Na John Gagarini, Mkuranga
Abdala ambaye alikuwa akiishi na wenzake wawili wenye ulemavu
huo akitokea mkoani Morogoro huku wenzake Tabora kwa lengo la kuepuka vitendo
vya kushambuliwa na watu ambao wamekuwa wakiwa kata viungo au kuwaua hali
iliyowafanya wakae huko chini ya Shirika la Under The Same Sun.
Akizungumza mbele ya mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist
Ndikilo, Samwel Masaga alisema kuwa mwenzao aliondoka siku hiyo majira ya jioni
kwenda kutembea lakini hakurudi tena hadi wakati anatembelea mkuu huyo.
Masaga alisema kuwa mwenzao alikuwa na tabia ya kutoka na
kutembetembea lakini wanashangaa ni kwa nini hajarudi na jitihada za kumtafuta
zimeshindikana licha ya kutoa taarifa sehemu mbalimbali ikiwa ni pamoja na
polisi na ofisi ya mkuu wa wilaya.
“Tunasikitika kupotea kwa mwenzetu na hatuji tutampataje
tunaomba vyombo vinavyohusika vitusaidie ili mwenzetu aweze kupatikana kwani
hatujui mwenzetu nini kimemsibu kwani ni muda mrefu umepita hakuna taarifa
yoyote juu yake,” alisema Masaga.
Alisema kuwa mazingira wanayosihi kwa bahati mbaya hayana
ulinzi wowote lakini wamekuwa wakiishi vizuri na wenyeji wao ambao waliwapokea
vizuri na wamekuwa wakiishi vizuri bila ya matatizo ila hawajui mwenzao yuko
wapi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Kijiji hicho Hassan Kafeni
alisema kuwa walemavu hao wako hapo tangu mwaka 2014 na ni wa awamu ya pili
baada ya awamu ya kwanza kukaa hapo kisha kuondoka ndipo walipoombewa hao wakae
hapo ili nao waishi kama wanakijiji.
Kafeni alisema kuwa Abdala tangu alipopotea walifanya
jitihada za kumtafuta lakini hata hivyo hawajamwona na bado wanaendelea
kumtafuta hadi watakapompata na wameshangazwa na tukio la kupotea kwake.
Kutokana na hali hiyo mkuu wa mkoa wa Pwani injinia Evarist
Ndikilo alisema kuwa shirika hilo linapaswa kuangalia upya namna ya kuwatunza
watu hao kwani mazingira waliyopo usalama wake ni mdogo.
Ndikilo alisema kuwa shirika hilo linaonyesha lina nia nzuri
lakini mazingira waliyopo si salama sana kwani hakuna ulinzi wa kutosha hali
ambayo imesababisha Abdala kupotea na kuwataka kuwahamishia sehemu nyingine.
“Nawashauri wawatafutie sehemu nyingine ya kuishi kwani pale
walipo hakuna usalama kwani kama mtu anania mbaya ni rahisi kuwazuru kwani
serikali inataka waishi kwenye mazingira yenye usalama wa maisha yao,” alisema
Ndikilo.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi alisema
kuwa Jeshi hilo linaendelea na msako wa kumtafuta Abdala na watahakikisha
wanamtafuta hadi wanampata ili aungane na wenzake waishi kama kawaida.
Mushongi alisema kuwa ushirikiano na wananchi utasaidia
kupatikana kwake hivyo watoe ushirikiano ili kufanikisha Abdala kupatikana
kwani jambo hilo si la kawaida kutokea na kuwataka wananchi kuwalinda Albino
kwani nao wana haki ya kuishi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment