Tuesday, May 19, 2015

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

Sunday, April 26, 2015

KILUVY UNITED YALILIA UDHAMINI TFF

Na John Gagarini, Kibaha
SHIRIKISHO la Soka Nchini (TFF) limeshauriwa kutafuta wadhamini kwa ajili ya ligi mbalimbali na si ligi kuu pekee ili kuzipunguzia gharama timu za madaraja ya chini.
Ushauri huo ulitolewa na mlezi wa timu ya soka ya Kiluvya United ya mkoa wa Pwani Edward Mgogo wakati wa sherehe za kutambulisha kombe walilochukua la ligi ya mabingwa wa mikoa kwa mkuu wa mkoa huo Evarist Ndikilo na kufanikiwa kupanda daraja la kwanza.
Mgogo alisema kuwa timu za madaraja ya chini zina mzigo mkubwa katika kuziendesha timu zao hivyo ni vema zikasaidiwa kupata ufadhili ili ziweze kushiriki ligi zao vizuri.
“Umefika wakati sasa ligi za chini nazo zikawa na udhamini ndiyo kazi ya TFF kuziwekea mazingira mazuri timu ziweze kushiriki vema kwenye ligi ambapo ligi kuu imekuwa na wadhamini tofauti tofauti,” alisema Mgogo.
Alisema kuwa msingi wa wachezaji wa ligi kuu ni ligi ndogo za chini hivyo ni vema TFF ikatafuta wadhamini ili wadhamini ligi hizo ambazo zinatoa wachezaji ambao wanatamba kwenye ligi ya Voda Com.
“Bila ya udhamini timu zinacheza kwenye mazingira magumu sana ambapo sisi tunatarajia kucheza ligi daraja la kwanza hivyo tunaomba TFF iliangalie hili pamoja na wadau wengine wajitokeze kutusaidia ili tufikie lengo letu la kupanda ligi kuu,” alisema Mgogo.
Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa mkoa ambaye ni ofisa elimu Yusuph Kipengele alisema kuwa mkoa hauna fungu maalumu kwa ajili ya michezo.
 Kipengele alisema kuwa wao kama mkoa wanachoweza ni kutoa barua kwa ajili ya timu kwenda kuomba misaada sehemu mbalimbali kwa ajili ya kusaidiwa ili kuendeleza michezo.
Mwisho.             

    

HABARI MBALIMBALI ZA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Pwani kimechagua viongozi wake kukiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Uchaguzi huo ambao ulifanyika mjini Kibaha mwishoni mwa wiki hii ulimerejesha madarakani mwenyekiti wa zamani John Kirumbi ambaye alijinyakulia jumla ya kura 43 kati ya kura 85 za wajumbe wa uchaguzi huo na kuwashinda wenzake sita.
Kirumbi aliwashinda Hamis Kwangaya aliyejipatia kura 41 na Rajab Chalamila aliyepata kura moja huku wengine wakiambulia patupu huku Stella Kiyabo akipata nafasi ya kuwakilisha mkoa ngazi ya Taifa alijinyakulia kura 58.
Katika nafasi hiyo wagombea Hebert Mgimi aliyepata kura 15 na Mikidadi Mbelwa 12 huku nafasi ya mwaka hazina ikienda kwa Abubakary Alawi aliyepata kura 48, Honesta Mwilenga akipata kura 34 na Neema Wasato akipata kura mbili.
Kwa upande wa mwakilishi wa wanawake Martha Kanyawana alipata kura 55, Happy Mahava alipata kura 29 na Ajenta Mrema alipata kura moja upande wa nafasi ya mwakilishi wa watu wenye ulemavu Mohamed Ngomero alipata kura 48 akifuatiwa na Robert Bundala kura 37.
Nafasi ya uwakilishi wa vijana Judith Mangi alishinda kwa kura 42, David Phares alipata kura 27 na Charles Tesha kura 11, mwakilishi wa wenyeviti ni Mustapha Julius kura 80 huku za hapana zikiwa ni tano.
Kwa upande wa mjumbe kwenda baraza la Wafanyakazi TUCTA ni Rajab Mhambage aliyepata kura 71 kura nane za hapana na moja iliharibika huku wajumbe wawili kwenda TUCTA ni Grace Kalinga kura 54 na  Herbet Ngimi kura 28 huku kura mbili zikiharibika.
Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo katibu wa CWT Pwani Joseph Nehemia alisema kuwa uchaguzi huo ulikwenda vizuri licha ya changamoto ndogondogo za hapa na pale.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha ACT Wazalendo mkoani Pwani kimeanza kujiimarisha baada ya kuweza kujinyakulia wanachama 1,200 kutoka vyama mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini  Kibaha katibu wa ACT mkoa wa huo Mrisho Halfan alisema kuwa chama hicho kimeweza kupata wanachama wengi kwa muda mfupi kutokana na sera nzuri ilizonazo.
Halfan alisema kuwa sera za chama hicho ni zile alizokuwa akitekeleza Mwalimu Julius Nyerere za uzalendo wan chi yake na si manufaa ya mtu au watu wachache.
“Uzinduzi wa matawi nao umesaidia kuwavutia watu kujiunga na chama chetu ambacho ni chama cha wazalendo na kina mlengo tofauti na vyama vingine na kitaleta mageuzi ya kweli,” alisema Halfan.
Alisema kuwa ACT inakuja kivingine ili kufikia lengo la kuwasaidia wananchi kwani baadhi ya vyama havina sera nzuri zaidi ya kushambuliana majukwaani.
“ACT ni chama cha ukweli sisi hatutaki siasa za kukashifiana kama baadhi ya vyama vinavyofanya ambapo hutumia muda mwingi kushambulia upande fulani lakini vinashindwa kuwajibika kwa wananchi,” alisema Halfan
Aidha alisema kwa sasa watu wanataka maendeleo na si malumbano kwani yamewapotezea muda watu badala ya kutafakari kuleta maendeleo ambayo ndiyo kiu ya kila Mtanzania.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha wa wafanyakazi wa hifadhi ya mahoteli na majumbani na huduma za jamii (CHODAWU) kimewaomba waajiri kuchagua wafanyakazi bora na hodari wakati wa sherehe za siku ya wafanyakazi duniani Mei Mosi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mwenyekiti wa CHODAWU mkoani Pwani Paul Msilu alisema kuwa waajiri wafanye uchaguzi mzuri juu ya wafanyakazi bora.
Msilu alisema kuwa kwa mwaka huu chama chao ndiyo kinachoandaa sherehe za wafanyakazi kupitia shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwenye mkoa huo zitakazofanyika wilayani Mafia.
“Tunawaomba waajiri kuwachagua wafanyakazi bora ili iwe motisha na kuondoa manunguniko juu ya uteuzi wa wafanyakazi wenye sifa za kuwa bora,” alisema Msilu.
Aidha alisema anaomba waajiri kuwapatia zawadi zinazostahili ili kuwafanya wafanyakazi wajitume wawapo kazini kwani motisha ya zawadi nzuri ndizo zitaleta jitihada za uwajibikaji.
“Maandalizi yanaendelea vizuri ambapo baadhi ya vitu vimekamilika na bado tunaendelea kuomba michango kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo waajiri ili kufanikisha sherehe hizo zinazofanyika kila mwaka,” alisema Msilu.
Alisema sherehe hizo ni muhimu kwa wafanyakazi ambao siku hiyo hukaa kwa pamoja na kubadilishana mawazo pamoja na kujua changamoto na mafanikio yao kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WALIMU na wanafunzi wametakiwa kushirikiana ili kuhakikisha Taifa la Tanzania linakuwa na watafiti na wagunduzi wa teknolojia mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka wakati wa sherehe za kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri kwenye shindano la Insha iliyokuwa inasema utatumiaje rasilimali zlizopo kukiabilina na umaskini lililoandaliwa na mbunge huyo.
Koka alisema kuwa utafiti na ugunduzi ndiyo utakaopelekea nchi kupata mafanikio katika maenedeleo kupitia tafiti na ugunduzi wa masuala mbalimbali.
“Tafiti na ugunduzi ndiyo silaha ya kujiletea maendeleo kwa nchi yoyote ile hivyo lazima tuwajenge wanafunzi wetu kuwa wagunduzi na watafiti wa mambo ya kimaendeleo,” alisema Koka.
Alisema kuwa endapo wanafunzi wataandaliwa katika katika masuala hayo basi watweza kugundua teknolojia ambazo wataziuza kama ilivyo kwa mataifa yaliyoendelea ambayo yananufaika.
“Hayo yote tunaweza kuyafikia kwa kuwa na ushirikiano baina ya pande zote wakiwemo walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe na insha kama hizi huwasaidia wanafunzi kujenga ujasiri wa kujieleza na kama maandalizi ya elimu ya juu,” alisema Koka.
Awali kwa upande wake mwenyekiti wa Asasi isiyo ya kiserikali ya Youth Under Umbrella Castro David alisema kuwa lengo la insha hiyo ambayo ilishirikisha shule 14 za sekondari ni kuwajengea wanafunzi ustadi wa uandishi wa kazi za fasihi za ubunifu .
David alisema kuwa pia lengo lingine ni  kuziunganisha shule ili ziwe na ushirikiano wa kitaaluma na kufanya utafiti ambapo mshindi alikuwa ni Sara Malambo kutoka shule ya sekondari ya Tumbi ambaye alijinyakulia 100,000, akifuatiwa na Hija Hega wa Visiga 50,000 na Peter Asenga 30,000 ambazo walikabidhiwa na Mbunge huyo.
Mwisho.

Saturday, April 11, 2015

PWANI YAINGIZA MABILIONI KUPITIA MISITU

Na John Gagarini, Bagamoyo
MKOA wa Pwani umefanikiwa kukusanya kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni nane kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika kipindi cha mwaka 2013/2014.
Hayo yalisemwa juzi wilayani Bagamoyo na Ofisa Misitu wa mkoa huo Daniel Isara, wakati wa maadhimisho ya upandaji miti kimkoa iliyofanyika kwenye eneo la la Gareza la Kigongoni ambapo ilipandwa zaidi ya miti 3,000.
Isara alisema kuwa fedha hizo zimetokana na kukabiliana na uharibifu wa rasilimali misitu na mazingira ambapo doria ziliimarishwa na ukusanyaji wa mapato kufikia kiasi hicho.
Alisema kuwa hadi kufikia mwezi Januari 2014/2015 makusanyo yalifikia kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni sita baada ya wakala hao kuongeza watumishi kwenye ngazi za wilaya.
“Mbali ya mafanikio ya ukusanyaji wa mapato hayo ya Serikali pia mkoa umehamasisha na mwamko umekuwa mkubwa na kuongeza uanzishwaji wa vitalu vya miche na upandaji wa miti kwe taasisi za serikali na zisizo za serikali na watu binafsi kutoka miche ya miti milioni 2,253,136 mwaka 2013/2014 na kufikia milioni 2,663,202 mwaka 2014/2015,” alisema Isara.
Aidha alisema kuwa pia wakala imeweza kuwaondoa wavamizi kwenye misitu ya Ruvu Kaskazini, Ruvu Kusini, Kiloka, Kazimzumbwi na wavuvi kwenye Delta ya Rufiji pia kuweka mipaka ya misitu ya hifadhi kiasi cha kilometa 640 katika hekta 10,704.
“Changamoto zinazoikabili rasilimali ya misitu ni pamoja na ongezeko kwa wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam ambalo huongeza mahitaji ya mkaa na kuni hivyo kuongezeka kwa ukataji na ufyekaji wa misitu na mapori,” alisema Isara.
Alibainisha kuwa kuna wafanyabiashara 320 waliosajiliwa kufanyabiashara ya kuvuna mazao ya misitu mkoani Pwani kwa  mwaka 2013/2014 na 336 mwaka 2014/2015 na zaidi ya asilimia 90 wanatoka nje ya mkoa.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Pwani  Evarist Ndikilo ambaye aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga alisema kuwa taasisi zinazotumia kuni kwa wingi kwa ajili ya kupikia na shughuli nyingine zinapaswa kupanda miti kwa wingi.
Ndikilo alisema kuwa zinapaswa kutumia majiko sanifu yanayotumia kuni au mkaa kidogo ili iwe sehemu ya ubunifu wa kupunguza matumizi makubwa ya nishati ya miti.
Aliwataka wananchi kila mtu kupanda miti ili kulinda mazingira pia mamalaka za serikali za mitaa kuomba vibali vya kuajiri watumishi kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa rasilimali misitu na misitu iliyohifadhiwa inatunzwa na kuzuia wavamizi wanaoingiza mifugo, uchimbaji wa mchanga, kilimo na makazi kwenye misitu.
Mkoa wa Pwani una misitu 34 ya hifadhi yenye jumla ya hekta 335,712 iliyohifadhiwa kisheria na hekta milioni 2.2 ya misitu kwenye ardhi huria ambayo hutegemewa na mikoa ya Pwani na Dar es Salaam kwa ajili ya matumizi ya nishati za magogo, mbao, samani na matumizi mengine.
Mwisho.      


 MKUU wa wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Majid Mwanga akipanda mti kwaniaba ya mkuu wa wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo kama ishara ya maadhimisho ya siku ya kupanda miti kimkoa kwenye eneo la Gereza la Kigongoni 

Sunday, April 5, 2015

PIMENI MAENEO YA SHULE NA WAKRISTO WAOMBEENI POLISI

Na John Gagarini, Chalinze
VIONGOZI wa Vijiji na Vitongoji kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo  mkoani Pwani wametakiwa kupima maeneo yao ya shule ili kupata hati miliki na kuepuka uvamizi wa maeneo hayo.
Hayo yamesemwa na Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa shule ya Msingi ya Happy Lukwambe kwenye kijiji cha Visakazi.
Ridhiwani alisema kuwa baadhi ya shule Jimboni humo maeneo yake hayajapimwa hivyo kufanay baadhi ya watu kuvamia maeneo ya shule.
“Kwa kuwa eneo lenu la shule liko kwenye mazingira mazuri na mmefanya uhifadhi wa misitu ni vema mkalipima eneo lenu ili muwe na hati ya umiliki wa ardhi muweze kukabiliana na wavamizi wa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shule,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kwa kuwa shule hiyo imejengwa kisasa ni moja ya shule za msingi ambazo ni za mfano katika wilaya ya Bagamoyo na hata nchi nzima lazima mazingira yake yalindwe.
“Isije ikawa baada ya muda si mrefu mkaja kwangu kulalamika kuwa eneo lenu limevamiwa nawashauri pimeni eneo lenu kupitia uongozi wa shule na Kijiji ili kufanikisha zoezi hilo,” alisema Ridhiwani.
Kwa upande wake moja ya wafadhili wa ujenzi wa shule hiyo Happy Frank kutoka nchini Uingereza alisema kuwa ameridhishwa na ujenzi huo na kusema kuwa kukamilika kwa shule hiyo japo ni madarasa matatu lakini ni mafanikio na ni kumbukumbu nzuri kwa familia yake.
Naye msimamizi wa ujenzi huo Remigius Mshenga alisema kuwa shule hiyo imejengwa kutokana na eneo hilo kutokuwa na shule ambapo wanafunzi walikuwa wakienda kilometa 17 kwenye shule ya Msingi Bwawani.
Mshenga alisema kuwa watoto wengi wa eneo hilo walikuwa wakishindwa kwenda shule kutokana na umbali ambapo wengine waliacha shule na sasa inaanza na wanafunzi 55 ambapo gharama za ujenzi ni shilingi milioni 60 pamoja na madawati na ujenzi wake ulianza mwaka 2013 wa madarasa matatu.
Naye ofisa elimu wa wilaya ya Bagamoyo Abdul Buheti alisema kuwa wataendelea kuisaidia shule hiyo kwa kuhakikisha wanapeleka walimu wenye sifa pamoja na vitabu vya ziada na kiada na kwa kuitambua shule hiyo tayari wameshapeleka walimu wawili wanaofundisha watoto hao wa darasa la kwanza hadi la tatu.
Shule hiyo imekengwa kwa ufadhili wa Happy Bricks Foundation ya nchini Uingereza na kusimamiwa na taasisi ya Ngerengere River Eco Camp.
Mwisho.  
Na John Gagarini, Kibaha
WAKRISTO nchini wametakiwa wakati wakiadhimisha sikukuu ya kufufuka Yesu Kristo  (Pasaka)  waliombee Jeshi la Polisi lisendelee kufanyiwa vitendo vya kinyama na baadhi ya watu wenye nia mbaya na nchi.
Siku za hivi karibuni kuwamekuwa na matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi na kuwaua askari kisha kupora silaha ambazo hazifahamiki huwa zinapelekwa wapi.
Akizungumza kwenye ibaada ya Pasaka kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Jimbo la Magharibi Usharika wa Maili Moja, Mchungaji wa kanisa hilo Isai Ntele alisema kuwa hali hiyo inahatarisha amani ya nchi.
Mch Ntele alisema kuwa hali hiyo ya uvamizi wa vituo vya polisi na kuwaua kisha kuchukua silaha havipaswi kuachwa kuendelea kwani haifahamiki silaha zinazoibiwa zinatumika vipi.
“Hali hii si ya kuifumbia macho hata sisi wakristo wakati tunasherehekea sikukuu hii ya kufufuka Yesu Kristo lazima tuiombee amani ya nchi kwani walinda amani wanashambuliwa sasa na kuuwawa sisi tutakuwa salama,” aliuliza Mch Ntele.
Aidha alisema kuwa watu hao wanaofanya vitendo hivyo wanaweza wakawa wanafanya uhalifu kwa kutumia silaha hizo hivyo wananchi wakawa hawawezi tena kuishi kwa amani na kuwajengea hofu.
“Watu hawa ni wabaya kwani wakiingia mtaani na hizo silaha tutakuwa hatuna amani tena kwani vitendo vya uhalifu vitaongezeka hivyo lazima tufanya maombi ya kuwaombea askari wetu ili wawe salama waweze kutulinda na sisi,” alisema Mch Ntele.
Aliwataka wakristo kuadhimisha sikukuu hiyo kwa upendo na mshakamano na kuacha vitendo ambavyo vitaleta athari ndani ya jamii ili kudumisha amani ya nchi yetu.
Mwisho.