Na
John Gagarini, Kibaha
CHAMA
cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Pwani kimechagua viongozi wake kukiongoza
chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Uchaguzi
huo ambao ulifanyika mjini Kibaha mwishoni mwa wiki hii ulimerejesha madarakani
mwenyekiti wa zamani John Kirumbi ambaye alijinyakulia jumla ya kura 43 kati ya
kura 85 za wajumbe wa uchaguzi huo na kuwashinda wenzake sita.
Kirumbi
aliwashinda Hamis Kwangaya aliyejipatia kura 41 na Rajab Chalamila aliyepata
kura moja huku wengine wakiambulia patupu huku Stella Kiyabo akipata nafasi ya
kuwakilisha mkoa ngazi ya Taifa alijinyakulia kura 58.
Katika
nafasi hiyo wagombea Hebert Mgimi aliyepata kura 15 na Mikidadi Mbelwa 12 huku
nafasi ya mwaka hazina ikienda kwa Abubakary Alawi aliyepata kura 48, Honesta
Mwilenga akipata kura 34 na Neema Wasato akipata kura mbili.
Kwa
upande wa mwakilishi wa wanawake Martha Kanyawana alipata kura 55, Happy Mahava
alipata kura 29 na Ajenta Mrema alipata kura moja upande wa nafasi ya
mwakilishi wa watu wenye ulemavu Mohamed Ngomero alipata kura 48 akifuatiwa na
Robert Bundala kura 37.
Nafasi
ya uwakilishi wa vijana Judith Mangi alishinda kwa kura 42, David Phares
alipata kura 27 na Charles Tesha kura 11, mwakilishi wa wenyeviti ni Mustapha
Julius kura 80 huku za hapana zikiwa ni tano.
Kwa
upande wa mjumbe kwenda baraza la Wafanyakazi TUCTA ni Rajab Mhambage aliyepata
kura 71 kura nane za hapana na moja iliharibika huku wajumbe wawili kwenda
TUCTA ni Grace Kalinga kura 54 na Herbet
Ngimi kura 28 huku kura mbili zikiharibika.
Akizungumza
mara baada ya uchaguzi huo katibu wa CWT Pwani Joseph Nehemia alisema kuwa
uchaguzi huo ulikwenda vizuri licha ya changamoto ndogondogo za hapa na pale.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Kibaha
CHAMA
cha ACT Wazalendo mkoani Pwani kimeanza kujiimarisha baada ya kuweza
kujinyakulia wanachama 1,200 kutoka vyama mbalimbali.
Akizungumza
na waandishi wa habari mjini Kibaha katibu
wa ACT mkoa wa huo Mrisho Halfan alisema kuwa chama hicho kimeweza kupata
wanachama wengi kwa muda mfupi kutokana na sera nzuri ilizonazo.
Halfan
alisema kuwa sera za chama hicho ni zile alizokuwa akitekeleza Mwalimu Julius
Nyerere za uzalendo wan chi yake na si manufaa ya mtu au watu wachache.
“Uzinduzi
wa matawi nao umesaidia kuwavutia watu kujiunga na chama chetu ambacho ni chama
cha wazalendo na kina mlengo tofauti na vyama vingine na kitaleta mageuzi ya
kweli,” alisema Halfan.
Alisema
kuwa ACT inakuja kivingine ili kufikia lengo la kuwasaidia wananchi kwani
baadhi ya vyama havina sera nzuri zaidi ya kushambuliana majukwaani.
“ACT
ni chama cha ukweli sisi hatutaki siasa za kukashifiana kama baadhi ya vyama
vinavyofanya ambapo hutumia muda mwingi kushambulia upande fulani lakini
vinashindwa kuwajibika kwa wananchi,” alisema Halfan
Aidha
alisema kwa sasa watu wanataka maendeleo na si malumbano kwani yamewapotezea
muda watu badala ya kutafakari kuleta maendeleo ambayo ndiyo kiu ya kila
Mtanzania.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Kibaha
CHAMA
cha wa wafanyakazi wa hifadhi ya mahoteli na majumbani na huduma za jamii (CHODAWU)
kimewaomba waajiri kuchagua wafanyakazi bora na hodari wakati wa sherehe za
siku ya wafanyakazi duniani Mei Mosi.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake mwenyekiti wa CHODAWU mkoani Pwani Paul
Msilu alisema kuwa waajiri wafanye uchaguzi mzuri juu ya wafanyakazi bora.
Msilu
alisema kuwa kwa mwaka huu chama chao ndiyo kinachoandaa sherehe za wafanyakazi
kupitia shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwenye mkoa huo
zitakazofanyika wilayani Mafia.
“Tunawaomba
waajiri kuwachagua wafanyakazi bora ili iwe motisha na kuondoa manunguniko juu
ya uteuzi wa wafanyakazi wenye sifa za kuwa bora,” alisema Msilu.
Aidha
alisema anaomba waajiri kuwapatia zawadi zinazostahili ili kuwafanya
wafanyakazi wajitume wawapo kazini kwani motisha ya zawadi nzuri ndizo zitaleta
jitihada za uwajibikaji.
“Maandalizi
yanaendelea vizuri ambapo baadhi ya vitu vimekamilika na bado tunaendelea
kuomba michango kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo waajiri ili kufanikisha
sherehe hizo zinazofanyika kila mwaka,” alisema Msilu.
Alisema
sherehe hizo ni muhimu kwa wafanyakazi ambao siku hiyo hukaa kwa pamoja na
kubadilishana mawazo pamoja na kujua changamoto na mafanikio yao kwa kipindi
cha mwaka mmoja.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Kibaha
WALIMU
na wanafunzi wametakiwa kushirikiana ili kuhakikisha Taifa la Tanzania linakuwa
na watafiti na wagunduzi wa teknolojia mbalimbali.
Hayo
yalisemwa mjini Kibaha na mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka wakati
wa sherehe za kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri kwenye shindano la Insha iliyokuwa
inasema utatumiaje rasilimali zlizopo kukiabilina na umaskini lililoandaliwa na
mbunge huyo.
Koka
alisema kuwa utafiti na ugunduzi ndiyo utakaopelekea nchi kupata mafanikio katika
maenedeleo kupitia tafiti na ugunduzi wa masuala mbalimbali.
“Tafiti
na ugunduzi ndiyo silaha ya kujiletea maendeleo kwa nchi yoyote ile hivyo
lazima tuwajenge wanafunzi wetu kuwa wagunduzi na watafiti wa mambo ya
kimaendeleo,” alisema Koka.
Alisema
kuwa endapo wanafunzi wataandaliwa katika katika masuala hayo basi watweza
kugundua teknolojia ambazo wataziuza kama ilivyo kwa mataifa yaliyoendelea
ambayo yananufaika.
“Hayo
yote tunaweza kuyafikia kwa kuwa na ushirikiano baina ya pande zote wakiwemo
walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe na insha kama hizi huwasaidia wanafunzi
kujenga ujasiri wa kujieleza na kama maandalizi ya elimu ya juu,” alisema Koka.
Awali
kwa upande wake mwenyekiti wa Asasi isiyo ya kiserikali ya Youth Under Umbrella
Castro David alisema kuwa lengo la insha hiyo ambayo ilishirikisha shule 14 za
sekondari ni kuwajengea wanafunzi ustadi wa uandishi wa kazi za fasihi za
ubunifu .
David
alisema kuwa pia lengo lingine ni
kuziunganisha shule ili ziwe na ushirikiano wa kitaaluma na kufanya
utafiti ambapo mshindi alikuwa ni Sara Malambo kutoka shule ya sekondari ya
Tumbi ambaye alijinyakulia 100,000, akifuatiwa na Hija Hega wa Visiga 50,000 na
Peter Asenga 30,000 ambazo walikabidhiwa na Mbunge huyo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment