Na John Gagarini,
Chalinze
VIONGOZI wa Vijiji na
Vitongoji kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kupima maeneo yao ya shule
ili kupata hati miliki na kuepuka uvamizi wa maeneo hayo.
Hayo yamesemwa na
Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa shule ya Msingi ya
Happy Lukwambe kwenye kijiji cha Visakazi.
Ridhiwani alisema kuwa
baadhi ya shule Jimboni humo maeneo yake hayajapimwa hivyo kufanay baadhi ya
watu kuvamia maeneo ya shule.
“Kwa kuwa eneo lenu la
shule liko kwenye mazingira mazuri na mmefanya uhifadhi wa misitu ni vema
mkalipima eneo lenu ili muwe na hati ya umiliki wa ardhi muweze kukabiliana na
wavamizi wa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shule,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kwa kuwa
shule hiyo imejengwa kisasa ni moja ya shule za msingi ambazo ni za mfano
katika wilaya ya Bagamoyo na hata nchi nzima lazima mazingira yake yalindwe.
“Isije ikawa baada ya
muda si mrefu mkaja kwangu kulalamika kuwa eneo lenu limevamiwa nawashauri
pimeni eneo lenu kupitia uongozi wa shule na Kijiji ili kufanikisha zoezi hilo,”
alisema Ridhiwani.
Kwa upande wake moja
ya wafadhili wa ujenzi wa shule hiyo Happy Frank kutoka nchini Uingereza alisema
kuwa ameridhishwa na ujenzi huo na kusema kuwa kukamilika kwa shule hiyo japo
ni madarasa matatu lakini ni mafanikio na ni kumbukumbu nzuri kwa familia yake.
Naye msimamizi wa
ujenzi huo Remigius Mshenga alisema kuwa shule hiyo imejengwa kutokana na eneo
hilo kutokuwa na shule ambapo wanafunzi walikuwa wakienda kilometa 17 kwenye
shule ya Msingi Bwawani.
Mshenga alisema kuwa
watoto wengi wa eneo hilo walikuwa wakishindwa kwenda shule kutokana na umbali
ambapo wengine waliacha shule na sasa inaanza na wanafunzi 55 ambapo gharama za
ujenzi ni shilingi milioni 60 pamoja na madawati na ujenzi wake ulianza mwaka
2013 wa madarasa matatu.
Naye ofisa elimu wa
wilaya ya Bagamoyo Abdul Buheti alisema kuwa wataendelea kuisaidia shule hiyo
kwa kuhakikisha wanapeleka walimu wenye sifa pamoja na vitabu vya ziada na
kiada na kwa kuitambua shule hiyo tayari wameshapeleka walimu wawili
wanaofundisha watoto hao wa darasa la kwanza hadi la tatu.
Shule hiyo imekengwa
kwa ufadhili wa Happy Bricks Foundation ya nchini Uingereza na kusimamiwa na
taasisi ya Ngerengere River Eco Camp.
Mwisho.
Na John Gagarini,
Kibaha
WAKRISTO nchini wametakiwa
wakati wakiadhimisha sikukuu ya kufufuka Yesu Kristo (Pasaka) waliombee Jeshi la Polisi lisendelee kufanyiwa
vitendo vya kinyama na baadhi ya watu wenye nia mbaya na nchi.
Siku za hivi karibuni
kuwamekuwa na matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi na kuwaua askari kisha
kupora silaha ambazo hazifahamiki huwa zinapelekwa wapi.
Akizungumza kwenye
ibaada ya Pasaka kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Jimbo la
Magharibi Usharika wa Maili Moja, Mchungaji wa kanisa hilo Isai Ntele alisema
kuwa hali hiyo inahatarisha amani ya nchi.
Mch Ntele alisema kuwa
hali hiyo ya uvamizi wa vituo vya polisi na kuwaua kisha kuchukua silaha havipaswi
kuachwa kuendelea kwani haifahamiki silaha zinazoibiwa zinatumika vipi.
“Hali hii si ya
kuifumbia macho hata sisi wakristo wakati tunasherehekea sikukuu hii ya
kufufuka Yesu Kristo lazima tuiombee amani ya nchi kwani walinda amani
wanashambuliwa sasa na kuuwawa sisi tutakuwa salama,” aliuliza Mch Ntele.
Aidha alisema kuwa
watu hao wanaofanya vitendo hivyo wanaweza wakawa wanafanya uhalifu kwa kutumia
silaha hizo hivyo wananchi wakawa hawawezi tena kuishi kwa amani na kuwajengea
hofu.
“Watu hawa ni wabaya
kwani wakiingia mtaani na hizo silaha tutakuwa hatuna amani tena kwani vitendo
vya uhalifu vitaongezeka hivyo lazima tufanya maombi ya kuwaombea askari wetu
ili wawe salama waweze kutulinda na sisi,” alisema Mch Ntele.
Aliwataka wakristo
kuadhimisha sikukuu hiyo kwa upendo na mshakamano na kuacha vitendo ambavyo
vitaleta athari ndani ya jamii ili kudumisha amani ya nchi yetu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment