Na John Gagarini, Kibaha
MABONDIA Said Seleman Ambokile Chusa wajijini Dar es Salaam
leo wanatarajia kupambana kwenye pambano la ngumi la kuwania ubingwa TPBO uzito
wa kati pambano litakalo pigwa kwenye ukumbi wa Container Maili Moja wilayani
Kibaha mkoani Pwani.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha moja ya
wasimamizi wa pambano hilo ambaye ni mwalimu wa ngumi Gordon Tambwe maarufu
kama Mawe alisema kuwa pambano hilo litakuwa kali na la kuvutia.
Mawe alisema kuwa lengo la kufanya pambano hilo Kibaha ni
kuhamasisha mchezo huo mikoani pia kuinua vipaji kwa mabondia wa mikoani ili
nao waweze kuonyesha uwezo wao.
“Tumeleta pambano hili Kibaha ili kuhamasisha mchezo wa ngumi
sehemu mbalimbali mikoani kwani michezo ni ajira na ngumi zimewasaidia vijana
wengi kujiajiri kupitia mchezo huo,” alisema Mawe.
Aidha alisema kuwa mabondia hao watapigana raundi 10 na pia
kutakuwa na mapambano ya utangulizi ambayo yatausisha mabondia kutoka mkoa wa
Pwani na wageni wao kutoka Jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Seleman alisema kuwa amejiandaa ipasavyo na
anatarajia kummaliza mapema mpinzani wake kwa KO kwani hatakuwa na muda wa
kupoteza katika kumaliza pambano hilo.
Naye Chusa alisema kuwa amekwenda Kibaha kwa ajili ya
kutafuta ubingwa na si kutalii na anatarajia kumpiga mpinzani wake ili kuwapa
raha wapenzi wake hivyo wasiwe na wasiwasi. Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa diwani
wa Viti maalumu Selina Wilson.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment