Friday, June 20, 2014
WATATU WADAKWA NA SILAHA NA SARE ZA JESHI
Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kuwakamata watu watatu akiwemo mtu Daniel Mtalisi mkazi wa Kisemvule wilaya ya Mkuranga ambaye alipitia mafunzo ya kijeshi kwa tuhuma za kufanya tukio la uhalifu wa kupora silaha na vitu mbalimbali.
Mtuhumiwa huyo ambayealiwahi kupata mafunzo ya kijeshi kwenye Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi namba 833 Oljoro Arusha na namba yake ni MT. 95150.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa waandishi wa habari mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 17 mwaka huu majira ya saa 2 usiku huko Kijiji cha Kisemvule kata ya Vikindu kata ya Mkuranga wilaya ya Mkuranga.
Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao wengine wakiwa ni Khalfan Abas (25) mkazi wa Mwanambaya na Mashaka Masanja (24) mkazi wa Mwongozo Kigamboni Jijini Dar es Salaam walikamatwa baada ya polisi kufanya msako mkali na kumkuta mtuhumiwa huyo akiwa na silaha hiyo ambayo walimpora Musa Kambangwa ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanambaya.
“Watu hao walimvamia mlalamikaji ambaye alikuwa akirejea nyumbani kutoa kwenye biashara zake walimteka kisha kumpiga na walimwamuru awapeleke nyumbani kwake na kuichukua silaha hiyo bastola yenye namba A 569542 aina ya Browning, Carriber 7.65 mm, magazine 2 na risasi 23, chaja 1 ambavyo alikuwa amehifadhi nyumbani kwake,” alisema Kamanda Matei.
Aidha Kamanda Matei alisema kuwa kabla ya kukamatwa watuhumiwa hao walifanya tukio hilo Juni 11 mwaka huu huko Kijiji cha Mwanambaya ambapo walimvamia mlalamikaji akiwa na mke wake.
“Walimjeruhi kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kumsababishia maumivu makali kisha kumtaka awape funguo ya nyumba yake ili waingie ndani lakini alikataa wakaendelea kumpiga hadi alipopoteza fahamu na kuichukua funguo na kuingia ndani na kuchuakua silaha hiyo na simu 2 aina ya Nokia, Inveta , deki 1 ya Dvd na viatu pea moja kisha kutoweka na ndipo walipokuja kukamatwa Juni 17,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa baada ya tukio hilo ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kuvikuta vitu hivyo ambapo mtuhumiwa wa kwanza alikutwa na sare za Jeshi.
Alibainisha kuwa mlalamikaji anaendelea vizuri na kuwataka watu kutoa taarifa za uhalifu ili kuzuia matukio hayo ambayo yameanza kuibuka kwa wingi na watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika.
Mwisho
JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kuwakamata watu watatu akiwemo mtu Daniel Mtalisi mkazi wa Kisemvule wilaya ya Mkuranga ambaye alipitia mafunzo ya kijeshi kwa tuhuma za kufanya tukio la uhalifu wa kupora silaha na vitu mbalimbali.
Mtuhumiwa huyo ambayealiwahi kupata mafunzo ya kijeshi kwenye Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi namba 833 Oljoro Arusha na namba yake ni MT. 95150.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa waandishi wa habari mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 17 mwaka huu majira ya saa 2 usiku huko Kijiji cha Kisemvule kata ya Vikindu kata ya Mkuranga wilaya ya Mkuranga.
Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao wengine wakiwa ni Khalfan Abas (25) mkazi wa Mwanambaya na Mashaka Masanja (24) mkazi wa Mwongozo Kigamboni Jijini Dar es Salaam walikamatwa baada ya polisi kufanya msako mkali na kumkuta mtuhumiwa huyo akiwa na silaha hiyo ambayo walimpora Musa Kambangwa ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanambaya.
“Watu hao walimvamia mlalamikaji ambaye alikuwa akirejea nyumbani kutoa kwenye biashara zake walimteka kisha kumpiga na walimwamuru awapeleke nyumbani kwake na kuichukua silaha hiyo bastola yenye namba A 569542 aina ya Browning, Carriber 7.65 mm, magazine 2 na risasi 23, chaja 1 ambavyo alikuwa amehifadhi nyumbani kwake,” alisema Kamanda Matei.
Aidha Kamanda Matei alisema kuwa kabla ya kukamatwa watuhumiwa hao walifanya tukio hilo Juni 11 mwaka huu huko Kijiji cha Mwanambaya ambapo walimvamia mlalamikaji akiwa na mke wake.
“Walimjeruhi kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kumsababishia maumivu makali kisha kumtaka awape funguo ya nyumba yake ili waingie ndani lakini alikataa wakaendelea kumpiga hadi alipopoteza fahamu na kuichukua funguo na kuingia ndani na kuchuakua silaha hiyo na simu 2 aina ya Nokia, Inveta , deki 1 ya Dvd na viatu pea moja kisha kutoweka na ndipo walipokuja kukamatwa Juni 17,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa baada ya tukio hilo ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kuvikuta vitu hivyo ambapo mtuhumiwa wa kwanza alikutwa na sare za Jeshi.
Alibainisha kuwa mlalamikaji anaendelea vizuri na kuwataka watu kutoa taarifa za uhalifu ili kuzuia matukio hayo ambayo yameanza kuibuka kwa wingi na watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika.
Mwisho
Monday, June 16, 2014
WANAJESHI WAWILI WAFA AJALINI
Na John Gagarini, Kibaha
WATU wawili wamefariki dunia huku mmoja akijeruhiwa baada ya
magari waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani
Pwani, kamishna Msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP) Ulrich Matei amesema kuwa
ajali hiyo ilihusisha lori na gari dogo.
Kamanda Matei alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Juni 16 mwaka
huu majira saa 1:15 usiku eneo la Chamakweza kata ya Pera tarafa ya Chalinze
wilayani Bagamoyo.
Alisema ajali hiyo ilihusisha lori aina ya Scania lenye namba
za usajili T 164 AUS na tela namba T 498 AZ likiendeshwa na Hassan Shaban mkazi
wa Dar es Salaam ambaye aligongana na gari aina ya Isuzu Carry lenye namba za
usajili Z 190 DR likitokea mkoani Morogoro.
“Waliokufa ni dereva
wa gari dogo Meja Edward Mosi ambaye ni ofisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ) kikosi cha Kinonko na mkaguzi Msaidizi wa Polisi wa wilaya ya Korogwe
mkoani Tanga Johnson Zakaria,” alisema Matei.
Aidha alisema katika ajali hiyo mtu mmoja alijeruhiwa na
kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi kwa ajili ya matibabu huku
miili hiyo nayo ikiwa hospitalini hapo kusubiri ndugu kwa ajili ya mazishi.
“Kutokana na ajali hiyo jeshi la polisi linamtafuta dereva wa
lori ambaye alikimbia mara baada ya tukio hilo, ili aweze kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria,” alisema Matei.
Mwisho.
Tuesday, June 10, 2014
WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUPIMA AFYA ZAO
Na John Gagarini, Kibaha
IDARA ya Afya ya Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani
imeanza uhakiki wa wafanyabiashara mbalimbali kama wamepima afya zao kwa mujibu
wa sheria ili watoe huduma hizo wakiwa na afya njema na endapo watashindwa
kufanya hivyo watafungiwa biashara zao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jana mjini Kibaha ofisa afya wa Halmashauri ya Mji
wa Kibaha David Vuo alisema kuwa wafanyabiashara hao pamoja na wamiliki wa
viwanda wanapaswa kuhakikisha watoa huduma wao wanapima afya zao.
“Utaratibu huu ni wa kisheria kwani hata wafanyakazi wa
serikali kabla ya kuanza kazi wanapaswa kupima afya zao na hii ni sheria ya
afya ya mwaka 2009 namba 169 kifungu namba 17ambapo kwa sasa maofisa afya wa
kata wanafanya uhakiki kuona zoezi hilo ili taratibu stahiki zichukuliwe kwa
wale watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo ,” alisema Vuo.
Alisema kuwa jambo hilo si geni kwani liko kisheria na
linawagusa wafanyabiashara wote na shughuli mbalimbali za wajasiriamali ambao
wanapaswa kufuata taratibu za kiafya.
“Lengo la kupima afya na kuhakikisha kuwa wahudumu hao
wanahudumia wateja wakiwa na afya njema na kama kuna atakayegundulika anapaswa
kutibiwa kwanza hadi atakapopona ndipo aendelee kutoa huduma na kutakuwa na
fomu maalumu itakayokuwa kwenye eneo la shughuli ili kuwatambua waliofanya
hivyo na wale watakaoshindwa hawataruhusiwa kuhudumiwa watu,” alisema Vuo.
Aidha alitaja magonjwa ambayo yanapimwa kuwa ni Taifodi,
Kuhara, Mkojo, magonjwa ya Kaswende, Gono, Kifua, magonjwa ya ngozi kama vile upele
na mengineyo.
“Suala la kupima virusi vya ugonjwa wa UKIMWI ni hiyari
ambapo upimaji wa magonjwa haya hayahusiani na kupima ugonjwa huo labda mhusika
atake mwenyewe ambapo upimaji huu utafanyika kwenye hospitali ya wilaya ya
Mkoani na kituo cha afya Kongowe,” alisema Vuo.
Ofisa afya huyo wa halmashauri ya Mji wa Kibaha alissema kuwa
kuhusiana na uchangiaji wa vipimo hivyo kila mhusika anapaswa kutoa kiasi cha
shilingi 5,000 kwenye ofisi ya kata kisha atapewa fomu kwa ajili ya kwenda
kupima ambapo alisema elimu ilishatolewa.
Alitaja biashara ambazo watumishi wake wanatakiwa kupima afya
zao kuwa ni mama na baba lishe, bekari, migahawa, hoteli, baa, nyumba za kulala
wageni, mashine za kusaga nafaka, maduka ya vyakula, mabucha, machinjio,
saluni, dobi, viwanda, wachoma chipsi, vilabu vya pombe za kienyeji,
wafanyakazi wa kampuni na vikundi vya ujasiriamali.
Saturday, June 7, 2014
WATAKIWA KUKABILIANA NA TABIA NCHI
WAKAZI wa wilaya za Bagamoyo mkoani Pwani na Pangani mkoani
Tanga wametakiwa kulinda misitu ikiwemo ile ya Mikoko iliyopo kandokando mwa
Bahari ya Hindi ili kuinusuru wilaya hiyo na athari zitokanazo na mabadiliko ya
Tabia Nchi.
Hayo yalisemwa na mkuu
wa wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi alipokuwa akifungua mafunzo ya juu ya namna
ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi kwa wajumbe wa kamati za mazingira
kutoka wilaya za Bagamoyo na Pangani mkoani Tanga.
Kipozi amesema kuwa watu wengi waliathirika na mvua kubwa
zilizonyesha ambazo zilileta mafuriko na kusababisha madhara yakiwemo ya watu
kufa, mazao yao kusombwa na maji, miundombinu ikiwemo ya barabara na madaraja
zilitokana na mabadiliko hayo ya Tabia Nchi.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi mratibu wa mafunzo hayo Dk
Beno Mnembuka ambaye ni mtafiti kiongozi kwenye mradi huo unaosimamiwa na Chuo
Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Ardhi,
Mamlaka ya hali ya Hewa na mtafiti mmoja toka nchini Norway amesema kuwa
mabadiliko ya Tabia Nchi pia yameathiri viumbe hai kama vile samaki.
Dk Mnembuka amesema kuwa viashiria vya mabadiliko ya Tabia
Nchi ni pamoja na mabadiliko ya misimu ya mvua, joto, upepo mkali wa Kasi na
Kusi, ukame, mafuriko ambapo hutokana na uharibifu wa mazingira ambapo ili
kukabiliana na madhara hayo lazima kurejesha uoto wa asili kwa kupanda miti na
kutoharibu vyanzo vya maji.
Naye meneja wakala wa
misitu Tanzania (TFS) wilaya ya wilaya Bagamoyo Charles Mwafute amesema kuwa
katika kutekeleza kwa vitendo washiriki wa mafunzo hayo walipanda miti ya
Mikoko eneo la ukubwa wa hekari mbili na nusu kwenye kijiji cha Kiharaka.
Mradi huo ambao utaisha mwezi Desemba mwaka huu unatekelezwa
kwenye vijiji vya Bumbwini, Kisakasaka Zanzibar, Magomeni, Kiharaka na Kondo
wilayani Bagamoyo, Matakani, Kipumbwi na Pangani Mjini wilaya ya Pangani.
Thursday, June 5, 2014
WABUNGE WA KATIBA WATAKIWA KUREJEA BUNGENI
WABUNGE wa Bunge Maalumu la Katiba ambao walisusia vikao vya
bunge hilo Mjini Dodoma wametakiwa kurejea kwenye mjadala wa marekebisho ya
katiba kwani kuendelea kususia ni sawa na kufanya uasi na usaliti kwa wananchi.
Wanapaswa kuheshimu mamalaka iliyopo kwa kulimaliza tatizo
lililopo kwa kutumia busara kwa kukaa chini kwa pamoja na kukubaliana na si kwa
kulalamika kwa kupiga kelele nje ya Bunge hilo ili suluhu ipatikane.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha Nabii Jofrey
John wa Huduma ya HAKI Ministry ya Kongowe Kibaha mkoani Pwani amesema kuwa
endapo wabunge hao wataendelea kususia bunge lijalo kama walivyosusa ni kwamba
watakuwa wanaihujumu nchi.
Nabii John amesema kususa na kulalamika nje ya bunge hilo ni
sawa na kuasi hali ambayo inaweza kujenga chuki na matokeo yake ni kuleta
mafarakano ambayo mwisho wake ni mbaya kwani urithi walionao Watanzania ni
amani na si vurugu
Nabii John amesema kuwa kusiwe na kundi ambalo linasusia
mchakato wa kuunda katiba hiyo mpya kwani ni moja ya njia ambayo inaweza
kusababisha kuvurugika kwa amani na litajenga roho za kuona kuwa wanaonewa.
Amesema kuwa haitapendeza kuona kuwa kuna wabunge wamekwenda
kwenye bunge hilo kwa ajili ya kuhujumu mchakato huo kwani watasababisha
kuvunja amani iliyopo ambayo imedumu kwa maiaka 50 tangu tulipopata uhuru hivyo
haipaswi kuvunjwa na kundi la watu.
Amesema kiongozi yoyote awe wa chama au sehemu yoyote
amechaguliwa na Mungu hivyo hapaswi kudharau mamlaka iliyopo madarakani ambayo
hata Mungu anaitambua.
Aidha amesema kuwa anaamini kuwa wabunge waliochaguliwa
kwenye bunge hilo la katiba ni wasomi hivyo wasijishushie heshima ya usomi wao
kwani wako pale kwa niaba ya wananchi na si kwa maslahi yao binafsi bali kwa
maslahi ya wananchi.
Amewataka waumini wa dini zote kufunga na kuomba kwa ajili ya
amani ya nchi ili Mungu aepushe roho ya umauti katika nchi yetu ambayo
inanyemelea kutokana na sababu ambazo
zinaweza kuzuilika za kumaliza tofauti ndogo ndogo zilizopo.
Ameiomba serikali kuwatumia viongozi wa dini kama sehemu ya
kudumisha amani ya nchi kwa kuwafanyia maombi viongozi waliopo madarakani ili
waweze kuongoza kwa kutumia hekima za Mungu kwani bila ya kuwa na maombi hayo
shetani anaweza kuleta roho ya uchonganishi na kusababisha amani kutoweka.
Amebainisha kuwa kwa kipindi chote cha mwezi huu hadi ujao
watakuwa na kongamano kubwa la kuiombea amani ya nchi ambapo halitakuwa na
itikadi ya dini yoyote bali ni madhehebu yote hivyo kuwataka watu kujitokeza
kufanya maombi hayo.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)