Na
John Gagarini, Kibaha
SHIRIKISHO
la Soka Nchini (TFF) limeshauriwa kutafuta wadhamini kwa ajili ya ligi
mbalimbali na si ligi kuu pekee ili kuzipunguzia gharama timu za madaraja ya
chini.
Ushauri
huo ulitolewa na mlezi wa timu ya soka ya Kiluvya United ya mkoa wa Pwani
Edward Mgogo wakati wa sherehe za kutambulisha kombe walilochukua la ligi ya
mabingwa wa mikoa kwa mkuu wa mkoa huo Evarist Ndikilo na kufanikiwa kupanda
daraja la kwanza.
Mgogo
alisema kuwa timu za madaraja ya chini zina mzigo mkubwa katika kuziendesha
timu zao hivyo ni vema zikasaidiwa kupata ufadhili ili ziweze kushiriki ligi
zao vizuri.
“Umefika
wakati sasa ligi za chini nazo zikawa na udhamini ndiyo kazi ya TFF kuziwekea
mazingira mazuri timu ziweze kushiriki vema kwenye ligi ambapo ligi kuu imekuwa
na wadhamini tofauti tofauti,” alisema Mgogo.
Alisema
kuwa msingi wa wachezaji wa ligi kuu ni ligi ndogo za chini hivyo ni vema TFF
ikatafuta wadhamini ili wadhamini ligi hizo ambazo zinatoa wachezaji ambao
wanatamba kwenye ligi ya Voda Com.
“Bila
ya udhamini timu zinacheza kwenye mazingira magumu sana ambapo sisi tunatarajia
kucheza ligi daraja la kwanza hivyo tunaomba TFF iliangalie hili pamoja na
wadau wengine wajitokeze kutusaidia ili tufikie lengo letu la kupanda ligi
kuu,” alisema Mgogo.
Kwa
upande wake mwakilishi wa mkuu wa mkoa ambaye ni ofisa elimu Yusuph Kipengele
alisema kuwa mkoa hauna fungu maalumu kwa ajili ya michezo.
Kipengele alisema kuwa wao kama mkoa
wanachoweza ni kutoa barua kwa ajili ya timu kwenda kuomba misaada sehemu
mbalimbali kwa ajili ya kusaidiwa ili kuendeleza michezo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment