo la Serikali la kuondoka katika eneo walilolivamia na kufanya shughuli za kibinadamu na kufanya uharibifu wa mazingira.

Akizungumza na wananchi kwenye Kitongoji hicho na kutoa maagizo hayo ya serikali akiwa katika kushughulikia changamoto zinazotokana na migogoro ya ardhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa kuna uharibifu mkubwa umefanywa na wananchi hao ikiwemo ukataji wa  mikoko ambayo inatunza kingo za bahari na kuhifadhi mazingira ya fukwe na mazalia ya samaki.

Kunenge amesema kuwa maagizo hayo ni utekelezaji wa maamuzi yaliyofanywa na baraza la Mawaziri kufuatia ushauri wa timu ya mawaziri nane wa kisekta iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mwaka 2019/2020 ambao walishirikiana na wataalamu kushughulikia migogoro ya ardhi mkoani humo na maeneo mengi nchini.

Akiwa Wilayani Bagamoyo alifika katika Kitongoji cha Sanzale Kata ya Magomeni na aliwaelekeza wakazi waliyovamia eneo la Yusuph Kikwete kupisha ili mwenyewe aweze kuendelea na shughuli za uwekezaji au wakae nae na kukubaliana watakavyoona inafaa.

Wakati huo huo ametoa muda wa siku 90 kwa Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo kukamilisha  zoezi la urasimishaji makazi kwa ajili ya mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa wananchi wa waliopewa eneo la hekari 5,520 za Ranchi ya Taifa ya Ruvu.